Internet katika Nokia E5

Internet katika Nokia E5

KAUMZA

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2010
Posts
699
Reaction score
241
Msaada wenu ni muhimu sana katika hili.
Nimenunua simu aina ya NOKIA E5. Nimejiunga na huduma za internet ili dunia iwe ktk kiganja changu. Cha ajabu ni kuwa kila nikitaka ku-surf ina-appear meseji isomekayo Insufficient memory. Nilipoichunguza nimegundua phone memory yake ni 364kb, na mpaka sasa ninapoandika post hii sijatumia hata kb moja. nimeweka memory card ya 4GB nikadhani labda itanisaidia, lakini hali ni ile ile.

Je, kuna uwezekano wa kuongeza capacity ya phone memory kutoka hiyo 364 kb na hata kufikia megabytes kadhaa, let say 12mb? Au kama kuna software yoyote, itakayoweza kui-activate simu yangu naomba nijulishwe.

KIKUBWA NI KUNIWEZESHA KUPATA MAWASILIANO NA HUDUMA ZA INTERNET.
 
E5 ina memory kubwa 2 kaka, cha msingi hapo toa vi2 kwenye simu peleka kwenye memory card... Kama bado itaendelea kufanya hvo format kwa *#7370# then pasword ya simu.. Coz hyo ni symbian
 
memory ya e5 ni 256 mb,kama una message ulitumiwa vitu kwa bluetooth,zifute zinajaza phone memory.uninstall software ambazo haztumii internet uziweke kwenye memory card.ukiona vip format kama jamaa anavyosema.kabla ya kuformat backup namba zako za simu .
 
Mgeni3 na isaac chikoma, nashukuru kwa msaada wenu. Nimejaribu imeshindikana. Na nikiformat kwa kupiga *#7370# naambiwa not available. Na kama mr isaac chikoma ulivyosema kuwa nijaribu ku-uninstal vitu, hakuna instalation yoyote iliyofanyika. Na simu ni mpya kabisa. MAWAZO ZAIDI NAYAKARIBISHA
 
Isaac, umeuliza swali zuri sana. Mi mwenyewe huwa najiuliza swali hilo. Naomba unielekeze namna ya kutambua u-orijinal wa nokia E5. Kiufupi, simu hii niliinunua USA mimi mwenyewe, ingawa kuinunua Amerika ama Ulaya haiondoi uwezekano wa kuuziwa feki.
 
bonyeza *#0000# na *06#,uangalie kama itakupa majibu.angalia kama main menu yako ina software nyingi au kidogo,pia angalia hizi software kama zipo,adobe reader,officesuite.
 
Nilipobonyeza *0000# ilileta meseji hii:
Software version
V12.0.024
Software version date
04-08-09
Customer version
12.0.024.C01.01
Custom version date
04-08-09
language set
26\model\nokia E5-00
Type
RM-505
Last update
2009/9/17

Na nilipobonyeza *#06# ili-display ujumbe huu: Imei: 354895008005261
SVN: 78

Kuhusu hizo software ulizozotaja hapo i.e adobe reader na officesuite zote hazipo katika simu hii

Je, hii simu ni original au feki? na nilipoifungua ndani imeandikwa made in finland
 
inaweza ikawa original ila mara nyingi bidhaa za nje ya nchi huwa kuna baadhi, vitu,zinakataa,nimesoma technical specifications za e5 zinaonyesha kuwa ina office application na pdf viewer.jaribu kutumia hii *#7780#. Angalia pia kwenye file manager phone memory,kama kuna vitu vinavyojaza phone memory.
 
inaweza ikawa original ila mara nyingi bidhaa za nje ya nchi huwa kuna baadhi, vitu,zinakataa,nimesoma technical specifications za e5 zinaonyesha kuwa ina office application na pdf viewer.jaribu kutumia hii *#7780#. Angalia pia kwenye file manager phone memory,kama kuna vitu vinavyojaza phone memory.

Nimejaribu *#7780# nayo inaleta ujumbe NOT AVAILABLE. Na ktk file manager naona vitu viwili tu. Phone memory ambayo ina kb 364(ktk phone memory nimefuta kila kitu) na memory card yangu yenye Gb 4. Tatizo hapa nadhan phone memory(364kb) ni ndogo sana na ndo maana kila niki-browse inaniletea ujumbe INSUFFICIENT MEMORY. Hivi hakuna njia ya kuongeza capacity ya phone memory?
 
hakuna,bro.simu yoyote ya nokia original lazma ikubali hizo codes,ikiwa inakataa itakuwa siyo original,megapixel ya camera ni ngapi?.
 
Ina megapixel 5.0. Simu hii imenichosha. Hata hamu sina
 
Hapana. Mi sipo DAR, ingawa mara kwa mara nakuja Dar. Nikija, wapi nitapata msaada?

Kuna "wachawi" wa NOKIA pale mtaa wa Magore. Jengo linatazama geti la Ngome "Makao Makuu ya Jeshi" kuna bango la Midcom.
 
Asante. Ninategemea kuja Dar katikati ya mwezi huu. Kama nitakuwa sijapata suluhisho nitawaona hao jamaa. Asante Mr Kombo
 
Msaada wenu ni muhimu sana katika hili.
Nimenunua simu aina ya NOKIA E5. Nimejiunga na huduma za internet ili dunia iwe ktk kiganja changu. Cha ajabu ni kuwa kila nikitaka ku-surf ina-appear meseji isomekayo Insufficient memory. Nilipoichunguza nimegundua phone memory yake ni 364kb, na mpaka sasa ninapoandika post hii sijatumia hata kb moja. nimeweka memory card ya 4GB nikadhani labda itanisaidia, lakini hali ni ile ile.

Je, kuna uwezekano wa kuongeza capacity ya phone memory kutoka hiyo 364 kb na hata kufikia megabytes kadhaa, let say 12mb? Au kama kuna software yoyote, itakayoweza kui-activate simu yangu naomba nijulishwe.

KIKUBWA NI KUNIWEZESHA KUPATA MAWASILIANO NA HUDUMA ZA INTERNET.

bila shaka hicho kimeo ni fake kwani nokia e5 Original internal memory yake ni 256mb. Nimeshakutana na vimeo vya kichina huwa vinatabia hiyo kila unapotaka kufungua page, hiyo inatokana na kwamba browser inapoload page huwa ina store cache kwenye phone memory na kama memory ni ndogo kuliko ukubwa wa page lazima itakupa hiyo message. For more original nokia e5 specification please open this link http://gsmarena.com/nokia_e5-3198.php
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom