Life2
JF-Expert Member
- Jun 8, 2016
- 3,377
- 4,847
Miaka inakimbia kama Tuisila Kisinda/Tk Masta hainisubiri sababu mimi sio special hata ningekua special isingeweza nisubiri.
Ukija kwenye sekta ya mahusiano nako ni afadhali ya jana kuliko leo sijui ndio kusema mtu kadandia mtumbwi wa... kila sehemu nakula za kichwa, nikienda kwa yule ananiambia yupo kwenye mahusiano yake na mwezi ujao anaolewa, nikienda kwa X wa zamani ananiambia sorry ulichezea bahati for now i have 3 kids na tunapendana na baba watoto wangu sana tena futa namba yangu.
Nafikiria sana je, niachane na mambo ya beb mamas na nijikite kwenye kutafuta mapene aka shekeri kidogo natembea navutiwa na binti mrembo wa mitaa ya mbele napewa namba za simu charting ya kwanza hello hello, za kwako nzuri, tunaendelea ehee unajua flani ninakupenda naomba uwe rafiki yangu, message inayorudi unajua pale ninapoishi kodi inaisha mwezi huu kati ya laki 6 nina laki moja niongezee laki 5 dia ndipo naitwa dia kwa mara ya kwanza.
Jibu langu sina pesa kwa hiyo afta natuma sms kimya naenda dukani kwa masawe naweka vocha ya mia 5 napiga hakuna salamu majibu yake achana na mimi bahili wewe.
Nataka kulia ila nakumbuka kauli ile inasema wanaume tumeumbwa mateso kuhangaika natulia navuta pumzi najipa moyo.
Nakuja Jf kwa watu wenye IQ kubwa kubwa naandika mada yenye kichwa cha habari “Natafuta mchumbwa wa Kike sina vigezo vingi,“ nako sipati mtu.
Sasa hapa najiuliza kwani kosa langu nini mbona mapenzi hayanitaki japo mimi nayataka.
Hebu nanyi wana Jf mnishauri nikimbilie wapi mimi au kisa mimi mshamba au niache ushamba, nzuri mbaya nafikiria hapa.
Ukija kwenye sekta ya mahusiano nako ni afadhali ya jana kuliko leo sijui ndio kusema mtu kadandia mtumbwi wa... kila sehemu nakula za kichwa, nikienda kwa yule ananiambia yupo kwenye mahusiano yake na mwezi ujao anaolewa, nikienda kwa X wa zamani ananiambia sorry ulichezea bahati for now i have 3 kids na tunapendana na baba watoto wangu sana tena futa namba yangu.
Nafikiria sana je, niachane na mambo ya beb mamas na nijikite kwenye kutafuta mapene aka shekeri kidogo natembea navutiwa na binti mrembo wa mitaa ya mbele napewa namba za simu charting ya kwanza hello hello, za kwako nzuri, tunaendelea ehee unajua flani ninakupenda naomba uwe rafiki yangu, message inayorudi unajua pale ninapoishi kodi inaisha mwezi huu kati ya laki 6 nina laki moja niongezee laki 5 dia ndipo naitwa dia kwa mara ya kwanza.
Jibu langu sina pesa kwa hiyo afta natuma sms kimya naenda dukani kwa masawe naweka vocha ya mia 5 napiga hakuna salamu majibu yake achana na mimi bahili wewe.
Nataka kulia ila nakumbuka kauli ile inasema wanaume tumeumbwa mateso kuhangaika natulia navuta pumzi najipa moyo.
Nakuja Jf kwa watu wenye IQ kubwa kubwa naandika mada yenye kichwa cha habari “Natafuta mchumbwa wa Kike sina vigezo vingi,“ nako sipati mtu.
Sasa hapa najiuliza kwani kosa langu nini mbona mapenzi hayanitaki japo mimi nayataka.
Hebu nanyi wana Jf mnishauri nikimbilie wapi mimi au kisa mimi mshamba au niache ushamba, nzuri mbaya nafikiria hapa.
