Inaniuma kuiona Liverpool katika hali hii

Inaniuma kuiona Liverpool katika hali hii

Yieen

Senior Member
Joined
May 8, 2012
Posts
103
Reaction score
27
Ki ukweli Liverpool fc, ni timu yangu na ninaipenda sana tena kwa chati ya moyo wangu.. Ila kuna kitu kinacho ni kera katika msimu huu, kuona mchezaji Kama Raheem stering, anapewa nafasi ya kucheza mechi zote tena kwa Dk 90 lakin mwisho wa siku ana deliver upuuzi mtupu chenga nyiiingi,,mwisho wa siku tunafungwa...kiukwel hii Ali inaniuma sana ndugu zangu hamjui tu.
 
Mie nilishangaa sana walipoamua kumuuza Suarez kirahisi rahisi. Suarez pamoja na matatizo yake lakini aliipaisha sana L`pool na kuwa tishio kwenye EPL na mwaka huu kama angekuwepo basi wangetesa sana UEFA na EPL. Sijui kama ni Suarez mwenyewe alitaka kuuzwa au management baada ya ile incident kule Brazil wakaamua kumtema. Maamuzi ya kumuuza kwa maoni yangu ni makosa makubwa sana sasa timu imebaki kuwa mdebwedo. Yaani jinsi Suarez alivyoipaisha Liverpool msimu uliopita sikutaka kuikosa hata mechi moja ya Liverpool.
 
Na bado mtalia sana mwaka huu, si mlijifanya wajanga kumuuza suarez mkamnunua balloteli!!! sasa subirini mpigwe mkono na real madrid ndo mtazidi kulalamika kama mwanamke aliyefunganishwa...
 
Liverpool wataishia kuongelea historia, baada ya miaka 10 itakuwa historia kama leeds.
 
Mkuu sio ww tu, mimi mwenyewe hapa geto nimefunga dstv ili kupata maraha, lakini maraha wanapata wanaokuja chungulia na bahati nzuri jana usiku salio limekwisha na namshukuru mungu na silipii tena mpaka liverpool itakapoimarika washibiki wa chelsea wanakuja kufurahia chumbani huku mimi naumia
 
Teh teh liva yupo mwezini

ImageUploadedByJamiiForums1412431818.932484.jpg kikosi cha leo tunauwa
 
Mie nilishangaa sana walipoamua kumuuza Suarez kirahisi rahisi. Suarez pamoja na matatizo yake lakini aliipaisha sana L`pool na kuwa tishio kwenye EPL na mwaka huu kama angekuwepo basi wangetesa sana UEFA na EPL. Sijui kama ni Suarez mwenyewe alitaka kuuzwa au management baada ya ile incident kule Brazil wakaamua kumtema. Maamuzi ya kumuuza kwa maoni yangu ni makosa makubwa sana sasa timu imebaki kuwa mdebwedo. Yaani jinsi Suarez alivyoipaisha Liverpool msimu uliopita sikutaka kuikosa hata mechi moja ya Liverpool.

mkuu kuuzwa kwa Suarez sio sababu ya msingi ya kujitetea kushuka kwa kiwango cha liver kwan pesa walizopaTa walishindwa kusajiri mtu mwingine mwenye uwezo wa kuziba Pengo la Suarez
 
Suarez kiboko wewe!!! Unaweza kuwa na bulungutu la pesa lakini kumpata mcheza mwenye uwezo wa Suarez si rahisi kama unavyodhani vinginevyo akina Suarez wangekuwepo wengi katika kila timu. Halafu yeye na yule Sturridge walielewana katika safu ya mashambulizi kwa kiwango kikubwa sana.

mkuu kuuzwa kwa Suarez sio sababu ya msingi ya kujitetea kushuka kwa kiwango cha liver kwan pesa walizopaTa walishindwa kusajiri mtu mwingine mwenye uwezo wa kuziba Pengo la Suarez
 
Kama vipi mtimueni Brendan Rogers tumchukuwe yanga aje atufanyie kazi...
 
Mafanikio ya mwaka jana yana tu cost zaidi yahayo timu ipo kwenye mchanganyiko mpya nazani tutakaa sawa haikua tarajio letu tulipoishia mwaka msimu ulioisha sasa tim zinajipanga kwaajili yetu
 
Back
Top Bottom