leroy
JF-Expert Member
- Dec 8, 2010
- 1,589
- 2,140
WANA JAMVI, Asalaam aleykum.
NB: Kama una maono ya kiuchumi kutatua tatizo tofauti na haya tujuze kwa manufaa ya Taifa letu.
Nawasilisha.
- Katika nchi zote duniani jukumu la kuteremsha chini mfumuko wa bei (Inflation) upo chini ya Benki kuu za nchi husika.
- Benki kuu huteremsha chini mfumuko wa bei kwa kurekebisha ujazo wa fedha kwenye mzunguko na riba ili kuathiri Mahitaji/matumizi ya Jumla (Aggregate Demand/spending).
- Mfumuko wa bei Tanzania haupo katika demand bali uzalishaji (Supply) kwa sababu ya makwazokwazo yanayoathiri uzalishaji.
- Hii inathibiitika kupitia kupanda kwa bei ya chakula kutokana na uzalishaji mdogo na mfumuko mwingine wa bei kutokana na bidhaa zinazoagizwa toka nje.
- Hapo pekundu, ndipo panapolimit uwezo wa Benki kuu kuzuia na kuuteremsha mfumuko wa bei kwa kuwa ni upande wa pili wa sarafu (supply) ambao Benki kuu hupata shida kuuathiri na matokeo kupatikana katika kipindi kifupi.
- Hii ina maanisha kuwa, juhudi za serikali kushusha mfumuko wa bei kupitia fiscal policies hazitaleta mafanikio katika kipindi cha muda mfupi bali muda wa kati na muda mrefu ujao.
NB: Kama una maono ya kiuchumi kutatua tatizo tofauti na haya tujuze kwa manufaa ya Taifa letu.
Nawasilisha.