Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,504
- 9,283
Serikali Mkoani Iringa imesema itawakamata wazazi na wanafamilia wanaoshindwa kutoa ushahidi mahakamani dhidi ya vitendo vya ubakaji na ulawiti walivyofanyiwa watoto.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Queen Sendiga wakati akizungumza na wanahabari juu ya kushamiri kwa vitendo hivyo vinavyochangiwa na wazazi kushindwa kutoa ushirikiano kesi inapofikishwa mahakamani.
“Tuna majalada mengi ambayo wazazi wamekimbia ninakusudia kutoa agizo kwa yale majalada ambayo wazazi walifika mpaka polisi wakaandika maelezo na kugoma kwenda mahakamani tutawakamata wao ili waje watuambie kwanini walikwenda hadi polisi wakaelezea tukio lilivyokuwa halafu hawataki kwenda mahakamani kutoa ushahidi”amesema Sendiga.
Sendiga amewataka waandishi wa habari mkoani humo kusaidia kutoa elimu katika jamii kuhusu vitendo vya ukatili wa kijinsia kwakuwa vitendo hivyo vimeshamiri mkoani humo.
“Ni jukumu la kila mwanajamii kusaidia kuelezea na kutoa elimu ya unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto ili kutokomeza ukatili huu,hawa tuwalee vizuri na tusiwafanyie vitendo vya kinyama”amesema
Mwananchi
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Queen Sendiga wakati akizungumza na wanahabari juu ya kushamiri kwa vitendo hivyo vinavyochangiwa na wazazi kushindwa kutoa ushirikiano kesi inapofikishwa mahakamani.
“Tuna majalada mengi ambayo wazazi wamekimbia ninakusudia kutoa agizo kwa yale majalada ambayo wazazi walifika mpaka polisi wakaandika maelezo na kugoma kwenda mahakamani tutawakamata wao ili waje watuambie kwanini walikwenda hadi polisi wakaelezea tukio lilivyokuwa halafu hawataki kwenda mahakamani kutoa ushahidi”amesema Sendiga.
Sendiga amewataka waandishi wa habari mkoani humo kusaidia kutoa elimu katika jamii kuhusu vitendo vya ukatili wa kijinsia kwakuwa vitendo hivyo vimeshamiri mkoani humo.
“Ni jukumu la kila mwanajamii kusaidia kuelezea na kutoa elimu ya unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto ili kutokomeza ukatili huu,hawa tuwalee vizuri na tusiwafanyie vitendo vya kinyama”amesema
Mwananchi