ITAKUSAIDIA HII; Tips za jikoni nyumbani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
Ukimarinate nyama au samaki kwa viungo( vitunguu saum, tangawizi, masala) ongeza mafuta kidogo na mtindi vijiko viwili inalainika na kunoga
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Ukikosa vanila unaweza saga Ganda la limao bichi kuleta harufu nzuri kwenye keki au chapati za maji

Ukitaka kupika mboga ya karanga, saga karanga kisha tumia maziwa kukorogea karanga badala ya maji inanoga sana
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Chapat ukiógeza kdg nazi ya unga na ukakandia maziwa chapati inakuwa zaid ya nzuri
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Ukitaka chips au ndiz ziwe nzuri, chemsha kdg dk 5 ipua zichuje maji then weka kwenye freezer.

Ukitaka kukaanga toa pasha mafuta choma usisubiri zitoke barafu, utastaajab radha yake
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Ukiunguza wali penyeza mapande makubwa ya pilipili hoho ndani ya wali huwa inaondoa kabisa harufu ya kuungua
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Ukiona mafuta yamekuwa mengi kwenye supu au mchuzi tumia mkate wa siles kupitisha juu kufyonza
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Ukitaka maharage yawe na rojo zuri,baada ya kubandika tia mafuta ya kupikia yaivie pamoja
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Ukitengeneza juice ya rosela au ubuyu unaweza weka mchaichai pale unapochemsha juice inavutia sana

Chapati ikilala ukitaka kuipasha iwe lain ichove kwenye maji baridi na kuitoa then pasha kwenye frypan bila mafuta..itakuwa kama umepika leo
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Ukipika matembele ukiweka tangawiz na pilipili manga yanakuwa matamu balaa
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Juice ya parachichi weka ndimu au limao utaipenda
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Ukitaka samaki wabichi wasivurugike au kung'ang'ania wakati wa kukaanga. Wapake unga wa ngano wakolee halafu kaanga ni watamu mno
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Ukitaka kubadili pishi la wali weka kitungú maji, saumu na iliki kdg wkt wa kuchemsha maji then yachuje halafu pika wali wako unanukia balaa
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Kama unatumia gesi kupikia wali, jaribu tumia maji ya baridi kupikia mchele unanoga hasa
upload_2017-8-23_16-19-23.gif


Ukitaka utumbo uive haraka weka limao pekee bila chumvi kwa yake maji ya kwanza.
 

Attachments

  • upload_2017-8-23_16-19-23.gif
    upload_2017-8-23_16-19-23.gif
    42 bytes · Views: 193
  • upload_2017-8-23_16-19-23.gif
    upload_2017-8-23_16-19-23.gif
    42 bytes · Views: 178
  • upload_2017-8-23_16-19-23.gif
    upload_2017-8-23_16-19-23.gif
    42 bytes · Views: 174
  • upload_2017-8-23_16-19-23.gif
    upload_2017-8-23_16-19-23.gif
    42 bytes · Views: 178
Kwenye wali mapande ya pilipili hoho unaikata kwanza au unaeka nzima? pia unaeza kueka kitunguu maji katikati ya sufuria kukata harufu ya kuungua.
 
Hapo kwenye gesi kupikia wali, maji ya baridi kivipi? fafanua.
Mchele ukishauosha, unauweka kwenye sufuria ya kupikia, kisha unatia maji yasiyochemchwa (baridi),chumvi na mafuta,koroga vizuri kisha bandika sufuria yako jikoni ikiwa imefunikwa vizuri!


Ni vizuri usigeuze wali mpaka maji yatakapokuwa yamekauka. Ila kumbuka kupunguza moto kwa kadri maji yanavyozidi kukauka
 
Mchele ukishauosha, unauweka kwenye sufuria ya kupikia, kisha unatia maji yasiyochemchwa (baridi),chumvi na mafuta,koroga vizuri kisha bandika sufuria yako jikoni ikiwa imefunikwa vizuri!


Ni vizuri usigeuze wali mpaka maji yatakapokuwa yamekauka. Ila kumbuka kupunguza moto kwa kadri maji yanavyozidi kukauka
Asante sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom