In defense of Spika Ndugai

In defense of Spika Ndugai

comte

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2011
Posts
9,014
Reaction score
6,834
Akizungumza na Shirika la Utangazaji la BBC Idhaa ya Kiswahili ambapo mwandishi alimuuliza kama kabla ya kumuita kwenye kikao aliwashirikisha watu waliomteua.

“Suala hilo lipo katika mamlaka ya spika,kumuita mtu ni kumpa haki ya yakusilizwa hivyo watu wanapaswa waelewe vizuri kwa sababu wahusika wanaweza wakachukua hatua za kinidhamu lakini bado wananchi wakawauliza kama tulimisikiliza na ili mtu umsikilize lazima aitwe,kwa hiyo kuitwa ni jambo la kawaida na ni kwa mamlaka ya spika.

“Atafika hapa atakwenda kukutana na wabunge wenziye ambao watamuuliza maswali yatakayokuwapo na yeye atapata haki ya kujielezea ndani ya bunge si nje,kama haki ni ya kwako ivi kwa nini wenzako wakuonee, ”alisema Ndugai.

Alisema hawajakurupuka kumuita mbunge huyo kwakuwa ameitwa kwa mambo ya hapa nyumbani ambayo yanahusisha utovu wa nidhamu na si hayo yanayoendelea katika bunge la Afrika.

“Yeye anaunganisha hilo na matendo ambayo anayafanya ambayo pia yanatudhalilisha kama nchi,lakini hatujamuita kwa mambo ya Afrika Kusini sisi tumemuita kwa mambo ya hapa nyumbani ya utovu mkubwa wa nidhamu,watanzania watulie baada ya muda suala hilo litaletwa bungeni wataelezwa anatuhumiwa nini na majibu yake yalikuwa ni nini kwa sababu lazima liletwe bungeni hilo suala,”alisema Ndugai.

 
Waswahili husema methali "Achezae na tope humrukia" Ukistaajabu ya wabunge upinzani, CAG,P Mayala na Masele utayaona ya Ndugai.
 
Tunasubiri saa tano ifike mchezo uanze, leo ndiyo tabia zote za ndugai zitafahamika
 
Ndugai ana act utra vires, kama Masele ame- misbehave kwenye bunge la PAP basi Masele achukuliwe hatua kwa mujibu wa kanuni za PAP na si kanuni za bunge la JMT chini ya Ndugai.
"Fumadilu Kalimanzila, kwa mujibu wa gazeti la mtanzania- Ndugai anasema hawajakurupuka kumuita mbunge huyo kwakuwa ameitwa kwa mambo ya hapa nyumbani ambayo yanahusisha utovu wa nidhamu na si hayo yanayoendelea katika bunge la Afrika.
 
"Fumadilu Kalimanzila, kwa mujibu wa gazeti la mtanzania- Ndugai anasema hawajakurupuka kumuita mbunge huyo kwakuwa ameitwa kwa mambo ya hapa nyumbani ambayo yanahusisha utovu wa nidhamu na si hayo yanayoendelea katika bunge la Afrika.
Kama ilikuwa ni kwa ajili ya mambo ya hapa nyumbanii, kulikuwa na haja gani ya kumwita haraka haraka kana kwamba ni dharura fulani hadi kumwachisha vikao vya bunge la PAP? Kwa nini asingesubiriwa amalize kwanza vikao?
 
Kama ilikuwa ni kwa ajili ya mambo ya hapa nyumbanii, kulikuwa na haja gani ya kumwita haraka haraka kana kwamba ni dharura fulani hadi kumwachisha vikao vya bunge la PAP? Kwa nini asingesubiriwa amalize kwanza vikao?
hilo muulize aliyemuita
 
Back
Top Bottom