Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 3,119
- 1,428
Kumekuwepo na taarifa za uongo na upotoshaji zinazozagaa kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa:
Mfumo wa Data za Uchaguzi unaotumiwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) umeunganishwa na mfumo wa NIDA na Mfumo huo umeunganishwa na chama kimoja cha siasa, na kwamba zoezi la kupiga kura limekamilika tayari.
Tume inapenda kufafanua na kukanusha vikali taarifa hizo kutokana na sababu zifuatazo:
1. Taarifa hizo ni za uongo na upotoshaji, zikitolewa na watu wasio na uelewa kuhusu mfumo wa uchaguzi wa Tanzania.
2. Daftari la Kudumu la Wapiga Kura halijaunganishwa na mfumo wowote wa Serikali au Taasisi binafsi kwa ajili ya kupigia kura.
3. Mfumo wa kupiga kura, kuhesabu kura na kutangaza matokeo hautumii mfumo wowote wa kielektroniki.
4. Utaratibu unaotumika ni wa kawaida (manual) katika hatua zote za kupiga kura, kuhesabu na kutangaza matokeo.
5. Baada ya kukamilika uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, vyama vya siasa vilikabidhiwa nakala za daftari linaloonesha idadi ya wapiga kura walioandikishwa katika kila kituo.
6. Mawakala wa vyama vya siasa hutumia daftari husika kumtambua mpiga kura anayefika kituoni kwa ajili ya kupiga kura.
7. Mchakato wa kupiga kura ni wa wazi:
Wito kwa Wananchi na Wadau wa Uchaguzi: Kupuuza taarifa za uongo na upotoshaji zenye lengo la kusababisha taharuki.
Kufuatilia taarifa sahihi za Tume kupitia vyanzo rasmi pekee, zikiwemo:
Kumbuka: Uchaguzi Mkuu unatarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba 2025.
Soma Pia: INEC, NIDA wamkana Polepole
Imetolewa: 23 Agosti 2025
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC)
Mfumo wa Data za Uchaguzi unaotumiwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) umeunganishwa na mfumo wa NIDA na Mfumo huo umeunganishwa na chama kimoja cha siasa, na kwamba zoezi la kupiga kura limekamilika tayari.
Tume inapenda kufafanua na kukanusha vikali taarifa hizo kutokana na sababu zifuatazo:
1. Taarifa hizo ni za uongo na upotoshaji, zikitolewa na watu wasio na uelewa kuhusu mfumo wa uchaguzi wa Tanzania.
2. Daftari la Kudumu la Wapiga Kura halijaunganishwa na mfumo wowote wa Serikali au Taasisi binafsi kwa ajili ya kupigia kura.
3. Mfumo wa kupiga kura, kuhesabu kura na kutangaza matokeo hautumii mfumo wowote wa kielektroniki.
4. Utaratibu unaotumika ni wa kawaida (manual) katika hatua zote za kupiga kura, kuhesabu na kutangaza matokeo.
5. Baada ya kukamilika uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, vyama vya siasa vilikabidhiwa nakala za daftari linaloonesha idadi ya wapiga kura walioandikishwa katika kila kituo.
6. Mawakala wa vyama vya siasa hutumia daftari husika kumtambua mpiga kura anayefika kituoni kwa ajili ya kupiga kura.
7. Mchakato wa kupiga kura ni wa wazi:
- Mpiga kura aliyeandikishwa hufika mwenyewe kituoni akiwa na kadi ya mpiga kura iliyotolewa na Tume.
- Jina lake hutusomwa kwa sauti na msimamizi wa kituo, ili mawakala wa vyama wahakikishe jina lipo kwenye daftari.
- Baada ya uhakiki, mpiga kura hupewa karatasi za kura na kuendelea na mchakato wa kupiga kura.
Wito kwa Wananchi na Wadau wa Uchaguzi: Kupuuza taarifa za uongo na upotoshaji zenye lengo la kusababisha taharuki.
Kufuatilia taarifa sahihi za Tume kupitia vyanzo rasmi pekee, zikiwemo:
- Tovuti ya Tume: www.inec.go.tz
- Kurasa rasmi za Tume kwenye mitandao ya kijamii.
Kumbuka: Uchaguzi Mkuu unatarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba 2025.
Soma Pia: INEC, NIDA wamkana Polepole
Imetolewa: 23 Agosti 2025
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC)