Jakaya Kikwete: Walimu wa Masters wafundishe shule za msingi

Cashman

JF-Expert Member
Jun 8, 2018
2,298
3,972
Nimeona mahali fulani Rais Mstaafu akisema tunakwama wapi hadi sasa kuna walimu wa daraja la 3A.

Yeye akifikiri kuwa suala hilo ni mindset tu ya watunga sera lakini ni suala linalowezekana.
na mimi namuunga mkono kuwa suala hili linawezekana sana iwapo serikali itajali maslahi ya elimu.

Wale wamama wanaofundisha KKK huku wakiimba na kuruka kwenye madarasa ya vumbi ama chini ya mti,Mungu awabariki sana. Kuna viongozi wanaamini wamama hao hawana masters kwa sababu ni vilaza.Lakini elimu ya Tanzania imefanywa kama anasa.

Wako watu wengi wameshindwa kufikia malengo yao ya elimu kwa sababu ya gharama za masomo.

Wafanye kutoa scholarships kwa kila mtu anayetaka kusoma hasa walimu hao wanaowaita wa daraja la 3A waone kama kuna mtu ataishia hapo alipo.

Pia nimeshangazwa na mtu kama yeye aliyewahi kuwa Rais hajui kuwa maslahi ndiyo chanzo cha kuwa na walimu wenye kiwango kidogo cha elimu.Serikali iweke kiwango cha mshahara wa milioni 3 kwa mtu mwenye masters anayefundisha shule ya msingi washangae jinsi walimu watakavyojitokeza kujiendeleza na watazipata hizo masters.

Pia ijaribu kuajiri walimu wa masters kwa mshahara wa laki 4 na kuwapeleka vijijini iwapo watawapata.Wakiwapata watakopa na kununua boda boda na wataacha kazi na kuwa waendesha boda. Mwendesha boda ana uhakika wa kupata laki 6 akiwa mvivu sana hadi milioni 1 kwa mwezi akijituma kazini.

Mwisho nadhani tuna mitaala ya kipumbavu sana ambapo tunayofundisha ujinga mwingi kupoteza muda badala ya kufundisha mambo ya msingi yanayoweza kutatua changamoto zetu.

Hii mitaala ni kuanzia shule za msingi hadi vyuo vikuu. Haya yote yanahitaji Rais mwehu kabisa kufuta huu upumbavu.
Kwa wagombea wanajitokeza sasa sijaona mtu mwenye fikra kama hizi.

Tunapaswa kuanza upya kabisa na kufikiri kwa namna yetu.Tuchague kwa umakini sana vitabu vya kusoma. Tuache mawazo ya wajinga wanaoamini elimu mfumo wa kubagua watu waliofeli na kuwaita hawana akili na waliofaulu kuwaita wana akili.

Tukiingia mtaani unakutana na wasio na akili ndio matajiri wenye akili ni wezi wa mali za umma na wauza nchi kupitia dili za mikataba.Wasomi wakitunga sheria kujipendelea na kutumia vyombo vya dola kulinda maslahi yao.

Wasomi wetu wanatengeneza kama kundi la kigaidi ili kuendelea kuwatawala wengi.Watachukua kodi zao,watazitumia wapendavyo na kurudisha ziada kwa walio wengi.
Turudi tufikiri upya tukitaka kuwa wakweli.
 
Serikali ya Tanzania elimu na afya sio kipaumbele chake
Sehemu zote mbona wanalegalega bora hata huko kwenye afya na elimu kidogo Kuna matumaini, hebu cheki kwenye kilimo na mifugo yaani mpaka leo 2023 lakini sheria ya kuhusu afya ya mifugo haifanyi kazi na kumbuka kwenye kilimo na mifugo ndo kumetoa ajira nyingi na kuchangia kwa kiasi kikubwa Pato la taifa
 
Hoja nzuri ya rais mstaafu Jakaya Kikwete maana Finland walimu wengi wa ngazi ya watoto wa vidudu na darasa la 1 & la pili wana PhD na masters sababu kuu ni kuwajengea msingi mzuri wa elimu kwa watoto wa umri wa miaka 3 - miaka 6 masomo yote mapema.
Teachers are considered equivalent in status to doctors and lawyers in Finland
 
Masters sio tatizo, tatizo ni kwenye malipo, ndiyo maana profesa wa chuo anakwenda kuwa mbunge anajua ndani ya miaka mitano malipo anayopata asingepata hata kama angefundisha miaka 80. Serikali iboreshe masilahi ya walimu alafu waone kama hizo masters hazito fundisha shule za msingi. Kupanga ni kuchagua.
 
Masters sio tatizo, tatizo ni kwenye malipo, ndiyo maana profesa wa chuo anakwenda kuwa mbunge anajua ndani ya miaka mitano malipo anayopata asingepata hata kama angefundisha miaka 80. Serikali iboreshe masilahi ya walimu alafu waone kama hizo masters hazito fundisha shule za msingi. Kupanga ni kuchagua.
[/QU


Umesomeka sana
 
boresha mshahara wa waalimu na marupurupu yao ili uone kama walipata Div One za form 6 hawatajiunga na vyuo vya ualimu badala ya kwenda University.
 
Masters zinabadili uwezo wa mwalimu? Mtu anapata masters lakini kufikra anajiona bado ni kama ana degree tu.
 
Tuache Siasa kwenye mambo ya Msingi, mengine yatajipa kuhusu nini kifanyike na kisifanyike, wadau / watunga Sera na through research na Continuous Improvement watagundua wafanye nini, vipi na kwa hatua zipi...

Hayo mambo ya nina nini (according to cheti chako) haimaanishi ufanisi..., unaweza ukawa una masters ya Quantum Physics ila Saikolojia na uvimilivu na wito hauna na unajiona upo under utilized hence not giving your all...

Narudia tena tuache Siasa kwenye mambo ya msingi....
 
Huyu jamaa si alikuwa raisi wa nchi hizi!hajui walimu hao hao ndo waliomfundisha hata yeye?alikuwa wapi kubadilisha hiyo mifumo akiwa raisi wa nchi hizi?ila sishangai sana hao ndo viongozi wetu wa nchi hizi.wakiondoka madarakani wakifanya ati washauri wazuri kumbe ni majitu ya hivyo tu.
 
Wanaombeza Mhe.Kikwete wengi wao wanaongozwa na Chuki na sio uhalisia na hizo Chuki wakizibadilisha kuwa mtazamo chanya wataona hoja za Mhe.Kikwete.

Kuna siku nilihoji kwenye Uzi wenye title kinachosema" maboresho katika utumishi wa Umma: Kwa nini watu wa "degree" wasiruhisiwe kuomba kazi za wenye "diploma" ? Mitazamo na maoni ya watu yaliegemea kwenye negativity.

Msingi wa hoja yangu ni kama msingi wa hoja ya Mhe. Kikwete umeegemea kwenye ujuzi ,vipaji na uwezo wa wenye elimu kubwa. Mtu mwenye elimu kubwa akitumiwa vizuri atasaidia kuleta tija na uboreshaji wa kitu na kufuta baadhi ya mitazamo hasi.

ninatamani sana mchakato wa ajira uruhusu wenye elimu za juu kuomba kazi za chini ya kada husika kama wakitaka
 
Tuache Siasa kwenye mambo ya Msingi, mengine yatajipa kuhusu nini kifanyike na kisifanyike, wadau / watunga Sera na through research na Continuous Improvement watagundua wafanye nini, vipi na kwa hatua zipi...

Hayo mambo ya nina nini (according to cheti chako) haimaanishi ufanisi..., unaweza ukawa una masters ya Quantum Physics ila Saikolojia na uvimilivu na wito hauna na unajiona upo under utilized hence not giving your all...

Narudia tena tuache Siasa kwenye mambo ya msingi....
Wachache watakuelewa. Handling ya watoto wadogo siyo mchezo
 
Tuache Siasa kwenye mambo ya Msingi, mengine yatajipa kuhusu nini kifanyike na kisifanyike, wadau / watunga Sera na through research na Continuous Improvement watagundua wafanye nini, vipi na kwa hatua zipi...

Hayo mambo ya nina nini (according to cheti chako) haimaanishi ufanisi..., unaweza ukawa una masters ya Quantum Physics ila Saikolojia na uvimilivu na wito hauna na unajiona upo under utilized hence not giving your all...

Narudia tena tuache Siasa kwenye mambo ya msingi....
Hayo yote ni matatizo ya mtumishi asiyelipwa vizuri. Ndiyo maana wadau wanasema, maokoto yaongezwe watu wa MA waende huko wakapambane. Hakuna wito bila mazingira mazuri ya kazi na posho +salary nzuri
 
Back
Top Bottom