Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Jamaa wawili walienda msituni kuwinda.Walipokuwa huko walifanikiwa kumuua swala mmoja.Wakiwa katika harakati za kumbeba,mara ghafla wakashambuliwa na nyati na mmoja wao kujeruhiwa vibaya.Jamaa mwingine akamtelekeza mwenzie aliyeumia na kumbeba swala na kurudi naye nyumbani.Alipoingia ndani akahojiwa kwa nini aliamua kumtelekeza mwenzie porini?.Jamaa akawajibu;"ningemwacha huyu swala angeibiwa na ndo maana nikaamua kumwacha jamaa kwa sababu hamna atakaye mchukua".