Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,440
- 1,029
Bosi mpya katika construction site aliamua kuonyesha yeye ni mchapakazi hodari kuliko wa zamani.Katika pita pita yake,akamkuta jamaa amelala kivulini muda wa kazi.Akamuuliza;wewe kijana,kwa nini umelala muda wa kazi?unalipwa sh.ngapi kwa mwezi?.Yule kijana akajibu;$4000 boss!.Bosi kwa hasira akaenda naye mpaka ofisini,akamlipa $4000 na kumtimua kazi muda ule ule.Baada ya hapo,bosi akaenda kuwauliza wafanyakazi wengine;yule kijana niliyemtimua kazi alikuwa anafanya kazi section ipi?.Jamaa wakamjibu;samahanibosi,unamaanisha yule jamaa muuza Ice-cream aliyekuwa amelala pale kivulini?