Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Urejeshaji fomu za kugombea urais umekamilika leo katika ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), ambapo mgombea urais kupitia ACT-Wazalendo, Luhaga Mpina, alizuiwa kuingia kutokana na kukosa vigezo.
Kwa mujibu wa kanuni za chama hicho, mgombea wa nafasi ya urais anatakiwa awe mwanachama aliyehudumu ndani ya chama kwa angalau siku 30 kabla ya uteuzi, jambo ambalo Mpina alishindwa kutimiza.
Mpina, ambaye aliwasili saa 6:40 mchana akiwa na mgombea mwenza wake, alizuiwa getini na maafisa wa Tume na kuambiwa wasubiri nje. Hata hivyo, hadi mwisho wa siku, yeye pamoja na wafuasi wake hawakuruhusiwa kuingia ndani kurejesha fomu hizo.
Awali, ACT-Wazalendo walieleza matumaini ya kurejesha fomu hizo ili kujiandaa kuanza kampeni rasmi katika maeneo mbalimbali nchini, lakini walikumbana na kikwazo hicho.
Wagombea wa Vyama VingineMgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, akiwa na mgombea mwenza wake Dk. Emmanuel Nchimbi, walifanikiwa kurejesha fomu zao kwa mujibu wa ratiba ya Tume.
Mbali na CCM, vyama vingine vilivyorejesha fomu ni: NRA, AAFP, Chama Makini, NLD, UPDP, ADA TADEA, UMD, TLP, CCK, CHAUMMA, DP, SAU, CUF, ADC, UDP, NCCR-Mageuzi na UMD.
Wagombea wa Urais Tanzania 2025
1. Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Chanzo: Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi
Kwa mujibu wa kanuni za chama hicho, mgombea wa nafasi ya urais anatakiwa awe mwanachama aliyehudumu ndani ya chama kwa angalau siku 30 kabla ya uteuzi, jambo ambalo Mpina alishindwa kutimiza.
Mpina, ambaye aliwasili saa 6:40 mchana akiwa na mgombea mwenza wake, alizuiwa getini na maafisa wa Tume na kuambiwa wasubiri nje. Hata hivyo, hadi mwisho wa siku, yeye pamoja na wafuasi wake hawakuruhusiwa kuingia ndani kurejesha fomu hizo.
Awali, ACT-Wazalendo walieleza matumaini ya kurejesha fomu hizo ili kujiandaa kuanza kampeni rasmi katika maeneo mbalimbali nchini, lakini walikumbana na kikwazo hicho.
Wagombea wa Vyama VingineMgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, akiwa na mgombea mwenza wake Dk. Emmanuel Nchimbi, walifanikiwa kurejesha fomu zao kwa mujibu wa ratiba ya Tume.
Mbali na CCM, vyama vingine vilivyorejesha fomu ni: NRA, AAFP, Chama Makini, NLD, UPDP, ADA TADEA, UMD, TLP, CCK, CHAUMMA, DP, SAU, CUF, ADC, UDP, NCCR-Mageuzi na UMD.
Wagombea wa Urais Tanzania 2025
1. Chama Cha Mapinduzi (CCM)
- Samia Suluhu Hassan - Mgombea Urais
- Emmanuel Nchimbi – Mgombea mwenza
- Hassan Kisabya Almas - Mgombea Urais
- Hamis Hassan - Mgombea mwenza
- Kunje Ngombare Mwiru – Mgombea Urais
- Chumu Abdallah Juma – Mgombea mwenza
- Coaster Kibonde – Mgombea urais
- Aziza Haji Suleiman – Mgombea mwenza
- Doyo Hassan Doyo – Mgombea urais
- Chausiku Khatibu Mohamed – Mgombea mwenza
- Twalib Ibrahim Kadege – Mgombea Urais
- Abdalla Mohamed Khamis – Mgombea mwenza
- George Bussungu – Mgombea Urais
- Ali Issa Makame - Mgombea mwenza
- Mwajuma Noty Mirambo – Mgombea Urais
- Mashavu Alawi - Mgombea mwenza
- Yustas Rwamugira – Mgombea Urais
- Aman Seleman Mzee - Mgombea mwenza
- David Daud Mwaijele – Mgombea Urais
- Masoud Ali Abdalla - Mgombea mwenza
- Salum Mwalimu – Mgombea Urais
- Devotha Minja - Mgombea mwenza
- Abdul Mluya – Mgombea Urais
- Abrahman Khatib - Mgombea mwenza
- Majalio Paul Kyara – Mgombea Urais
- Satia Mussa Bebwa - Mgombea mwenza
- Gombo Gombo – Mgombea Urais
- Husna Mohamed Abdalla - Mgombea mwenza
- Wilson Elias Mulumbe – Mgombea Urais
- Shoka Khamis Juma - Mgombea mwenza
- Saum Rashid – Mgombea Urais
- Juma Hamis - Mgombea mwenza
- Haji Ambar Khamis – Mgombea Urais
- Dkt. Eveline Wilbard Munisi - Mgombea mwenza
Chanzo: Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi