Interview ya TPDC utata mtupu!!!


Yes..ni kijana mdogo hivi mwembamba..jina ntaliweka hapa nikikumbuka..kwa ufupi kilichotokea ni hivi....Jana pale Msimbazi center baada ya zengwe walokutana nalo wenzetu waloambiwa majina yao hayaonekani, interview iliendelea na baada ya hapo tukaelekezwa majibu ya watakaoitwa kwenye oral interview yatabandikwa kwenye saa kumi na moja jioni jana ile ile..sasa basi kweli namba zilibandikwa maana majina hayakutumika..now i understand why...wakasema wafuatao waje kufanya oral interview pale TPDC mikocheni kesho saa tatu asubuhi (yani leo) na walikuwa wengi tu. Cha ajabu leo watu tumeamkia pale tukiwa bado tunashangaa maana ni pale brajec..kajamaa kakatokea kamevalia suti safi kabisa na briefcase tena katokea ndani ya mjengo na sio magetini walikopita wengine..kwa ufupi kila mtu akawa attention..maana hakuonekana kama mwenzetu..mara akaitwa kule ndani alikotokea..wewe ndo umekuja na taxi? unaitwa...akaenda huko ndani..baada ya muda zengwe likaanza..panel walikuwa washakaa (changa la macho) kisha watu wakaanza kuuliza what now..mbona muda unayoyoma..kwenda kumuuliza receptionist aliyekuwa anafanya registration..ikaonekana wote waliokuwa wamefika pale hakuna hata mmoja anayetakiwa kuingia interview...isipokuwa kale kajamaa tu...akaja huyo mmoja wa panelist akasema wamepigia watu 3 tu simu ambao ndo wanatakiwa kufanya oral interview..cha kusikitisha jana hawakusema watapiga simu bali watabandika majina na kweli walibandika na kuwaita watu waje mikocheni...cha ajabu zaid hadi saa tatu na nusu ni mmoja tu kati ya watu watatu waliopigiwa simu according to panelist ambaye ndo huyo kajamaa ambaye alikuwepo..ndo kusema hao wengine wawili walikuwa hawaitaki hiyo kazi hadi wasije?
 

mkuu. muda wa kufanya maamuzi ni sasa hivi au October 2015? unashauri yafanyike mageuzi kama Misri?:frusty:
 
halafu mie nilionaga pia first day walitoa majina na kesho yake wakatoa tena

nikajua wamerudia tu watu ambao hawakupata nafasi ya kuona jana waone leo kumbe

wana Mission zao..mwenye nacho anazid kuongezewa

Mtoto wa Rita Mlaki kala shavu
 
Last edited by a moderator:
 
mi niliona hilo tangazo lililorudiwa nikajua tu lazima watu waumie......
 
mi niliona hilo tangazo lililorudiwa nikajua tu lazima watu waumie......

Watu wameumia kweeeli mkuu!!!ha ha ha ha ha ila.huu nih uonezi kabisa
 


Nadhani akienda pale CMA(Mahakama ya Kazi) haraka anaweza kuwa na madai ya Msingi.Atafute wataalamu wa Sheria wakumsaidia haraka iwezekanavyo.
 
Hapo kuna uwezekano watu wamekula bila kunawa.
 
Yaani mimi ndo wamenikera wameniboa na kila kitu, walisema watabandika kwenye website ya coet.udsm jana saa 11 jioni tangu jioni hiyo mpaka leo asubuhi ya saa nne kasoro ndo majibu waruhusu web kufunguka. Hoja yangu ni, kama kweli walikuwa wanahitaji kusaili watu walishindwa nini kuweka results toka jana. Cha ajabu eti waliopita jana waende leo kufanya oral hivi mtu angeota kama kapita? Halafu kwa hiyo saa 4 na foleni za dar mtu anafikaje kwenye interview. Kiukweli TPDC HAMNA HAKI, MNA UONEVU ULIOKITHIRI, HUO SI UUNGWANA.
 
kumbe usanii uliendelea...hii kali.. halafu jamaa hawana hata aibu yani
 
Nashauri vijana wote tusio na ajira tuunganishe nguv na kuhakikisha kila mtu ana kadi ya kupiga kura 2015 jaman tubadilisheni mambo ili hata haya malalamiko yetu yapungue!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…