kwa upande wa NSSF huduma ya matibabu wanayoitoa inaitwa social health insurance benefit (SHIB), ni moja katika mafao wanayotoa ya muda mfupi kwa wanachama wao. ili uweze kufaidika na fao hili lazima uwe mwachama wa nssf kwa muda usiopungua miez mitatu. utatibiwa wewe na mwenza wako mke au mume na watoto wanne. mwananchi yoyote anaruhisiwa kujiunga na mfuko ukiwa ktk sekta isio rasmi (informal sector)au sekta rasmi ( formal sector ). kiwango cha chini kuchangia ktk kwa mfuko kwa informal sector ni sh 20,000 kwa mwezi ambapo mbali ya kupata matibabu pia utapata mafao yote yanayotolewa na shirika kama mafao ya uzaz kwa wanachama wanawake, mafao ya kuumia kazini, mazishi , mafao ya kujitoa ,pension ya uzeen na penshen ya warithi. kumbuka kuwa ukichangia kiwango kikubwa zaidi nipo utakapokuja kupata mafao ya uzeen (pension) kubwa zaidi. tembelea ofisi yoyote ya nssf ilio karibu nawe kwa ajili ya kujiandikisha uanachama na kama tayar ni mwanachama nenda kajaze fomu za kujiunga huduma hii ya matibabu na kuchagua hospital unayotaka kutibiwa wewe na familia yako.