Inawezekana ikawa kweli?

Inawezekana ikawa kweli?

Tiba

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2008
Posts
4,607
Reaction score
3,187
Nimefuatilia kwa karibu posting zinazofanyika kwa siku za hivi karibuni nyingi na kugundua kwamba nyingi zinahusu mahusiano na mambo ya mapenzi ukilinganisha zile zinazohusu mijadala juu ya mustakabali wa nchi kuhusu rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, uhujumu uchumi, EPA na mafisadi wake na siasa za nchi yetu kwa ujumla.

Nikiangalia kwa karibu kulikuwa na wimbi la watu kujiunga na JF some 6 months ago ambapo mijadala juu ya ufisadi ilikuwa imepamba moto na ninajikuta nalazimika kufikiria kwamba kulikuwa na msukumo fulani kutoka kwa mafisadi kuingiza "watu wao" kwa wingi hapa JF na kupost issues za mahusiano ili kupindisha attention ya watu kutoka kwenye kupigia kelele ufisadi na badala yake tuzame kwenye kujadili mambo yanayohusu mahusiano na mapenzi.

Ikibidi Mods watupe data za aina za posting kwa siku za karibuni (at least for the past 6 months) ili tupime ukweli wa fikira zangu.

Mnalionaje wazo hili, je lina ukweli wowote?
 
toa maelezo mazuri kijana!haupo uchi unajua?
bado umevaa nguo.nenda straight kwenye point
 
toa maelezo mazuri kijana!haupo uchi unajua?
bado umevaa nguo.nenda straight kwenye point

Mi bado naisoma sijaimaliza bado. Nikimaliza ntatoa comments zangu.
 
Nimefuatilia kwa karibu posting zinazofanyika kwa siku za hivi karibuni nyingi na kugundua kwamba nyingi zinahusu mahusiano na mambo ya mapenzi ukilinganisha zile zinazohusu mijadala juu ya mustakabali wa nchi kuhusu rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, uhujumu uchumi, EPA na mafisadi wake na siasa za nchi yetu kwa ujumla.

Nikiangalia kwa karibu kulikuwa na wimbi la watu kujiunga na JF some 6 months ago ambapo mijadala juu ya ufisadi ilikuwa imepamba moto na ninajikuta nalazimika kufikiria kwamba kulikuwa na msukumo fulani kutoka kwa mafisadi kuingiza "watu wao" kwa wingi hapa JF na kupost issues za mahusiano ili kupindisha attention ya watu kutoka kwenye kupigia kelele ufisadi na badala yake tuzame kwenye kujadili mambo yanayohusu mahusiano na mapenzi.

Ikibidi Mods watupe data za aina za posting kwa siku za karibuni (at least for the past 6 months) ili tupime ukweli wa fikira zangu.

Mnalionaje wazo hili, je lina ukweli wowote?

Hee kwani kama mtu ana interest na siasa anawezakupotea mlango aingie kule kwenye mahusiano? Ingekuwa mahusiano na siasa yapo chumba kimoja basi ingekuwa ni rahisi kwa mtu kuwa distracted. Mimi sidhani kama kuna ukweli katika hili. Ni mtazamo wangu tu
 
Mhhh! hii nayo kali,leo nimekosa coment,ngoja na mimi nisome vizuri kama mchumba anavyofanya,labda nitapata mchango badae.
 
Hee kwani kama mtu ana interest na siasa anawezakupotea mlango aingie kule kwenye mahusiano? Ingekuwa mahusiano na siasa yapo chumba kimoja basi ingekuwa ni rahisi kwa mtu kuwa distracted. Mimi sidhani kama kuna ukweli katika hili. Ni mtazamo wangu tu

Turudi kwenye nyumba yetu mama, tuache wanasiasa waendelee na mambo yao. Watu wengine bana, eti wanafikiri threads ndio nguvu za kupambana na ufisadi. Chukua form kagombee ubunge uwaletee watu wako maendeleo na kubwabwaja kuupiga vita ufidani. Ngoja nisepe, napitwa kule na utamu.
 
Nimefuatilia kwa karibu posting zinazofanyika kwa siku za hivi karibuni nyingi na kugundua kwamba nyingi zinahusu mahusiano na mambo ya mapenzi ukilinganisha zile zinazohusu mijadala juu ya mustakabali wa nchi kuhusu rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, uhujumu uchumi, EPA na mafisadi wake na siasa za nchi yetu kwa ujumla.

Mkuu Tiba heshima mbele sana,

Niseme tu kwamba kwanza hii hoja yako imenishangaza, I mean where is diversity in JF? kwa nini kuna majukwaa tofauti tofauti? ungependa wote wachangie siasa?

Pili, hadi leo hii jukwaaa ka siasa lina posts zaidi ya 220,000, huku jukwaa la mahusiano na mapenzi likiwa na posts 36,000 hivi, je huo wingi unaozungumzia uko wapi? Huo uchunguzi mkuu uliufanyia forum hii hii ama nyingine?


Nikiangalia kwa karibu kulikuwa na wimbi la watu kujiunga na JF some 6 months ago ambapo mijadala juu ya ufisadi ilikuwa imepamba moto na ninajikuta nalazimika kufikiria kwamba kulikuwa na msukumo fulani kutoka kwa mafisadi kuingiza "watu wao" kwa wingi hapa JF na kupost issues za mahusiano ili kupindisha attention ya watu kutoka kwenye kupigia kelele ufisadi na badala yake tuzame kwenye kujadili mambo yanayohusu mahusiano na mapenzi.

mkuu labda tukumbushane karibu serikali nzima ilijiuzulu mwezi wa pili mwaka jana (2008), ungesema hapo kulikuwa na mijadala mizito nitakuelewa. Hoja ya EPA na Richmond au kagoda na wadogo zake si za mwaka huu wala mwaka jana ni za muda mrefu na zimejadiliwa hapa kwa mapana na marefu. Ni kitu gani cha ajabu kimetokea 6 months ago kiasi cha mafisadi kutuma watu wao huku kudivert mada?


Ikibidi Mods watupe data za aina za posting kwa siku za karibuni (at least for the past 6 months) ili tupime ukweli wa fikira zangu.

Mnalionaje wazo hili, je lina ukweli wowote?

mkuu hapa utakuwa unawapa mods kazi bila sababu, wenyewe wana kazi nzito kuhakikisha tupo hewani.

Mwenyewe kwa nini usicheki tu ukaja hapa na data kila kitu si kipo hewani ?

Otherwise, with all due respect, hii hoja siwezi kusema kama ina ukeli au haina, naiona totally irrelevant na isiyotegemewa kutoka kwa mtu wa kiwango chako.

respect.
 
Yametengwa majukwaa tofauti kwa sababu watu tuna interests tofauti vilevile. Si wote waliojiunga na JF wanapendelea mambo ya EPA na SIASA, na kwa maoni yangu naona si kweli kuwa watu tuliojiunga miezi sita iliyopita tumetumwa na mafisadi kufunga mijadala ya ufisadi(tuombe[niombe] radhi tafadhali), mbona mijadala inaendelea kama zamani?
Kuhusu jukwaa la mahusiano kuwa na post nyingi kipindi hiki, labda watu wengi wana matatizo ya kimahusiano zaidi na pale ni sehemu ya kupata ushauri na mafunzo.
Ni hayo tu mkuu!!!!!!!!!!
 
Turudi kwenye nyumba yetu mama, tuache wanasiasa waendelee na mambo yao. Watu wengine bana, eti wanafikiri threads ndio nguvu za kupambana na ufisadi. Chukua form kagombee ubunge uwaletee watu wako maendeleo na kubwabwaja kuupiga vita ufidani. Ngoja nisepe, napitwa kule na utamu.

Mkuu,

Haujajibu hoja ndugu yangu. Sema kuna ukweli kwenye observation yangu au hakuna na utoe sababu!!!

Tiba
 
Yametengwa majukwaa tofauti kwa sababu watu tuna interests tofauti vilevile. Si wote waliojiunga na JF wanapendelea mambo ya EPA na SIASA, na kwa maoni yangu naona si kweli kuwa watu tuliojiunga miezi sita iliyopita tumetumwa na mafisadi kufunga mijadala ya ufisadi(tuombe[niombe] radhi tafadhali), mbona mijadala inaendelea kama zamani?
Kuhusu jukwaa la mahusiano kuwa na post nyingi kipindi hiki, labda watu wengi wana matatizo ya kimahusiano zaidi na pale ni sehemu ya kupata ushauri na mafunzo.
Ni hayo tu mkuu!!!!!!!!!!

Mkuu,

Nakushukuru sana kwa mchango wako lakini sioni sababu ya kuomba radhi kwani sikumhukumu mtu hapa. Just my observations ambazo not necessarily ziwe kweli.

Tiba
 
Tiba.

Tafadhali elewa sio kila mtu ni mwanasiasa na mimi sipendi kabisa siasa, na kutokana na data zako unaonekana unaongea kwa hisia za kisiasa zaidi ya utashi ambao Mungu amekujalia na kama jina lako TIBA lilivyo.

Mfano mimi nimejiunga tangu 2008 fwatilia thread zangu so utaona kwamba unasukumwa na hisia zaidi.

Kama ni mapendekezo wafungie jukwaa la mapenzi pamoja na watu wake ambalo linachangiwa zaidi ili wabakie wanasiasa tu.

Ningeomba pia uongozi wa JF utoe tamko au jibu kwa TIBA kwa kukaa kimya inaweza kuwa mme msupport au mmemuignore kitu ambacho sio haki kwani hizo ni fikra zake.
 
Mkuu Tiba heshima mbele sana,

Niseme tu kwamba kwanza hii hoja yako imenishangaza, I mean where is diversity in JF? kwa nini kuna majukwaa tofauti tofauti? ungependa wote wachangie siasa?

Pili, hadi leo hii jukwaaa ka siasa lina posts zaidi ya 220,000, huku jukwaa la mahusiano na mapenzi likiwa na posts 36,000 hivi, je huo wingi unaozungumzia uko wapi? Huo uchunguzi mkuu uliufanyia forum hii hii ama nyingine?



mkuu labda tukumbushane karibu serikali nzima ilijiuzulu mwezi wa pili mwaka jana (2008), ungesema hapo kulikuwa na mijadala mizito nitakuelewa. Hoja ya EPA na Richmond au kagoda na wadogo zake si za mwaka huu wala mwaka jana ni za muda mrefu na zimejadiliwa hapa kwa mapana na marefu. Ni kitu gani cha ajabu kimetokea 6 months ago kiasi cha mafisadi kutuma watu wao huku kudivert mada?



mkuu hapa utakuwa unawapa mods kazi bila sababu, wenyewe wana kazi nzito kuhakikisha tupo hewani.

Mwenyewe kwa nini usicheki tu ukaja hapa na data kila kitu si kipo hewani ?

Otherwise, with all due respect, hii hoja siwezi kusema kama ina ukeli au haina, naiona totally irrelevant na isiyotegemewa kutoka kwa mtu wa kiwango chako.

respect.

Mkuu Kaizer,

Asante kwa mchango wako lakini nisaidie kunielewesha kiwango changu ni kipi mkuu, nisaidie hapa!!! Inawezekana sijijui sawasawa!!!!

Hizo data ulizotoa ni kwa kipindi kipi mkuu? Tangia JF ianzishwe? au kuanzia tarehe ngapi mpaka lini?

Tiba
 
sasa si ungekuja na thread kwenye siasa? Instead of talking politics, you r talking about people not talking about politics!! Unafaa kuwa mwenyekiti wa kijiji wewe kweli?
 
sasa si ungekuja na thread kwenye siasa? Instead of talking politics, you r talking about people not talking about politics!! Unafaa kuwa mwenyekiti wa kijiji wewe kweli?

Mkuu nakushukuru kwa hiyo Offer lakini ungevumilia mapungufu yangu na kujibu hoja. Mkuu mtu yupi niliyemsema mimi hapa?

Asante.

Tiba
 
Mkuu,

Haujajibu hoja ndugu yangu. Sema kuna ukweli kwenye observation yangu au hakuna na utoe sababu!!!

Tiba
My God!,kweli ugonjwa huu wa kuhisi ni mbaya sana,unaweza kufa bure! huu ukweli hebu tuthibitishie wewe uliyekuja na hiyo hoja.
ushauri wangu jiunge na jukwaa la mapenzi na mahusiano kwa kuwa naona siasa haikufai kwa mtaji huu kwani ishakuchanganya akili.Hivi tutawaondoa mafisadi kweli hapa? kazi bado ipo.
 
Tiba.

Tafadhali elewa sio kila mtu ni mwanasiasa na mimi sipendi kabisa siasa, na kutokana na data zako unaonekana unaongea kwa hisia za kisiasa zaidi ya utashi ambao Mungu amekujalia na kama jina lako TIBA lilivyo.

Mfano mimi nimejiunga tangu 2008 fwatilia thread zangu so utaona kwamba unasukumwa na hisia zaidi.

Kama ni mapendekezo wafungie jukwaa la mapenzi pamoja na watu wake ambalo linachangiwa zaidi ili wabakie wanasiasa tu.

Ningeomba pia uongozi wa JF utoe tamko au jibu kwa TIBA kwa kukaa kimya inaweza kuwa mme msupport au mmemuignore kitu ambacho sio haki kwani hizo ni fikra zake.

Mkuu,

Nakushukuru kwa mchango wako lakini nasikitika umekwenda mbali kwa kutaka JF watoe tamko. Mimi nimeomba kama wanaweza kutoa data kusupport au kukanusha mawazo yangu. Very simple.

Najua post kama hii inawagusa wengi hapa na hasa wale waliojiunga kwa nia niliyoifikiria mimi (sijasema na wewe ni mmoja wapo lakini!).

Hizi ni fikira zangu tu sio lazima ziwe sahihi.

Tiba
 
we tibakyenda wewe, kwani lazima wote tuongee siasa? wengine hatutaki stress bado tu wadogo kufa na pressure, nchi yenyewe ishauzwa hii, kwa nini sasa tuendelee kujipa machungu? sisi na mahusiano na mapenzi tu maana ndo maisha yetu tunayoyaishi kila siku, so kama unapenda siasa nenda kwenye siasa, wanaopenda mapenzi waache kwa raha zao maana naona unawapa mods kibarua kisichokuwa na maana wakati yeye mwenyewe ndo alipanga jukwaa la siasa, elimu, mahusiano, habari mchanganyiko etc. so have peace bro.
 
Mkuu,

Nakushukuru kwa mchango wako lakini nasikitika umekwenda mbali kwa kutaka JF watoe tamko. Mimi nimeomba kama wanaweza kutoa data kusupport au kukanusha mawazo yangu. Very simple.

Najua post kama hii inawagusa wengi hapa na hasa wale waliojiunga kwa nia niliyoifikiria mimi (sijasema na wewe ni mmoja wapo lakini!).

Hizi ni fikira zangu tu sio lazima ziwe sahihi.

Tiba
Hizo fikra zako ni potofu, but in a way i understand you, you must be very stressed na politics, don worry it happens.
BTW karibu kule jukwaa la mahusiano , you should be ok after 30 minutes when you are there. Karibu.
 
My God!,kweli ugonjwa huu wa kuhisi ni mbaya sana,unaweza kufa bure! huu ukweli hebu tuthibitishie wewe uliyekuja na hiyo hoja.
ushauri wangu jiunge na jukwaa la mapenzi na mahusiano kwa kuwa naona siasa haikufai kwa mtaji huu kwani ishakuchanganya akili.Hivi tutawaondoa mafisadi kweli hapa? kazi bado ipo.


Mkuu asante kwa mchango wako. Je tutaupiga vita ufisadi kwa kutumia muda wetu kuchangia hoja za mapenzi? Au inawezekana sijakuelewa mkuu!!!

Tiba
 
Hizo fikra zako ni potofu, but in a way i understand you, you must be very stressed na politics, don worry it happens.
BTW karibu kule jukwaa la mahusiano , you should be ok after 30 minutes when you are there. Karibu.

Mkuu, naomba uthibitishe upotofu wa fikra zangu.

Tiba
 
Back
Top Bottom