Inasikitisha Jinsi Njaa na Tamaa Zinavyochafua Taifa: "Recharging Hope" Wameanika Mizengwe ya Rushwa waliyoikuta Tanzania

Inasikitisha Jinsi Njaa na Tamaa Zinavyochafua Taifa: "Recharging Hope" Wameanika Mizengwe ya Rushwa waliyoikuta Tanzania

Fascinating

Member
Joined
May 14, 2025
Posts
93
Reaction score
224
Kuna mfululizo wa dokumentari nilikuwa naufuatilia unaoonyesha safari ya timu ya Recharging Hope. Hawa ni vijana wabunifu, wanaosafiri kwa pikipiki zinazotumia umeme wa jua (Solar-powered electric motorcycles) kutoka Nairobi kuelekea Cape Town. Lengo lao ni kuonyesha kuwa teknolojia za kijani (Green Tech) zinawezekana Afrika kwa kutimiza azma ya kuendesha pikipiki kwa zaidi ya kilomita 6,000 kupitia nchi sita-Kenya, Tanzania, Malawi, Zambia, Botswana, na Afrika Kusini.
c643c813-4a94-49cf-8ba1-07ad00416e2c.png

Lakini kama kawaida yetu hapa nyumbani, huwa hatukosagi namna ya kujichafua. Yaani tumejishikiria, wamepita kote huko salama, lakini kimbembe kimeenda kuwakuta mwishoni kabisa mwa ardhi yetu. Hali hii inatia kichefuchefu na inacha maswali mazito juu ya uelekeo wetu kama taifa linalojinasibu kutaka maendeleo:

Urasimu wa Kipumbavu kupata huduma za Mipakani
Katika Episode ya 3, timu ya Recharging Hope imeweka wazi madhila yaliyowakuta mpaka wa Tanzania na Malawi. Wanasema walisota kwa zaidi ya saa nne kutokana na urasimu usio na kichwa wala miguu. Kibaya zaidi, wanakiri kuwa kuna watu walijaribu kuwatapeli (scam) mchana kweupe, jambo lililozua malumbano makali. Hii ni aibu ya kitaifa jamani! Badala ya kuwapokea kwa stara watu wanaotengeneza makala kwa tabasamu na kuwapa kila msaada ili kuitangaza nchi kwenye hizo Makala zao, sisi tunawatazama kama "fursa" ya kupooza njaa zetu na tamaa za muda mfupi.

Tunafukuza "Startups" na Kujichimbia Kaburi la Uwekezaji
Dunia haitusubiri. Startups na makampuni ya teknolojia yanatafuta mazingira ambako akili na muda wao vinaheshimiwa. Ikiwa watu wanapata "stress" ya kijinga na kukumbana na ukasuku wa kishamba wa maafisa wetu, nani mwingine atathubutu kuja akiiona hii Makala? Kwa tabia hizi, tusishangae kuona wawekezaji wakikimbilia nchi jirani ambako mifumo yao imetulia na haina "njaa" ya namna hii.

Tunaharibu Taswira ya Nchi Kimataifa (Reputational Damage)
Video hii inatazamwa na dunia nzima. Jamaa wameipa Title ya "Stopped by ICE in Tanzania???" ni pigo kwa utalii na diplomasia yetu. Inatengeneza taswira ya nchi "iliyooza" (rotted) kuanzia kwenye mifumo ya utoaji huduma. Hata kama tuna mibuyu mizuri na ukarimu wa watu wa vijijini kama jamaa alivyosema, uchafu huu wa maafisa wetu wa mipakani wanafuta mema yote yaliyotangazwa kupitia kwenye hiyo "Royal Tour".

Jamani tuache ushabiki usio na tija. Nchi yetu inahitaji mabadiliko ya kifikra kuanzia ngazi za chini hadi juu. Vinginevyo, tutabaki tunapiga makofi kwa mafanikio ya wenzetu huku sisi tukiishia kuwakamua na kuwakatisha tamaa wageni wachache wanaokuja na mwanga wa matumaini.

Tazama aibu hii hapa:
Stopped by ICE in Tanzania???

Wakuu, nawasilisha kwa uchungu mno!
ba699326-28ba-4a81-8956-03515c601475.png
 
Tatizo kubwa si hawa wageni waliokutana na changamoto mpakani, tatizo kubwa ni mfumo unaowazalisha maafisa wanaoona mgeni kama fursa ya kipato cha haraka badala ya fursa ya kuitangaza nchi.

Nchi nyingi zimejifunza kuwa mipaka yao ndiyo dirisha la kwanza la taswira ya taifa. Mtu akipokelewa vizuri mpakani, tayari nusu ya sifa za nchi zimejengwa. Lakini akikutana na urasimu, vitisho au ishara za rushwa, anabeba simulizi hilo kwenda kulisambaza duniani.

Hawa vijana wa Recharging Hope hawakuwa watalii wa kawaida; walikuwa wanabeba hadithi ya Afrika ya teknolojia ya kijani. Hiyo ilikuwa nafasi ya bure kabisa kwa Tanzania kuonekana kwenye ramani ya ubunifu.
Badala yake, tukawaweka kwenye simulizi ya kusubiri, kubishana na kutiliwa mashaka.

Hii ndiyo tofauti ya mataifa:
Wengine huona mgeni kama balozi wa sifa, sisi mara nyingi tunamwona kama pochi inayotembea.

Mpaka tukibadilisha fikra hii ya muda mfupi, tutabaki tunashangaa kwa nini wawekezaji wanapita karibu nasi lakini hawakai.
 
Tatizo kubwa si hawa wageni waliokutana na changamoto mpakani, tatizo kubwa ni mfumo unaowazalisha maafisa wanaoona mgeni kama fursa ya kipato cha haraka badala ya fursa ya kuitangaza nchi.

Nchi nyingi zimejifunza kuwa mipaka yao ndiyo dirisha la kwanza la taswira ya taifa. Mtu akipokelewa vizuri mpakani, tayari nusu ya sifa za nchi zimejengwa. Lakini akikutana na urasimu, vitisho au ishara za rushwa, anabeba simulizi hilo kwenda kulisambaza duniani.

Hawa vijana wa Recharging Hope hawakuwa watalii wa kawaida; walikuwa wanabeba hadithi ya Afrika ya teknolojia ya kijani. Hiyo ilikuwa nafasi ya bure kabisa kwa Tanzania kuonekana kwenye ramani ya ubunifu.
Badala yake, tukawaweka kwenye simulizi ya kusubiri, kubishana na kutiliwa mashaka.

Hii ndiyo tofauti ya mataifa:
Wengine huona mgeni kama balozi wa sifa, sisi mara nyingi tunamwona kama pochi inayotembea.

Mpaka tukibadilisha fikra hii ya muda mfupi, tutabaki tunashangaa kwa nini wawekezaji wanapita karibu nasi lakini hawakai.
Yani... Njaa imefanya tunaandikwa vibaya huko mitandaoni.... Hizi ni fursa ambazo tunapaswa kusemwa vizuri na sihivi tulivyosemwa... Tumelia hapa kutaka yule jamaa wa Mambio kuja bongo alafu nyuma ya Pazia tunasumbua watu wanaofanya makala ambazo tungeweza kuzitumia kujitangaza vizuri kwenye majukwaa ya kimataifa... Huzuni kwakweli
 
mada yako imekaa kisomi sana

Ndio maana haina wachangiaji

Humu leta mada za mapenz utashangaa uzi unavyopepea

Sio jambo la ajabu kwa nchi yetu kunuka rushwa kwenye hiz boarder wakiona mgen wanajua watapata chochote
Wewe kama unapenda mada za MMU pita kimya kimya watu wachukue madini😏
 
Hao ni miongoni tu wa walioonesha ushuhuda. Lakini mipakani,airport wageni huwa wanaombwa rushwa sana.

Nlikuwa na wageni siku moja tumeshuka airport wanaambiwa walipe dollar 100 bila sababu au watoe rushwa ya USD 50.,

Wakakubali tulipofika kwenye gari inatutoa airport wakanipa dollar 100( wawili) nimpelekee yule afsa wa kike wa airport. Nlivyofika nikampa elf 60 ya Kitanzania. Nlikuwa najua hana namna ya kunihoji ,(hata hii iliniuma)

Ile dollar nlikaa nayo mpaka ikataka kuchakaa😁😁😁,nlivyoenda bank kubadilisha kidogo waikatae. Hata haikuwa inaniuma pia
 
mada yako imekaa kisomi sana

Ndio maana haina wachangiaji

Humu leta mada za mapenz utashangaa uzi unavyopepea

Sio jambo la ajabu kwa nchi yetu kunuka rushwa kwenye hiz boarder wakiona mgen wanajua watapata chochote
Mzee acha kabisa.. ni aibu sana .. nimeshawahi kushuhudia wageni fulani wakipata usumbufu wa kulazimishwa kutoa so called tips . Aibu niliona mimi yaani
 
Kupita na gari kama umetokea south nchi ambazo niliona raha kwenye mipaka yao Botswana, Namibia na Zimbabwe unapita vizuri bila usumbufu na unachukua mda mchache. Sasa kuingia Zambia na Tanzania kuna usumbufu mkubwa sana wa kuombwa rushwa na kodi za ajabu ajabu. Hapo ikawa mwisho wangu na ni bora kupanda ndege tu kwa urasimu niliokutana nao.
 
Hao wawekezaji watakuja tu Wala usiogope watawala wenyewe wa ccm Hawa wakishapewa mlungula Nchi yote hii wanaiuza Kwa bei ya mkaa ,

So kuhusu investors usiogope watakuja tu ila ndio sio wawekezaji wanaoweza kuwekeza kwaajili ya maslahi ya watanzania
 
Wakuu, nawasilisha kwa uchungu mno!
Mboni wa wenyewe wameandika

16:54 - Border Post Chaos: Scams and Tensions in Malawi

Au ndio hapa Malawi unapopazungumzia, basi nimekuelewa nimeona jamaa mpaka anawaambia wenzie wazime camera ili watapeliwe vizuri
 
Anamaanisha Mafinga
Wamesema Mapunga, Tanzania elewa neno Mapunga, Tanzania unaelewa maana ya Mapunga, Tanzania? Fika mpaka pale dakika ya 13:50 mpaka 56 utaona wamechapa Day Ride 4 Mapunga, Tanzania yeah yeah yeah
 
Kuna mfululizo wa dokumentari nilikuwa naufuatilia unaoonyesha safari ya timu ya Recharging Hope. Hawa ni vijana wabunifu, wanaosafiri kwa pikipiki zinazotumia umeme wa jua (Solar-powered electric motorcycles) kutoka Nairobi kuelekea Cape Town. Lengo lao ni kuonyesha kuwa teknolojia za kijani (Green Tech) zinawezekana Afrika kwa kutimiza azma ya kuendesha pikipiki kwa zaidi ya kilomita 6,000 kupitia nchi sita-Kenya, Tanzania, Malawi, Zambia, Botswana, na Afrika Kusini.
View attachment 3558026
Lakini kama kawaida yetu hapa nyumbani, huwa hatukosagi namna ya kujichafua. Yaani tumejishikiria, wamepita kote huko salama, lakini kimbembe kimeenda kuwakuta mwishoni kabisa mwa ardhi yetu. Hali hii inatia kichefuchefu na inacha maswali mazito juu ya uelekeo wetu kama taifa linalojinasibu kutaka maendeleo:

Urasimu wa Kipumbavu kupata huduma za Mipakani
Katika Episode ya 3, timu ya Recharging Hope imeweka wazi madhila yaliyowakuta mpaka wa Tanzania na Malawi. Wanasema walisota kwa zaidi ya saa nne kutokana na urasimu usio na kichwa wala miguu. Kibaya zaidi, wanakiri kuwa kuna watu walijaribu kuwatapeli (scam) mchana kweupe, jambo lililozua malumbano makali. Hii ni aibu ya kitaifa jamani! Badala ya kuwapokea kwa stara watu wanaotengeneza makala kwa tabasamu na kuwapa kila msaada ili kuitangaza nchi kwenye hizo Makala zao, sisi tunawatazama kama "fursa" ya kupooza njaa zetu na tamaa za muda mfupi.

Tunafukuza "Startups" na Kujichimbia Kaburi la Uwekezaji
Dunia haitusubiri. Startups na makampuni ya teknolojia yanatafuta mazingira ambako akili na muda wao vinaheshimiwa. Ikiwa watu wanapata "stress" ya kijinga na kukumbana na ukasuku wa kishamba wa maafisa wetu, nani mwingine atathubutu kuja akiiona hii Makala? Kwa tabia hizi, tusishangae kuona wawekezaji wakikimbilia nchi jirani ambako mifumo yao imetulia na haina "njaa" ya namna hii.

Tunaharibu Taswira ya Nchi Kimataifa (Reputational Damage)
Video hii inatazamwa na dunia nzima. Jamaa wameipa Title ya "Stopped by ICE in Tanzania???" ni pigo kwa utalii na diplomasia yetu. Inatengeneza taswira ya nchi "iliyooza" (rotted) kuanzia kwenye mifumo ya utoaji huduma. Hata kama tuna mibuyu mizuri na ukarimu wa watu wa vijijini kama jamaa alivyosema, uchafu huu wa maafisa wetu wa mipakani wanafuta mema yote yaliyotangazwa kupitia kwenye hiyo "Royal Tour".

Jamani tuache ushabiki usio na tija. Nchi yetu inahitaji mabadiliko ya kifikra kuanzia ngazi za chini hadi juu. Vinginevyo, tutabaki tunapiga makofi kwa mafanikio ya wenzetu huku sisi tukiishia kuwakamua na kuwakatisha tamaa wageni wachache wanaokuja na mwanga wa matumaini.

Tazama aibu hii hapa:
Stopped by ICE in Tanzania???

Wakuu, nawasilisha kwa uchungu mno!
View attachment 3558027
Aina ya watu wenye uwezo ndogo wakufikiri ndio waendeshaji wa mipango mikubwa katika taifa...

Pascal Mayalla pengine waweza kuwakumbusha wahusika katika kazi yako kuwa mambo yamebadilika na wabadilike
 
Back
Top Bottom