MIDFIELD
JF-Expert Member
- May 27, 2013
- 1,944
- 703
Habari za kutwa wapendwa. Kuna hili suala la kuvaa majoho kwa wahitimu wa ngazi mbalimbali za elimu kama ilivyoshamiri siku hizi. Kusema kweli, joho katika siku za nyuma lilikuwa ni vazi maalum lenye hadhi kubwa na lenye kuonesha heshima fulani anayopewa mtu kutokana na kazi au hatua kubwa aliyofikisha katika elimu yake. Hili lilidhihirishwa zamani pale ilipowekwa picha ya wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) katika fedha halali ya Tanzani, kama sikosei ilikuwa noti ya 1000. Hii ilionesha uthamani wa Joho kutoa taswira ya utaalamu aliofikia mtu na kuwa tayari kulitumikia Taifa kwa utaalamu aliokwisha upata. Kipindi hiki Joho lilivaliwa na mhitimu wa Chuo Kikuu pekee. Hii ilitufanya sisi tuliokuwa tunasoma kuwa na shauku ya kufikia hatua hiyo, ili nasi tuje tuweke historia ya kuvaa joho ktk maisha yetu.
Hata hivyo siku za hivi karibuni mambo yamekuwa tofauti kabisa. Joho limekosa thamani kwani linavaliwa na hata anayemaliza sekondari, shule ya msingi, diploma au mbaya zaidi hata chekechea!!! Jamani, hivi Joho limekosa thamani kiasi hicho! Au ndiyo mambo ya utandawazi?
Wenzangu mnalionaje hili, Karibuni tubadilishane mawazo:
Hata hivyo siku za hivi karibuni mambo yamekuwa tofauti kabisa. Joho limekosa thamani kwani linavaliwa na hata anayemaliza sekondari, shule ya msingi, diploma au mbaya zaidi hata chekechea!!! Jamani, hivi Joho limekosa thamani kiasi hicho! Au ndiyo mambo ya utandawazi?
Wenzangu mnalionaje hili, Karibuni tubadilishane mawazo: