Iron Mike Tyson Vs Muhammad Ali

Chief Kumbyambya

JF-Expert Member
Jun 16, 2022
490
1,461
Wasalaam mazee,

Natumai muwazima wa afya tele kabisa na mambo yanakwenda sawa bin sawia.

Kipindi anapigana Muhammad Ali mimi sikuwepo lakini sababu ya mambo ya utandawazi uliopo sazi nimebahatika kuangalia mapambano mengi sana ya Muhammad Ali kama nikikuwepo vile na kiukweli jamaa alikuwa anajua na alizikonga nyoyo za mashabiki haswa.

Lakini pia nimebahatika kufuatilia mapambano mengi sana ya Mike Tyson ambayo sikuyaona lakini kwa msaada wa mtandao nimeyaona yote kama nilikuwepo vile wakati kwa umri wangu nimekuta Mike Tyson ndiyo anaishia ishia hivi lakini kupitia mitandao nimeyaangalia mapambano yake yote ya nyuma kama nilikuwepo vile.

Tuje Muhammad Ali Vs Iron Mike Tyson.

Wazee nafikiri Muhammad Ali anapewa heshima yake na kuangaliwa na wengi kama kivutio cha mchezo wa ngumi sababu yeye ndiye alisababisha mchezo huu kuanza kufuatiliwa na kuwa mchezo namba mbili wenye mashabiki wengi zaidi duniani ukitanguliwa na mpira wa miguu ambao ndio unashikilia nafasi ya kwanza.

Ila kuikweli Mike Tyson alikuwa anapiga ngumi mazee. Aisee ngumi za Mike Tyson zilikuwa zinasisimua mzee, yani mtu anakula kichapo mpaka unaeangalia kama una roho nyepesi unaweza kufunga macho usione mtu anavyokufa live.

Kwa upande wangu ukiwapambanisha hawa wawili kama wangekuwa katika era moja na kwa mapambano yao niliyoyaona wakipigana basi Muhammad Ali naamini angechakazwa vilivyo na Iron Mike Tyson. Tyson alikuwa na style yake hatari sana ya kupigana inayojulikana kama ”Peek A Boo.” Hii ni moja kati ya style ngumu inayowashinda mabondia wengi kuimaster hivyo ukimtoa aliemfundisha Tyson bwana D’Amanto hakuna bondia yeyote yule anayeiweza style hii zaidi ya Tyson mwenyewe.

Sijajua kama huu ni mtazamo wangu tu au kuna wengine wanaliona hili.

simshushi cheo Muhammad Ali, atabakia kuwa mtangulizi aliesababisha mchezo huu kupendwa na watu wengi zaidi ilaaaa narudia tena ilaaaaa Mike Tyson alikuwa anapiga ngumi bwana, wacha kabisa.
 
Kuna Mwamba alimpiga Ali alikua anaitwa Larry kama sijakosea na haukupita muda mrefu Ali alistaafu ndondi kutokana na afya yake kubadilika.Kipindi hicho Tyson ndo anachipukia na alimuahidi Ali kua atamlipizia kisasi kwa huyo mwamba, mwisho wa siku Tyson akakutana na Larry sikumbuki kama alimaliza round ya kwanza.
 
Kuna mkuu alileta post ambapo watu walikuja na maswali yanayofanana na ya kwako, yule mleta post akawa anawajibu kwa jinsi anavyoelewa yeye.
 
Kuna Mwamba alimpiga Ali alikua anaitwa Larry kama sijakosea na haukupita muda mrefu Ali alistaafu ndondi kutokana na afya yake kubadilika.Kipindi hicho Tyson ndo anachipukia na alimuahidi Ali kua atamlipizia kisasi kwa huyo mwamba, mwisho wa siku Tyson akakutana na Larry sikumbuki kama alimaliza round ya kwanza.
Ally.. hakustaafu ndondi kwasababu ya kuzorota kwa afya yake, fuatilia vizuri
 
Wasalaam mazee,

Natumai muwazima wa afya tele kabisa na mambo yanakwenda sawa bin sawia.

Kipindi anapigana Muhammad Ali mimi sikuwepo lakini sababu ya mambo ya utandawazi uliopo sazi nimebahatika kuangalia mapambano mengi sana ya Muhammad Ali kama nikikuwepo vile na kiukweli jamaa alikuwa anajua na alizikonga nyoyo za mashabiki haswa.

Lakini pia nimebahatika kufuatilia mapambano mengi sana ya Mike Tyson ambayo sikuyaona lakini kwa msaada wa mtandao nimeyaona yote kama nilikuwepo vile wakati kwa umri wangu nimekuta Mike Tyson ndiyo anaishia ishia hivi lakini kupitia mitandao nimeyaangalia mapambano yake yote ya nyuma kama nilikuwepo vile.

Tuje Muhammad Ali Vs Iron Mike Tyson.

Wazee nafikiri Muhammad Ali anapewa heshima yake na kuangaliwa na wengi kama kivutio cha mchezo wa ngumi sababu yeye ndiye alisababisha mchezo huu kuanza kufuatiliwa na kuwa mchezo namba mbili wenye mashabiki wengi zaidi duniani ukitanguliwa na mpira wa miguu ambao ndio unashikilia nafasi ya kwanza.

Ila kuikweli Mike Tyson alikuwa anapiga ngumi mazee. Aisee ngumi za Mike Tyson zilikuwa zinasisimua mzee, yani mtu anakula kichapo mpaka unaeangalia kama una roho nyepesi unaweza kufunga macho usione mtu anavyokufa live.

Kwa upande wangu ukiwapambanisha hawa wawili kama wangekuwa katika era moja na kwa mapambano yao niliyoyaona wakipigana basi Muhammad Ali naamini angechakazwa vilivyo na Iron Mike Tyson. Tyson alikuwa na style yake hatari sana ya kupigana inayojulikana kama ”Peek A Boo.” Hii ni moja kati ya style ngumu inayowashinda mabondia wengi kuimaster hivyo ukimtoa aliemfundisha Tyson bwana D’Amanto hakuna bondia yeyote yule anayeiweza style hii zaidi ya Tyson mwenyewe.

Sijajua kama huu ni mtazamo wangu tu au kuna wengine wanaliona hili.

simshushi cheo Muhammad Ali, atabakia kuwa mtangulizi aliesababisha mchezo huu kupendwa na watu wengi zaidi ilaaaa narudia tena ilaaaaa Mike Tyson alikuwa anapiga ngumi bwana, wacha kabisa.
Sikulaumu kwa kuamini kwamba Tyson ni bora kuliko Muhammad Ali. Mwenyewe umesema kwamba umeanza kufuatilia ngumi hivi karibuni.

Si kweli kwamba Muhammad Ali ndiye aliyefanya mchezo wa ngumi kuwa maarufu. Boxing ni mchezo maarufu duniani kabla ya era ya kina Ali. Jaribu kufuatilia historia utasikia watu kama kina Rocky Marciano, Joe Louis, Jack Dempsey, Sonny Liston, Floyd Petterson, Max Schmelling, Joe Walcot na wengieo ambao walikuwepo kabla Ali hajaja.

Njia bora ya kumlinganisha Tyson na Ali si tu kuangalia alishindaje bali pia alipigana na kina nani. Era ya kina Ali ilijaa boxers wenye uwezo mkubwa kuliko era ya Tyson. Ali alipigana na miamba kama Sonny Liston, Joe Frazier, Leon Spinks, Ken Norton, George Foreman na Ernie Shavers ambao wote ni Hall of Famers. Ukiondoa Evander Holyfield na Lennox Lewis, ambao wote walimpiga, Tyson alipigana na boxers wengi ambao walikuwa just average.
 
Kuna Mwamba alimpiga Ali alikua anaitwa Larry kama sijakosea na haukupita muda mrefu Ali alistaafu ndondi kutokana na afya yake kubadilika.Kipindi hicho Tyson ndo anachipukia na alimuahidi Ali kua atamlipizia kisasi kwa huyo mwamba, mwisho wa siku Tyson akakutana na Larry sikumbuki kama alimaliza round ya kwanza.
Yah,katika mechi hiyo Larry Holmes alileta kiburi mno kwa Ali mpk akapaniki na kumwambia I'm your master dogo acha kiburi Ali alipigwa huku Tyson akiwa bado janki anacheki kwenye Tv akisema huyu kima kampiga star wangu ipo siku nitalipa kisasi.

Baadae Tyson akawa maarufu akapata nafasi ya kukutana na Larry huku Ali akiwa mgeni rasmi wa hilo pambano kubwa sana lililosubiriwa kwa hamu kabla ya mapambano kuanza Ali alimng'ata Tyson sikio ulingoni na kumwambia" Mike destroy him" refa alivyoruhusu tu Tyson alirusha ngumu kama mvua kea kasi ya ajabu jamaa akawa anaanguka hovyo tu mwishowe akapigwa kubwa kuliko mpk akasema basi na kuamka kama mtu aliyechanganyikiwa vile na Mike kulipa kisasi chake cha miaka mingi mbele ya Star wake.
 
Siku zote ukioambanisha old school na kizazi kipya usitegemee kizazi kipya kushinda

Wazee wanajipendelea sana.utasikia mziki ulikuwa zamani sio siku hizi.mara ohh mpira ulikuwa enzi zetu bwwna siku hizi hamna kitu

Kwa muktadha huo mohamed ali atatetewa sana humu na wazee
 
Sikulaumu kwa kuamini kwamba Tyson ni bora kuliko Muhammad Ali. Mwenyewe umesema kwamba umeanza kufuatilia ngumi hivi karibuni.

Si kweli kwamba Muhammad Ali ndiye aliyefanya mchezo wa ngumi kuwa maarufu. Boxing ni mchezo maarufu duniani kabla ya era ya kina Ali. Jaribu kufuatilia historia utasikia watu kama kina Rocky Marciano, Joe Louis, Jack Dempsey, Sonny Liston, Floyd Petterson, Max Schmelling, Joe Walcot na wengieo ambao walikuwepo kabla Ali hajaja.

Njia bora ya kumlinganisha Tyson na Ali si tu kuangalia alishindaje bali pia alipigana na kina nani. Era ya kina Ali ilijaa boxers wenye uwezo mkubwa kuliko era ya Tyson. Ali alipigana na miamba kama Sonny Liston, Joe Frazier, Leon Spinks, Ken Norton, George Foreman na Ernie Shavers ambao wote ni Hall of Famers. Ukiondoa Evander Holyfield na Lennox Lewis, ambao wote walimpiga, Tyson alipigana na boxers wengi ambao walikuwa just average.
Tyson ni mzuri kuliko Ally hilo liko wazi.

Ally alikua celebrity boxer ila kwa uwezo Tyson ni mzuri kuliko Ally.

Ally alikua anabebwa sana na marefa.

Msikilize hata G. Foreman anasema hapaa.
 
Kuna Mwamba alimpiga Ali alikua anaitwa Larry kama sijakosea na haukupita muda mrefu Ali alistaafu ndondi kutokana na afya yake kubadilika.Kipindi hicho Tyson ndo anachipukia na alimuahidi Ali kua atamlipizia kisasi kwa huyo mwamba, mwisho wa siku Tyson akakutana na Larry sikumbuki kama alimaliza round ya kwanza.
Larry Holmes.

Alikua bingwa toka mwaka 1978 hadi 1985 kwa kuutetea mkanda wake kwa zaidi ya mapambano 20.

Tyson alikuja kumpiga Larry tayari alikua ile kitaalam tunaitwa past his prime time.
 
Sikulaumu kwa kuamini kwamba Tyson ni bora kuliko Muhammad Ali. Mwenyewe umesema kwamba umeanza kufuatilia ngumi hivi karibuni.

Si kweli kwamba Muhammad Ali ndiye aliyefanya mchezo wa ngumi kuwa maarufu. Boxing ni mchezo maarufu duniani kabla ya era ya kina Ali. Jaribu kufuatilia historia utasikia watu kama kina Rocky Marciano, Joe Louis, Jack Dempsey, Sonny Liston, Floyd Petterson, Max Schmelling, Joe Walcot na wengieo ambao walikuwepo kabla Ali hajaja.

Njia bora ya kumlinganisha Tyson na Ali si tu kuangalia alishindaje bali pia alipigana na kina nani. Era ya kina Ali ilijaa boxers wenye uwezo mkubwa kuliko era ya Tyson. Ali alipigana na miamba kama Sonny Liston, Joe Frazier, Leon Spinks, Ken Norton, George Foreman na Ernie Shavers ambao wote ni Hall of Famers. Ukiondoa Evander Holyfield na Lennox Lewis, ambao wote walimpiga, Tyson alipigana na boxers wengi ambao walikuwa just average.
Nakazia
 
Tyson ni habari nyingine

Weakness ya Tyson, alikua hawezi kumaliza rounds
Yani zile round za mwanzo ukichelewa basi round ya tano. Ndio mapambano mengi alikua anashinda hivyo

Wahuni, wakamgundua hizo pigo zake
Wakawa wanadefence sana round za mwanzo
Hapo mike anafunguka, full kupanic. Akifika round ya 8. Ndio game inamgeukia, nakupoteza pambano

Ally alikua anajua kumaliza mapambano
Lipi alimalize mapema, lipi litembee round nyingi

Tyson still the best over Ally
 
Tyson ni mzuri kuliko Ally hilo liko wazi.

Ally alikua celebrity boxer ila kwa uwezo Tyson ni mzuri kuliko Ally.

Ally alikua anabebwa sana na marefa.

Msikilize hata G. Foreman anasema hapaa.
Umeweka interview ya Ken Norton halafu unasema ni ya George Foreman. Hilo peke yake linanipa mashaka juu ya uelewa wako kuhusu boxing.

Tyson ni bora kuliko Ali kwa vigezo vipi? Ali kuwa celebrity kunahusiana vipi na boxing talent? Tyson hakuwa celebrity? Kichekesho cha mwaka ni kudai Ali alikuwa anabebwa na marefa. Hakika nyie Tyson stans mna shida sana.
 
Siku zote ukioambanisha old school na kizazi kipya usitegemee kizazi kipya kushinda

Wazee wanajipendelea sana.utasikia mziki ulikuwa zamani sio siku hizi.mara ohh mpira ulikuwa enzi zetu bwwna siku hizi hamna kitu

Kwa muktadha huo mohamed ali atatetewa sana humu na wazee
Wanakera sana ila ukweli ni kwamba Mike ni zaid ya Ali alafu ukianglia jinsi Mike anavopigana ile style ni hatari sana hakuna bondia mwenye style nzuri kama yeye
 
Wanakera sana ila ukweli ni kwamba Mike ni zaid ya Ali alafu ukianglia jinsi Mike anavopigana ile style ni hatari sana hakuna bondia mwenye style nzuri kama yeye
Ukiacha Evander Holyfield na Lennox Lewis ni bondia gani wa maana ambaye Tyson alipigana naye? Peter McNeely? Bruce Seldon? Please ...

Tyson ameshawahi kupigana "vita" kama ya Ali vs Frazier (mara tatu)? Tyson kishawahi kukutana na mtu mwenye ngumi nzito kama George Foreman na akashinda wakati kila mtu alijua anaenda Zaire kufa?Tyson kishawahi kuchukua ubingwa wa dunia wa uzito wa juu mara 3 kama Ali?
 
Back
Top Bottom