Itakuwa kibao cha jeshi hakukiona...

Itakuwa kibao cha jeshi hakukiona...

Wewe mtoto umeanza kuendesha gari juzi gari yenyenye unaweka D unasongo mbele R unarudi nyuma
Miaka 30 niko barabarani sijui nini utanidanganya nimeendesha Pulling kwa miaka 9 na sidhani kama ulikuwepo duniani au ulikuwa bado kwenye zipu ya baba yako
Mzee bado utaalamu wako wa kizamani kama mpk leo hii reverse lazima utoe kichwa bado sana bora upumzike tu
 
Kijana kutoa kichwa nje si kwamba nilishindwa kurudi revarse la hasha ni ubovu wa barabara ndiyo maana mjeda aliamua kunikomoa kwa kuniambia nitumie sidemirror mwanzo mwisho kingine kumbuka kuna sehemu ukiwa unarudi nyuma lazima kuwe na mtu wa kukuelekeza haswa kwa gari kubwa Pulling usinichukulie poa kijana
 
Hawa jamaa nuksi kweli niliingia kambini kwa mbwembwe na gari la kuazima napiga honi karibu na maeneo ya hospital yao akaja mmoja ananiambia chagua moja
Uruke kichura mpaka ulikotoka na urudie gari lako kwa kichura kutokea huko au urudi kwa Rivasi mpaka barabara kuu piga hesabu sasa ngoma uichekeche kutoka pale hospitalini mpaka barabara kuu nilikoma mbona na nimesimamiwa mpaka barabara hakuna kutoa kichwa nje tumia sidemirror

Sasa kurudi reverse na Gari nayo ni adhabu? Mbona rahisi sana mkuu???
 
Siyo adhabu mkuu ila barabara yenyewe ilikuwa ni adhabu tosha kumbuka hapo ni mwaka 96 palikuwa hovyo hovyo tu makorongo ya kufa mtu kuna sehemu barabara imekatika unatoa kichwa kuchungulia ili uendelee na safari jamaa anakumbia ukichungulia tu unaanza mwanzo ikabidi nirudi kiubishi mpaka mwisho halafu jamaa ananiambia na kesho uje kwa mbwembwe sawa dereva
 
Back
Top Bottom