EINSTEIN112
JF-Expert Member
- Oct 26, 2018
- 21,713
- 35,534
Iran yailaumu Israel kwa shambulio la ndege isiyo na rubani yaonya, kulipiza kisasi
Iran imeilaumu Israel kwa shambulio la ndege isiyo na rubani kwenye eneo la kijeshi katikati mwa mji wa Isfahan siku ya Jumamosi.
Balozi wake katika Umoja wa Mataifa alisema matokeo hayo yalionyesha kuwa Israel "ilihusika na jaribio hilo la uchokozi".
Iran, alisema, inahifadhi haki "ya kujibu kwa uthabiti vitisho vyovyote au vitendo viovu" vya Israel.
Israel haijathibitisha au kukanusha kuwa ilihusika na shambulio hilo, ambalo Iran ilisema lilisababisha uharibifu mdogo, ingawa hii haijathibitishwa.
Nchi hizo mbili ni maadui wakubwa na katika miaka ya hivi karibuni zimekuwa zikishiriki katika kile kilichoelezwa kuwa ni "vita kivuli" vya mashambulizi yasiyodaiwa dhidi ya mali, miundombinu na raia wa kila mmoja wao.
Israel inajulikana zaidi kufanya mashambulizi kwa kile inachosema kuwa ni uhamisho wa silaha za Iran kwa wanamgambo nchini Lebanon na pia inaaminika kuhujumu maeneo ya nyuklia ya Iran na kuwaua wanasayansi wa nyuklia wa Iran.
Iran, ambayo inakataa haki ya Israel kuwepo, imeshutumiwa na Israel kwa kupanga kushambulia raia wa Israel na Wayahudi. Kila upande pia unaaminika kushambulia meli ya mwingine.
Katika barua kwa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, balozi wa Iran Amir Saeid Iravani aliishutumu Israel kwa "jaribio... la kuanzisha shambulio la kigaidi dhidi ya uwanja wa warsha" wa wizara ya ulinzi ya Iran. Hakubainisha ni ushahidi gani Iran inao kwa hili.
Bw Iravani alisema Iran ina haki ya kujibu "popote na wakati wowote inapoonekana inafaa".
Madhumuni ya eneo lililoshambuliwa haijulikani, ingawa ripoti zinaonyesha kuwa inaweza kuhusishwa na utengenezaji wa makombora