Jacqueline Wolper anatamani kumpa penzi Rais

Ketoka

JF-Expert Member
Sep 23, 2015
1,091
1,922
Msanii wa filamu za Bongo Movie na mfanyabiashara Jacqueline Wolper amefunguka na kudai anatamani sana kama angetoa Penzi lake kwa Raisi.
Wolper amedai anaona ni bora kama atakuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi na Raisi yoyote Afrika kwani atakuwa salama zaidi kuliko kufaidi Penzi na wadanga wengine.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Wolper alisema mara nyingi amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na wanaume ambao mwishoni wanamsaliti jambo ambalo halipendi na linamkera, lakini anaamini akimpa moyo wake wa upendo Rais yeyote Afrika anaona atakuwa salama.

Unajua ndoto yangu mimi ningependa kutoa penzi langu kwa Rais maana najua kabisa, kwanza atakuwa ananiheshimu na itakuwa ni ngumu sana kunitenda kama wafanyavyo wengine na hapo nitatulia kabisa wala sitakumbuka wanaume wazugaji“.

Wolper amekuwa muwazi kuhusu maumivu anayokutana nayo Kwenye mapenzi yake ambapo uhusiano wake na staa wa Bongo fleva Harmonize uliisha baada ya kumuacha na Harmonize kuanza Mahusiano na sarah ambaye ana kipato kikubwa.

Screenshot_20180827-080107.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fursa hiyo kwa Jiwe aichangamkie ila Madam DC hatokubali kunyang'anywa tonge kirahisi, itabidi kujipinda na kuzungusha kama pangaboi ili kumtega zaidi Bw. Jiwe
Kweli pesa na madaraka ndio kila kitu maana kama Jiwe angekuwa dalali wa vyumba yombo Buza angekuwa anaishia kutongoza walevi wa gongo tu, leo hii warembo wanamtangazia fursa.
 
Back
Top Bottom