Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,096
- 828,932
Niwapongeze mawakili walioenda South Africa kupambana hadi kufanikiwa kuirudisha ndege aina ya airbus mali ya serikali ya Jamhuri? Ya Tanzania.. Nawapongeza sana kwakuwa ni nadra sana kutokea mawakili wetu kushinda kesi za nchi hasa nje ya nchi
Angalizo muhimu kwao:
Wasibweteke wakalewa sifa... Hii fungate ya ushindi isiwe ndefu... Wajipange... Hii ngoma bado mbichi sana... Ndege imerudi lakini deni bado liko pale pale na linazidi kuongezeka kutokana na riba
Bwana stein kadhamiria... Hata kama hatakata rufaa south Africa bado kuna mahakama ya Africa anaweza kukimbilia huko na bado kuna mahakama ya haki za binadamu anaweza kukimbilia huko na kusajili upya kesi yake
Ameshalipwa za kutosha na pengine ameshaona hakuna dalili za kulipwa tena hivyo atakachofanya sasa ni kusumbua na kuharibu taswira ya nchi kimataifa...
Hii inaitwa NIGUSE UNUKE.. unamwaga mboga namwaga ugali...
Kipindi hiki cha fungate zitafutwe mbinu za kumalizana na mzungu kiroho safi ILI maisha yaendelee bila hofu... Hapa Tanzania vinapokamatwa vitu kwenye misako ya polisi watu hutangaziwa kwenda kuvitambua vitu vyao
Akikamatwa jambazi sugu wananchi hutangaziwa kwenda kumtambua...
Nina hofu wadeni wetu wanatafutana na kutengeza group za mawasiliano ILI siku mali yetu ikikamatwa popote watoke kila kona.... Tuna nafasi bado ya kulimaliza hili kabla madhara hayajawa mengi
Angalizo muhimu kwao:
Wasibweteke wakalewa sifa... Hii fungate ya ushindi isiwe ndefu... Wajipange... Hii ngoma bado mbichi sana... Ndege imerudi lakini deni bado liko pale pale na linazidi kuongezeka kutokana na riba
Bwana stein kadhamiria... Hata kama hatakata rufaa south Africa bado kuna mahakama ya Africa anaweza kukimbilia huko na bado kuna mahakama ya haki za binadamu anaweza kukimbilia huko na kusajili upya kesi yake
Ameshalipwa za kutosha na pengine ameshaona hakuna dalili za kulipwa tena hivyo atakachofanya sasa ni kusumbua na kuharibu taswira ya nchi kimataifa...
Hii inaitwa NIGUSE UNUKE.. unamwaga mboga namwaga ugali...
Kipindi hiki cha fungate zitafutwe mbinu za kumalizana na mzungu kiroho safi ILI maisha yaendelee bila hofu... Hapa Tanzania vinapokamatwa vitu kwenye misako ya polisi watu hutangaziwa kwenda kuvitambua vitu vyao
Akikamatwa jambazi sugu wananchi hutangaziwa kwenda kumtambua...
Nina hofu wadeni wetu wanatafutana na kutengeza group za mawasiliano ILI siku mali yetu ikikamatwa popote watoke kila kona.... Tuna nafasi bado ya kulimaliza hili kabla madhara hayajawa mengi





