Is God Evil? ( Je Mungu ni Muovu?)

Is God Evil? ( Je Mungu ni Muovu?)

WATU WA DINI UPO KUNDI GANI?

A. Viongozi (Elite): Kwa viongozi wa dini, wanasiasa, na watu wenye ushawishi mkubwa, dini ni mtaji mkubwa sana. Inawapa himaya za kifedha zisizolipa kodi, umiliki mkubwa wa ardhi, na kundi la watu wa kuwapigia kura bila kuhoji. Wanautumia mfumo huo kupata nguvu na utajiri wa hapa duniani.

B. Wafuasi (The Masses): Kwa muumini wa kawaida asiyenufaika kiuchumi wala kisiasa, faida pekee anayoipata ni ya kisaikolojia (faraja ya akili). Wao wanatoa fedha zao walizozitolea jasho (sadaka, zaka, michango) na muda wao wa maisha, wakibadilishana na ahadi za mambo yajayo wasiyoweza kuyaona kwa macho.

NYIE NDO HAMTAKI RAHA HAPA DUNIANI?
 
Malipo ya Baada ya Kifo: Kwenye ulimwengu wa biashara, ukifanya kazi unalipwa mwisho wa wiki au mwezi. Dini inatumia mfumo wa malipo yanayokuja baada ya kifo. Huu ni mfumo wa kibiashara wa kipekee sana kwa sababu mteja hawezi kurudi duniani kulalamika kuwa bidhaa aliyouziwa ina kasoro au hajapewa alichokiwania.

Mbaya zaidi dini Inakutengenezea Deni la Kisaikolojia: Wafuasi hufundishwa tangu utotoni kuwa wao ni wakosaji na wana deni kubwa mbele ya Mungu. Ili kulipa deni hilo la kiroho, wanatakiwa kuendelea kufadhili na kujenga majengo na himaya za kidini hapa duniani.
 
Interesting yet confusing.

Nafikiri kwa mustakabali wa ustawi wa kiumbe mwanadamu MUNGU angetakiwa kujidhihirisha kwa wanadamu kama tunavyosoma kwenye "vitabu vitakatifu". Angalau kila baada ya karne moja

Ila sasa kuna Mungu wa Buddhism na Hinduism nao inabidi wafanye mambo angalau waamini wapate CLEAR and ASSURANCE ya hicho tunacho amini.

Swali litaendelea kusimama kama vile ligi ya kuku na yai, nani kaja wa kwanza
 
Malipo ya Baada ya Kifo: Kwenye ulimwengu wa biashara, ukifanya kazi unalipwa mwisho wa wiki au mwezi. Dini inatumia mfumo wa malipo yanayokuja baada ya kifo. Huu ni mfumo wa kibiashara wa kipekee sana kwa sababu mteja hawezi kurudi duniani kulalamika kuwa bidhaa aliyouziwa ina kasoro au hajapewa alichokiwania.

Mbaya zaidi dini Inakutengenezea Deni la Kisaikolojia: Wafuasi hufundishwa tangu utotoni kuwa wao ni wakosaji na wana deni kubwa mbele ya Mungu. Ili kulipa deni hilo la kiroho, wanatakiwa kuendelea kufadhili na kujenga majengo na himaya za kidini hapa duniani.
Duh ur making a lot of sense.
 
Interesting yet confusing.

Nafikiri kwa mustakabali wa ustawi wa kiumbe mwanadamu MUNGU angetakiwa kujidhihirisha kwa wanadamu kama tunavyosoma kwenye "vitabu vitakatifu". Angalau kila baada ya karne moja

Ila sasa kuna Mungu wa Buddhism na Hinduism nao inabidi wafanye mambo angalau waamini wapate CLEAR and ASSURANCE ya hicho tunacho amini.

Swali litaendelea kusimama kama vile ligi ya kuku na yai, nani kaja wa kwanza
Yes kabisa mkuu upo sahihi
 
Back
Top Bottom