Imeniuma sanaa!

Kongosho wala usishangae kuna wadada/wamama kibao hapa nchini ambao akilini mwao wameandika kua mtoto lazima alelewe na baba. Baba hana kipato kikubwa, mama ana kipato kikubwa lakini yuko radhi aache kumlipia mtoto wake shule inayoeleweka maana anategemea baba afanye. Mtoto anaweza kuchelewa kurudi shule kwa sababu baba hajapata pesa, wakati mama anayo na hatalipa, ukimuuliza atakuambia baba yake hajaleta school fees. Vituko kama hivi viko kibao na wanaona ni sawa. Hivyo sioni ajabu huyu kulialia hapa kua hataweza kulea mtoto mwenyewe. Wakati anafungua miguu bila precaution sijui alitegemea nini.


Mwanachuo mzima ushindwe lea katoto kamoja? Hivi wengine mmekulia wapi?
Naona ni mie tu nimekulia kwenye mikiki mikiki, huu umayai unatoka wapi?

Kwa hiyo unashawishika kutoa?
 
amri ya sita usizini
ya tano usiue na kutoa mimba ni kuua ila ww ndio wa kuamua "Nakushauri usitoe hata kwa kushurutishwa"
 

sasa kama anajua hilo nani alimtuma afanye uzinzi kabla hajaoa???? au nani alimwambia apige kavukavu wkt anajua matokeo yake???? watu wengine bana
Naamini ukisema na moyo wako utaweza tu.......mbona single mom wapo wengi tu,wanafight na wanaweza tena wanamafanikio makubwa tu..... huyo asiyemtaka sasa hv atamtafuta baadae amkose

hiivi dunia ya leo kuna wanaume bado wanafikiria hayo wkt siku hizi hata kupata mimba ya kusingiziwa ni ngekewa kwa wengine??????
 
 
pole sana ndugu yangu wala usiitoe hiyo mimbakwani ukitoa utakuwa umeingia kwenye dhambi ya uuaji hivyo lea hiyo mimba zaa mtoto wako kisha umtunze kwani ndo matokeo yake hayo bestito lazima uyachukulie tuu
 
Mungu amekubariki with a chance ya kuitwa mama kwanini ukatae?usitoe mimba na endelea na maisha... its not going to be as hard as u think....ninavyopenda watoto halafu mtu anakataa wa kwake inaniudhi sana
 
Binafsi nimemwelewa sana Kongosho kwa ushauri wake
 
Acha kujilemaza…mimi nimeanza kusoma mtoto wangu akiwa na miezi 7 na sasa nshamaliza inshallah…na sijapata msaada wa mtu yoyote kwasababu babaake hahusiki kwenye lolote kwa hali wala kwa mali….kwahio kama wewe unataka kuzaa zaa na kama unataka kutoa utoe kwa ridhaa yako….
 

Sina cha kuongeza mamy umemaliza kila kitu kama wakuelewa ataelewa tu
 
wala ata usiumie,mi yalinitokea km yako na nilikua sijaanza ata chuo,sikutoa,nilizaa kababygirl kangu kana miaka mitano,yuko class one,alipoanza nursery ndo na mm nikapga shule,saiv nshamalza,nina kazi yangu,na babake ni mtu mwny ela bt mi nlikomaa nkamlea ivyoivyo kibish now tunakula tu gudtime na mrembo wangu,ye amebak tu kusema tusameane yaishe,mara shetan alimpitia,sa sijui alimptia waende wapi,gangamala mwanamke,mtoto ni zawadi ktoka kwa mungu,plz zaa,utaona faida ya uyo mtt,am proud to be a mother eti.
 
chuo kikuu uko matured sana ujue asa hizi habar za kuumia kwa majibu alitoa huyo kijana aiseee sio level zako kabisa yan hivyo angelalamika mtu wa o level vilee!!!!! by ze wi tulia leo mtoto ndugu wala usijar na akiwa zaliwa mtoto wa kike ahahahahaaa kuna mume wake huku ahahahahaaa usijareeeeeeeee bana kwani nini lea mimba mama maisha yanaendelea mungu ni mwema
 
pole sanah mkuhu hulitoha hujasiri huho wapi kabla kuholewa mkuhu???
 
Pole bidada, usiwaze namna ya kumlea mtoto. Automatically utapoteza mwelekeo wa maisha, ukijifungua salama utaona jinsi atakavyolelewa vizuri kushinda hata wanaopata malezi ya baba zao.
 
Kama ulitembea mguu pande na wewe inabidi uilee hyo mimba
 
Here we go again!! Anyway tafuta kuna manyuzi kibao humu yana maudhui kama yako. Inaonekana watu hawatojifunza kamwe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…