Zimekuwepo taarifa kutoka kwa mashabiki na wanachama wa club ya Yanga wakishawishi na kutaka sana ndugu Hers agombee urais wa Yanga.
Nafikiria hivi hawaoni mgongano mkubwa wa kimaslahi iwapo kweli Injinia Hersi akiamua Kugombea na akawa Rais!!?
Kvp!!? Hers ni sehemu ya wafadhili wa sasa wa Yanga ambao wanatarajiwa kuwa wawekezaji kwenye mfumo mpya ambao club ya Yanga inauendea, sasa unampaje urais mtu ambae anahitaji kuja kuwa mwekezaji!! Atajisimamia vipi? Je wawekezaji wengine watatendewa fair kweli??
Makosa ya mihemko kama hii ndo waliifanya Simba halafu leo wanalalamika et Mwekezaji amepewa mamlaka yote na mwenyekiti wa club hana lolote zaidi ya kufungua na kufunga vikao. Kipindi wanapitisha katiba ilipelekwa kishabiki sasa akili zimeanza kutumika mianya ya udhaifu wameanza kuiona. Yanga nao nawaona wanataka kuyapeleka mambo kihisia zaid kitu ambacho baadae kitaibua migogoro isiyoisha.
Nawasilisha.....
Nafikiria hivi hawaoni mgongano mkubwa wa kimaslahi iwapo kweli Injinia Hersi akiamua Kugombea na akawa Rais!!?
Kvp!!? Hers ni sehemu ya wafadhili wa sasa wa Yanga ambao wanatarajiwa kuwa wawekezaji kwenye mfumo mpya ambao club ya Yanga inauendea, sasa unampaje urais mtu ambae anahitaji kuja kuwa mwekezaji!! Atajisimamia vipi? Je wawekezaji wengine watatendewa fair kweli??
Makosa ya mihemko kama hii ndo waliifanya Simba halafu leo wanalalamika et Mwekezaji amepewa mamlaka yote na mwenyekiti wa club hana lolote zaidi ya kufungua na kufunga vikao. Kipindi wanapitisha katiba ilipelekwa kishabiki sasa akili zimeanza kutumika mianya ya udhaifu wameanza kuiona. Yanga nao nawaona wanataka kuyapeleka mambo kihisia zaid kitu ambacho baadae kitaibua migogoro isiyoisha.
Nawasilisha.....