Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Hakuna shaka kwamba ifikapo mwaka 2015 au kabla ya hapo kutatokea mabadiliko makubwa sana ya kiuongozi Tanzania!
Lakini taswira iliyopo ni kwamba mabadiliko hayo hayataihusisha CCM ambayo yenyewe ndiyo inayotakiwa kuondolewa ili mabadiliko "yatokee". Kwa maana nyingine ni labda CCM yenyewe ibadilike kabisa (over hauling party System), jambo linaloonekana kwamba haliwezekani kutokana na minyukano ya kimaslahi iliyomo ndani ya chama hicho.
kwa hiyo tunapozungumzia mabadiliko yatakayotokea 2015 au kabla ya hapo tunazungumzia wakati huo huo kuondoka kwa CCM. Ni lazima tujitayarishe kuipokea uongozi CCM na kuhimili athari za kuondoka kwake, ziwe ni athari chanya au athari hasi. Watu wanaotaka tuamini kwamba CCM ikiondoka madrakani kutakuwa hakuna athari ni watu wanaotaka kutudanyanya.
KANU ilipoondoka madarakani nchini Kenye aliacha athari kubwa sana ya ukabila. Wakati wote ilipokuwa madarakani KANU haikushughulika kabisa na tatizo la ukabila nchini mwao. Hata USSR iliposambaratika athari za mfumo wa Kikomunisti inaonekana mpaka sasa. CCM kwa kukaa kwake madarakani kwa zaidi ya miaka 35 ni lazima mfumo wake uache madhara makubwa sana kwenye jamii yetu.
Sote tunakumbuka jinsi watu walivyovunja sheria (na bado wanavunja) bila kuchukuliwa hatua kwa sababu tu sehemu zao wanazofanyia shughuli wametundika bendera za CCM au wao wenyewe waliichangia CCM. Mali ngapi za umma ambazo zimechukuliwa na CCM zitarudishwa.
Ukiangalia kwa makini utaona baada ya kuondoka kwa CCM kuna kazi ya kufanya. Kuna kazi ya kubadilisha mfumo mzima wa jinsi ya kuendesha mambo na kila raia awajibike na kuepusha chama kutawala serikali. Watu wote walipe kodi na wanaokabiddhiwa jukumu la kuchunga kodi na kupanga matumizi yake ni lazima wahahakishe wanatimiza wajibu wao.
Lakini taswira iliyopo ni kwamba mabadiliko hayo hayataihusisha CCM ambayo yenyewe ndiyo inayotakiwa kuondolewa ili mabadiliko "yatokee". Kwa maana nyingine ni labda CCM yenyewe ibadilike kabisa (over hauling party System), jambo linaloonekana kwamba haliwezekani kutokana na minyukano ya kimaslahi iliyomo ndani ya chama hicho.
kwa hiyo tunapozungumzia mabadiliko yatakayotokea 2015 au kabla ya hapo tunazungumzia wakati huo huo kuondoka kwa CCM. Ni lazima tujitayarishe kuipokea uongozi CCM na kuhimili athari za kuondoka kwake, ziwe ni athari chanya au athari hasi. Watu wanaotaka tuamini kwamba CCM ikiondoka madrakani kutakuwa hakuna athari ni watu wanaotaka kutudanyanya.
KANU ilipoondoka madarakani nchini Kenye aliacha athari kubwa sana ya ukabila. Wakati wote ilipokuwa madarakani KANU haikushughulika kabisa na tatizo la ukabila nchini mwao. Hata USSR iliposambaratika athari za mfumo wa Kikomunisti inaonekana mpaka sasa. CCM kwa kukaa kwake madarakani kwa zaidi ya miaka 35 ni lazima mfumo wake uache madhara makubwa sana kwenye jamii yetu.
Sote tunakumbuka jinsi watu walivyovunja sheria (na bado wanavunja) bila kuchukuliwa hatua kwa sababu tu sehemu zao wanazofanyia shughuli wametundika bendera za CCM au wao wenyewe waliichangia CCM. Mali ngapi za umma ambazo zimechukuliwa na CCM zitarudishwa.
Ukiangalia kwa makini utaona baada ya kuondoka kwa CCM kuna kazi ya kufanya. Kuna kazi ya kubadilisha mfumo mzima wa jinsi ya kuendesha mambo na kila raia awajibike na kuepusha chama kutawala serikali. Watu wote walipe kodi na wanaokabiddhiwa jukumu la kuchunga kodi na kupanga matumizi yake ni lazima wahahakishe wanatimiza wajibu wao.