Is it just a game?

PetCash

JF-Expert Member
Mar 20, 2012
1,997
1,997
Ni ndoto ya mvulana wa kawaida(an average boy) anayekua ambaye hajafungwa kimaadili na kiimani(not commited moraly&spiritualy) kuwa na
msichana baada ya msichana kadiri atakavyoweza. Akitegemea kwamba kwa kuishi hivyo hatimaye umri ukifika atampata anayemtaka na kuwa naye
Kama mke …KWA UPANDE mwingine msichana huingia deeper emotionally kwenye haya mahusiano akitegemea kitu zaidi ya kubadilishwa
(It makes one always wonder-what more would u get off a relationship at 15/16 years of age?).
SO as they grow:
Mvulana/mwanaume atapata ufahamu kwamba si kweli kwamba kubadilisha wanawake ni rahisi kwa sababu kila uhusiano
una ‘emotional’ na ‘spiritual attachment’
Na kwenye hizo hatua za kuvunja hayo mahusiano much more is lost than they bargained for…
matokeo yake mioyo yao hulipa gharama za mahusiano hayo wakatiexperience ya mahusiano na maisha kiujumla ikipatikana.

Msichana/mwanamke ataumia baada ya muda mrefu wa kulea matarajio yasiyofikiwa (or should I say yasiyofikika?),
kwa sababu kwa wastani mwanamke atafanya maandalizi kabla ya mahusiano(yes-huwa ni mahusiano japokuwa kwa upande wa kiume siyo)…
Ila kwa jinsi mahusiano hayo yanavyovunjika hupata uzoefu na kuweza kuyachambua mahusiano vizuri zaidi kabla ya kuyaanza.


Mwisho wa siku;
Huyo ‘special one’ wa mwanaume inakuwa ngumu sana kupatikana na mara nyingi mke atatoka kwa yule msichana atakayekuwa
naye muda ukifika na wengine mpaka wategeshewe mimba ndio hukumbuka;
He, kumbe kuna kuoa?
Na baada ya kuoa inakuwa shida kubond na mkewe na familia kwa sababu mazoea ya miaka hiyo yote hayafutiki overnight.

Kwa mwanamke, well tukichukulia mambo yatabaki kawaida(hakuna uhitaji wa kutegesha mimba ama mimba isiyotarajiwa)
watakuwa na hao wanaume wanaowataka usually after along chase na kupambana na wenzie anamuweka ndani….
Only to realize that;
(i) if you chase someone wanting him so much u fail to asses viability or value of your object on run(is he worth it?)
because all you worry about is what if you don’t get him…
AND (ii) you can take the man out of the game but taking the game out of the man is a whole new mission.

CONCLUSION: kwenye hii safari tumewapoteza ndugu zetu(literally) –RIP brothers n sisters, wengine wamepata ajira(TACAIDS),
wengine wamevunjika mioyo na wengine wako tu hawaelewi kilichowapata over the years wakati kwa wengi life is life.

But in the beginning the man said, ‘LIKE FOOTBALL IT’S JUST A GAME’
Sasa mi swali langu ni, Is it just a game really?
 
Back
Top Bottom