ITV wana agenda ya siri dhidi ya CHADEMA??

Watanzania tunaishi maisha magumu sana hatuna uhuru wa kweli! kituo cha Tv cha mtu binafsi lakini hakipo huru
 
Watanzania tunaishi maisha magumu sana hatuna uhuru wa kweli! kituo cha Tv cha mtu binafsi lakini hakipo huru

Kweli hakipo huru ila ni utumwa uliofungamana na biashara zenye ukungu na ukwepaji wa kodi, wangekuwa ni wafanyabiashara huku kusingekuwa na haja ya kulambalamba miguu na kujipendekeza.
 
Baada ya kufuatilia kwa makini mwenendo mzima wa kampeni huko Arumeru na hali halisi ya upepo wakisiasa unavyovuma, ITV tofauti na TBC wameshafanya tathmini na kugundua kuwa CHADEMA itashinda kwa kishindo hivyo wakaona wasije wakaonekana wamechangia kuinenepesha CDM na baadae wakaingizwa kwenye report ya majumuisho ya ccm baada ya kushindwa kuwa nao walichangia ushindi wa CHADEMA na baada ya hapo TRA au TCRA wakatumwa pale kutafuta sababu ili wasulukubiwe. TBC wao kwa habari zisizo rasimi sana kwa sasa wanapokea maelekezo kutokea Lumumba hasa kwa vijana ambao ofisi yao wamejengewa ghorofa jipya na mbele yake kuna ile barabara inayoelekea Legency hopsital. Mpaka hapo CDM haina promo kwenye nyanja hiyo but still inafanya vema. Bravo CHADEMA na MAKAMANDA WOTE WALIOKO MSTARI WA MBELE! Hakuna kulala mpaka kieleweke!
 

Hizo ni njama za ccm za siku nyingi na zinaelekea ukingoni sasa
 
Lakini hii haitawasaidia; maana wapiga kura wapo Arumeru na uhalisia wa mambo uko huko! kuchakachua picha haibadilishi msimamo wa wana wa Arumeru!

Nadhani magamba bado hawajalitambua hilo mpaka sasa
 
almost kila chaguzi huwa inategemewa chadema kushinda kwa vishindo na kila matokeo yakitoka vocabulary ya kuchakachua inazaliwa!!! cdm wamekuwa kwenye game tangu 92........mawakala wao

1. wanakagua masanduku
2. wanasimamia kura
3. wanahesabu kura
4. wanasign matokeo

matokeo yakija CCM wanakuwa wameiba kura???

kuna mchezo mchafu hapa ambao mnachezewa na hawa wanasiasa!! soon to be revealed
 
almost kila chaguzi huwa inategemewa chadema kushinda kwa vishindo na kila matokeo yakitoka vocabulary ya kuchakachua inazaliwa!!! cdm wamekuwa kwenye game tangu 92........mawakala wao...matokeo yakija CCM wanakuwa wameiba kura???
Jaribu kutafuta vocabulary ya kuchakachua ilizaliwa lini na kwa nini. Je, umefuatilia chaguzi ndogo ndogo zilizofanyika huko Mbeya hivi karibuni? Kuna moja imerudiwa mara tatu, sababu? Ambaye hatakiwi kushinda, kashinda! Mara zote msimamizi kapata kigugumizi kutangaza, chaguzi ikabidi zirudiwe! Je zingekuwa chaguzi kubwa? For every mistake made, so much knowledge is gained!
kuna mchezo mchafu hapa ambao mnachezewa na hawa wanasiasa!!
Jaribu kufuatilia kesi inayoendelea huko Segerea. Ukweli ulio mchungu ni kuwa Chadema haina dola, haina polisi, haina tume na haina Tendwa. Hakuna mchezo mchafu zaidi ya ule auchezao anayeamini yeye ni gwiji kumbe hawezi hata kutambua kuwa ngoma yenyewe anayocheza bado hata haijaanza, lakini, yeye huyo...! keshalowa jasho hadi utosini!
soon to be revealed
Jaribu kufuatilia mijadala humu JF, revealers mizuka wanajitokeza wengi tu karibu kila siku, what is one or two more, you are very welcome! Lakini taratibu hatua zinapigwa, baada ya kuuchapa usingizi kwa miaka 50, ukiamshwa lazima upate taabu kidogo kuzoea mazingira utakayoyakuta. Wapo ambao mwanga watakaoukuta unaweza kuwafanya wasione wakaamini bado wamelala kumbe ndio wamepofuka moja kwa moja.
 


Good grammar but biased and personalized arguments.
 
Magwanda kila mtu anawaonea nyinyi, sasa hao wapiga kura kwanini na wao wasiwaonee?

peleka umagamba wako huko...inamaana wewe uonevu unaoendelea hapa nchini kwa hiv vyombo vya habari yaani hata televishen ya taifa ni bure tu.
 

Kuna uhusiano mkubwa sana wa milango yote ya fahamu (mgomo, masikio, ngozi, macho, pua). Inwezekana kabisa matusi yanayosemwa na CHADEMA majukwaani yakafanya milango yako ya fahamu ikashindwa kkuwasiliana na kusababisha ubongo wako kushindwa kutafsiri vizuri na matokeo yake ni kuwa mtazamo hasi kwa vyombo vyetu vya habari vinavyofanya kazi kwa ufasaha kabisa.
 

Unapoanza kuandika angalau uwe na ulinganisho wa kile uandikacho, kama ITV hawaonyeshi mambo ya CCM mbona hujasema TBC ambao tangu kampeini kufunguliwa wanatangaza habari ya CCM pekee au hakuna vyama vingine huko Arumeru Mashariki?
Fungua kituo chako utangaze hizo habari ambazo ITV haitangazi.
 


kama taarifa ya habari ya tar 19/03 ndo imenifurahisha kweli, na ndo nmeona huo upuuzi wa kukwepesha kamera, ni bora wasiwe wanaonyesha kuliko kutuonyesha uongo
 
Kwa wale Ndugu milomstari wa mbele wa mapambano......namaanisha on ground Arumeru Mashariki mnaweza kufanya jambo moja nalo linaweza kuwaaibisha hawa magamba....kwenda kwenye campaign za magamba chukua picha kila eneo wanalokuwepo....halafu unapost hapa kwenye jukwaa huru....na kuuelezea umma hiyo ilikuwa wapi...Tosha sana na aibu kubwa kwa vituo vya Tv ambavyo haviko huru.....
 

Mkuu, please remember kituo cha ITV nicha mtu binafsi, yeye ndiye mwenye sauti ya mwisho kwa lipo lionyeshwe, na lipi liwekwe kapuni. Kwa bahati nzuri JK ametoa uhuru wa makampuni chungu nzima kuhanzisha vituo vyao vya TV; kama unaona ITV haikidhi kiu yako switch kwenye vituo vingine au better still ishauri CHADEMA ifanya mpango wa kuhanzisha kituo chao kabla ya 2015.
 

the highlighted words are highly appreciated
 

mkuu umeongeamengi, umespeculate vitu vingi, mpaka kunisema thread nyingine...always against me

ninachotaka kusema ni rahisi sana lakini chenye umuhimu sana

CCM wanafanya mambo kwenye kutengeneza hizi karatasi, how and how and how ndilo swala ambalo lina hitaji kuwa revealed,,,,

mengine yote umeandika ni utumbo tu au umeandikiwa na mkeo! it was irrelevant reply to my post! grow up
 
Mujwahuzia:
Naomba niwakumbushe Wtz kuwa shirika la Utangazaji (TBC)nchini ni chombo cha habari kwa Watanzania wote bila kujali rangi chama chochote cha siasa lakini kwa muda mfupi chombo hiki sasa kimegeuka kuwa chmbo cha Chama Cha Mapinduzi CCm hasa wakati wa kampeini za uchaguzi hili halina ubishi. kila mpenda habari analishuhudia hili jikite na Taarifa ya habari ifikako saa mbili usiku utaona chombo hiki kinavyoripoti matukio ya kila siku hata kama Mke wa rais alikwenda kwenye Bustani ya mchicha wao wapo tayali kuonyesha anavyo ufurahia mchicha lakini wasionyeshe maisha halisi yalivyo ili mradi wasikose cha kuonyesha umma watanzania kilichotokea tz wakati kuna mambo chungu nzima yanayogusa maisha ya walala hoi wa nchi hii hayaonyeshwi.Ndio kwa maana gwiji David Wakati aliachishwa kazi kwa sababu yeye alitakataa kuburuzwa na siasa uchwara za CCm ndugu zetu waliobaki TBC kwa sasa wanatetea kibarua kwa manaa kibarua ni kigumu wanamtumikia Kafiri wapate usingizi ndio kwa maana zinatangazwa habari za upande mmoja. lakini chadema yasonga mbeleeeeeeeeeeeeeeeeeeeee kwa P.power..........
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…