Intelijensia ya kijiweni

Intelijensia ya kijiweni

KEMPANJU BOY

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2014
Posts
508
Reaction score
1,255
Niende moja kwa moja kwenye mada! Leo mchana kwenye pita pita zangu kuna kijiwe kimoja nimekuta mjadala kwa kiasi fulani nilivutiwa ikabidi nisogee kuongeza maarifa. Mjadala ulikuwa baina ya mtu mmoja aliyekuwa akihubiri injili lakini baadaye akaonekana anatangaza dhehebu lake na Wale wana kijiwe. Yule mtu aliulizwa maswali mpaka akakimbia, ningependa tushiriki angalau mwenye ufahamu kidogo tuelimishane. Maswali ni kama ifuatavyo:

i) Kati ya Ukristo na biblia ni kipi kimetangulia?( Aya maswali yanayofuata yalikuja baada ya jamaa kusema ukristo ulitangulia).

ii) Kama biblia iliandikwa Karine ya 3 kama baadhi ya historia zinavyoonesha Ukristo umeanzishwa kwa Misingi ipi? Mfano dini ya kiyahudi ilianzishwa kwa misingi ya tourati ya Musa.

iii) Kama Ukristo umeanzishwa kwa kufuata Injili ( mafundisho ya Yesu) inakuwaje kuna vyeo makanisani kama Ushemasi, Uaskofu na Uchungaji ambavyo kimsingi havipo kwenye injili bali vimetajwa na Nyaraka za Paulo na siyo wainjili?(Luka, Marko, Mathayo na Yohane).

iv) Je kuna aja ya Madhehebu ya Kikristo yaliyoanzishwa kabla ya kui compile biblia, mafundisho yao yote kuwa kwenye biblia? mfano: RC na othodox au ili linayahusu madhehebu yale yalochipukia baada ya mwaka 1500 BC?.

Karibu kwa Michango yenu wadau!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Niende moja kwa moja kwenye mada! Leo mchana kwenye pita pita zangu kuna kijiwe kimoja nimekuta mjadala kwa kiasi fulani nilivutiwa ikabidi nisogee kuongeza maarifa. Mjadala ulikuwa baina ya mtu mmoja aliyekuwa akihubiri injili lakini baadaye akaonekana anatangaza dhehebu lake na Wale wana kijiwe. Yule mtu aliulizwa maswali mpaka akakimbia, ningependa tushiriki angalau mwenye ufahamu kidogo tuelimishane. Maswali ni kama ifuatavyo:

i) Kati ya Ukristo na biblia ni kipi kimetangulia?( Aya maswali yanayofuata yalikuja baada ya jamaa kusema ukristo ulitangulia).

ii) Kama biblia iliandikwa Karine ya 3 kama baadhi ya historia zinavyoonesha Ukristo umeanzishwa kwa Misingi ipi? Mfano dini ya kiyahudi ilianzishwa kwa misingi ya tourati ya Musa.

iii) Kama Ukristo umeanzishwa kwa kufuata Injili ( mafundisho ya Yesu) inakuwaje kuna vyeo makanisani kama Ushemasi, Uaskofu na Uchungaji ambavyo kimsingi havipo kwenye injili bali vimetajwa na Nyaraka za Paulo na siyo wainjili?(Luka, Marko, Mathayo na Yohane).

iv) Je kuna aja ya Madhehebu ya Kikristo yaliyoanzishwa kabla ya kui compile biblia, mafundisho yao yote kuwa kwenye biblia? mfano: RC na othodox au ili linayahusu madhehebu yale yalochipukia baada ya mwaka 1500 BC?.

Karibu kwa Michango yenu wadau!



Sent using Jamii Forums mobile app
Inabidi usiwe na majibu kichwani halafu kuwa tayari kujifunza utaelewa vizuri...maswali yako ni mepesi Sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maana Kama ukiukubali kama Kuna ukristo Na kristo ndio aliouanzisha ,halafu ukamkataa Paulo ambaye nae ni Mtume wa kristo basi hoja yako itakua Haina uthabiti acha niishie Hapo,maana Kama hautaelewa kuanzia hapa hata mbele hautoelewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukristo ni ufuaswi wa Kristo. Kristo ukisoma Yohana anaitwa Neno. Neno alikuwa kwa Mungu na vyote vilifanyika kwa huyo. Naye Neno alikuwa ni Mungu. Nikuulize wewe na wakijiweni ulio wawakilisha Mungu alianza lini? Pili wafuasi wa Mungu au wanao mwamini Mungu walianza lini? Ukijibu hili la pili utakuwa umejibu Ukristu ulianza lini?

Ids za kibubuni, chomoa mojawapo hapo ipiganishe.
 
Ukristo ni ufuaswi wa Kristo. Kristo ukisoma Yohana anaitwa Neno. Neno alikuwa kwa Mungu na vyote vilifanyika kwa huyo. Naye Neno alikuwa ni Mungu. Nikuulize wewe na wakijiweni ulio wawakilisha Mungu alianza lini? Pili wafuasi wa Mungu au wanao mwamini Mungu walianza lini? Ukijibu hili la pili utakuwa umejibu Ukristu ulianza lini?

Ids za kibubuni, chomoa mojawapo hapo ipiganishe.
Mungu Alianza lini ndio nini?

Au ulikusudia kusema kua mungu alizuka vipi au ni lini chanzo cha huyo mungu kilipoanza?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom