Ipo nafasi yako itendee haki usishindane sana

Victor Mlaki

JF-Expert Member
May 1, 2016
3,542
3,451
IPO NAFASI NAFASI YAKO, FANYA YANAYOKUHUSU.

Maisha siyo vita wala kupambana sana ili kuwazidi wengine, maisha pia siyo kusubiri wakati tunaouita mzuri na majaliwa tu halikadhalika maisha siyo kile unachoambiwa au kukiona kwa wengine ila ni vile unavyoishi wewe.

Tafsiri sahihi ya maisha yako ipo kwako na siyo kwa mwingine yeyote. Maisha ya mwingine hayawezi kuwa tafsiri sahihi ya maisha yako.Maana ya maisha yako ni wewe unavyoishi na kuuelewa ulimwengu wako.

Suala la msingi zaidi ni kujielewa wewe mwenyewe kabla ya kutaka kuwaelewa wengine na kushindana nao. Kumbuka kila mtu anacho kitu chake anachoweza kukifanya kwa wepesi zaidi katika maisha yake.

Tambua kitu chako cha kufanya kuliko kukazana kutambua wanachofanya wengine na kujishidanisha nao. Kumbuka wao pia wana uwezo ambao wewe huna. Ipo nafasi ya kwanza kwa kila mtu inaitwa "upekee".

Tumia nafasi yako ya kwanza kufanya vitu vyako kwa sababu kila mtu ana nafasi yake ya kwanza katika kufanya mambo yake. Hivyo jitahidi sana kufanya yale yanayokuhusu zaidi kuliko kuumia na namna wengine wanavyotumia nafasi yao ya kwanza.

Kumbuka kuna vitu unaweza kuvifanya wewe na wengine wasiweze kabisa ila haimaanishi wao hawana vya kwao ambavyo wewe huwezi hata ukijilazimisha. Nadhani kufanya mambo yako ndiyo jambo la msingi zaidi.
"Live your life".
 
Nakubaliana na wewe asilimia mia.

Tunashindwa kusonga mbele kwa sababu ya kujadili maisha ya watu wengine, tunashindwa kujitathimini sisi kama sisi badala yake tunajishughulisha zaidi na maisha ya wengine yaani "wao'

Ishi maisha yako , siku zote siri ya mafanikio ya mtu ajuaye yeye mwenyewe, usihangaike kusikiliza mwingine anasema nini kwani ukweli wa kile akisemacho akijua yeye mwenyewe, nimeshuhudia watu wengi sana wakieleza maisha ambayo si yao kwa wengine na kwakuwa binadamu tunatabia ya kuchukua MANENO kama yalivyo tunajikuta tunaingizwa mkenge!


Naunga mkono hii hoja kwamba tunapaswa kuishi kama sisi na si kama wao!
 
Nakubaliana na wewe asilimia mia.

Tunashindwa kusonga mbele kwa sababu ya kujadili maisha ya watu wengine, tunashindwa kujitathimini sisi kama sisi badala yake tunajishughulisha zaidi na maisha ya wengine yaani "wao'

Ishi maisha yako , siku zote siri ya mafanikio ya mtu ajuaye yeye mwenyewe, usihangaike kusikiliza mwingine anasema nini kwani ukweli wa kile akisemacho akijua yeye mwenyewe, nimeshuhudia watu wengi sana wakieleza maisha ambayo si yao kwa wengine na kwakuwa binadamu tunatabia ya kuchukua MANENO kama yalivyo tunajikuta tunaingizwa mkenge!


Naunga mkono hii hoja kwamba tunapaswa kuishi kama sisi na si kama wao!

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Asante kwa kushadidisha kwa mifano kuntu.
 
Victor umeongea kitu chenye mashiko sana, dhana hii nimekuwa nikiitumia kumshauri moja ya watu wangu wa karibu ambaye yeye amekuwa na shida ya kupanic pale anapoona mtu wa karibu anamuacha kimaendeleo, hii hupelekea kudharau kile anachokifanya yeye na kukiona hakina maana!
 
Back
Top Bottom