iNJIL ya viwanda kama ilivyoandikwa na...

iNJIL ya viwanda kama ilivyoandikwa na...

Nichumu Nibebike

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2016
Posts
8,658
Reaction score
15,813
Leo ni mwendo wa mahubiri ya viwanda: Kwa hiyo tujikumbushe jinsi Bwana alivyozindua kiwanda cha kwanza kule kana ya Galilaya.
Ufunguzi wa kiwanda cha kutengneza wine uliharakishwa kwa vile kulikuwa na dharura.
Bwana hakuwa amejiandaa kuzindua kiwanda lakini kwa vile mama yake alimuomba akizindue, na uzalishaji uanze mara moja, basi Bwana, hakuna na namna.
Bwana alimuuliza mama yake, nina nini nawe, saa yangu ya uzinduzi bado.
Mama yake akawambia wale watumishi, lolote atakalowaambia, fanyeni.
Basi Bwana akwaambia wayajaze maji yale ma Simtank (mabalasi).
Wakafanya hivyo. Bwana akafanya mambo yake pale, yale maji yakageuka kuwa divai (wine).
Waonjaji wa TBS (mkuu wa meza) alipoionja ile wine akasema, hapajawahi kutokea kiwanda hapa nchini kwetu kinachotengeneza wine nzuri kama hii. Wakaibandika ile wine alama ya ubora wa TBS wakairuhusu iingie sokoni.

WITO: Maaskof, mahubiri ya viwanda ni wito unaotekelezeka kabisa. Tuhubiri viwanda.
 
Ndipo mfalme akamwuliza mwanae mpendwa " ni nani huyu apingaye utengenezaji wa viwanda vya mablanket, nyama , juis na biskut " ndipo mwanaye Paulo akamjibu " ni mafarisayo wametoa waraka baba na hawataki ukaongoze malaika mbinguni" waraka kwa wakolomije 3:1
 
Inabidi hii injili ihuishwe iwe ya kweli...tuzindue na viwanda vya kuchonga maneno na vingine vya kuwalisha watu maneno ili neno la mkuu litimie!
 
Na kiwana cha mana je?
Mana cha mtoto! Bwana aliendelea na ufunguzi wa kiwanda cha kuoka mikate na ku chakata samaki.
Bwana akawaambia wanafunzi wake: Nawaonea huruma makutano kwa kuwa wako nami nyikani siku tatu hawajala kitu. Wanafunzi wake wakamwambia, Bwana tunao hapa samaki watatu na mikate mitano! Bwana akwambia huo ni mtaji tosha. Leteni hapa hizo samaki watano na mikate mitatu tuitumie kama malighafi ya kutengeneza chakula cha kuwatosha makutano.
Basi Bwana akafanya uzalishaji, kukapatikana mikate na samaki wa kutosha kulisha wanaume elfu tano na vyakula vingi tu vikabaki.
Hivyo ni baadhi ya viwanda ambavyo Bwana alivizindua ndani ya miaka mitatu aliyokuwepo akitumika actively hapa Duniani.
 
Mana cha mtoto! Bwana aliendelea na ufunguzi wa kiwanda cha kuoka mikate na ku chakata samaki.
Bwana akawaambia wanafunzi wake: Nawaonea huruma makutano kwa kuwa wako nami nyikani siku tatu hawajala kitu. Wanafunzi wake wakamwambia, Bwana tunao hapa samaki watatu na mikate mitano! Bwana akwambia huo ni mtaji tosha. Leteni hama hizo samaki watano na mikate mitatu tuitumie kama malighafi ya kutengeneza chakula cha kuwatosha makutano.
Basi Bwana akafanya uzalishaji, kukapatikana mikate na samaki wa kutosha kulisha wanaume elfu tano na vyakula vingi tu vikabaki.
Hivyo ni baadhi ya viwanda ambavyo Bwana alivizindua ndani ya miaka mitatu aliyokuwepo akitumika actively hapa Duniani.
U killed it
 
Na pia Bwana akasema, Yakaisari mpeniKaisari Haya Mungu mpeni Mungu. Hivyo tusizuiwa kudai pesa zetu 26,042,018 tu.
 
Back
Top Bottom