Jamaa anataka kupima DNA na mtoto

Jamaa anataka kupima DNA na mtoto

huggies

Member
Joined
Jul 1, 2014
Posts
54
Reaction score
1
Nimerudi tena. Yule baba wa mtoto anataka dna alfu kumbe ana mtoto mwingine nimechanganyikiwa.
 
we nae una kiherehere, unachanganyikiwa nini sasa?

Kwani akiwa na mtoto unakatika wapi?

Kama anataka kuhakiki, mwache ajiridhishe, tena muda huu ungemwangalia tu afanye maamuzi yake. Hata mie ningehakiki, mimba ya kuambiwa ina miezi sijui saba?!

Utapata kwashakoo ya uzazi bure.
 
we nawe hatukuelewi,unachanganyikiwa na nini? Si uliambiwa urelax? Au HUYO MTOTO SI WA HUYO BWANA??? Lea mtoto huyo ebo! Kama huna hela ya uji wa mtoto ni pm ntakupa so kulialia hapa kulilia huyo mwanaume !! Ka ulilikoroga ndo ulinywe!!
 
Unachanganyikiwa eeh? nina mashaka, haya tulia sasa unyolewe.
 
Kuchepuka kubaya aisee ona unavyopata shida sasa
 
Shoga husomeki kabisa. Hujasema kama una mimba yake hadi unakaribia kujifungua, akakutaa ukaja kulalamika hapa. Leo anataka akapime DNA unahara bata, ulichepuka au? Me nahisi ulichepuka afu ukapata mimba, na mwenye mimba akakukataa ndo dakika za mwisho ukaamua umbambikizie mimba kaka wa watu. Pole sana

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
hahahaaaaa kama nakuona vile unavyosoma hizi comment....

ndugu yangu mi nilidhani umechanganyikiwa mtoto kagoma kunyonya

we endelea kujifanya unachanganyikiwa na matendo ya baba yake maziwa yakauke hayo halafu urudi tena hapa hapa tukushauri jinsi ya kuyarudisha tena
 
hahahaaaaa kama nakuona vile unavyosoma hizi comment....

ndugu yangu mi nilidhani umechanganyikiwa mtoto kagoma kunyonya

we endelea kujifanya unachanganyikiwa na matendo ya baba yake maziwa yakauke hayo halafu urudi tena hapa hapa tukushauri jinsi ya kuyarudisha tena
No am so careful na mtoto she is ok na maziwa yana toka sana kiasi kwamba mtoto akiwa kalala mda mrefu yana ni mwagikia.
 
Nimerudi tena. Yule baba wa mtoto anataka dna alfu kumbe ana mtoto mwingine nimechanganyikiwa.

Dada ulishaambiwa DNA kiboko yao - pumba kule, mchele huku.
Kama anataka DNA wewe tatizo lako ni lipi endapo una uhakika mimba ni yake?
Jumuiya ya wana JF hawana msaada tena kwako. Kubali DNA ikigoma bila shaka utajua la kufanya. Kama wapima oil walijuwa wengi kubali kuwajibika!
 
No am so careful na mtoto she is ok na maziwa yana toka sana kiasi kwamba mtoto akiwa kalala mda mrefu yana ni mwagikia.

sasa endelea kujipa stress za ajabu ajabu tu halafu baada ya wiki mbili uone kama tukikuuliza jibu litakuwa hilo hilo
 
Hapo ndio utaelewa maana ya "mchepuko sio dili baki njia kuu".

Wewe hata raha ya mtoto huna maana tangu juzi ujifungue unachanganyikiwa tu
 
Dada ulishaambiwa DNA kiboko yao - pumba kule, mchele huku.
Kama anataka DNA wewe tatizo lako ni lipi endapo una uhakika mimba ni yake?
Jumuiya ya wana JF hawana msaada tena kwako. Kubali DNA ikigoma bila shaka utajua la kufanya. Kama wapima oil walijuwa wengi kubali kuwajibika!
Isije ikawa anajifanya anataka dna lakini kumbe anataka kufanya mambo ya tamthilia kubadilisha damu huko hospitali ionekane sio yake au wapange na hao watu wa lab ndo maana nimechanganyikiwa sabubu nikimwambia sitaki nitampa nguvu.
 
Isije ikawa anajifanya anataka dna lakini kumbe anataka kufanya mambo ya tamthilia kubadilisha damu huko hospitali ionekane sio yake au wapange na hao watu wa lab ndo maana nimechanganyikiwa sabubu nikimwambia sitaki nitampa nguvu.

DNA kwa ufahamu wangu inapimwa kwa mkemia mkuu wa serikali. Huo ujanja ujanja sidhani kama unaweza kufanyika. Wakati wa kupima nenda na ndugu unayemwamini. Kwanza hawapimi bila ushauri nasaha
 
we nawe hatukuelewi,unachanganyikiwa na nini? Si uliambiwa urelax? Au HUYO MTOTO SI WA HUYO BWANA??? Lea mtoto huyo ebo! Kama huna hela ya uji wa mtoto ni pm ntakupa so kulialia hapa kulilia huyo mwanaume !! Ka ulilikoroga ndo ulinywe!!
nipe mimi hiyo hela nipike uji wa futari lol
 
Back
Top Bottom