Mimi nashauri jamii tuwe na utaratibu wa kusomesha watoto kama hawa yaani(adopting) wakati tukiendelea kuelimisha umma kuiondoa ccm 2015 ambayo imeleta adha hizi kwa watoto wetu
Kijana anaonekana si wa shida sana. Unajuaje kama hafanyi hiyo biashara baada ya shule au wakati wa likizo? Zamani tulikuwa tunawasaidia wazazi wetu shambani na bado wanafanya hivyo huko vijijini. Ilitutayarisha kwa ajili ya maisha ya kijijini. Tulijifunza kilimo, uvuvi, n.k. Huyo kijana anaweza kuja kuwa mjasiriyamali mzuri sana baadaye. Mimi nadhani hizi concepts kama child labour tuziangalie katika mazingira yetu badala ku-parrot yale tunayolishwa na wazungu. Mtoto wa kizungu akifua nguo zake inaweza kuwa child labour kwa sababu kwao kuna washing machine. Je wa kwako hutamfundisha kufua nguo zake kwa kuhofia label ya child labour? Washing machine unayo au uliishaiona?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.