Katika hali ambayo haikutarajiwa na wengi Donald J Trump ameibuka na ushindi wa kutosha dhidi ya Hilary Clinton aliungwa mkono na Rais wa sasa na baadhi ya marais wastaafu. Kwenye uchaguzi huu kuna mengi nimejifunza hasa kuhusu wanaharakati wa haki za wanawake kwenye nchi za kiafrika. Wanawake wengi walikuwa wakimuunga mkono Clinton hata kuweka hashtag za I'm with her ila ukiwauliza kwanini wanamuunga mkono Hillary wanakuambia Hilary ni mwanamke, Can real be the reason to elect a person to the job seat? wamarekani wamesema hapana wao pia wana vigezo vyao na sio gender. Imekuwa kawaida kwa baadhi ya watu kupewa position ya flani hata kama wako weak kisa tu ni wanawake na matokeo yake ni kuharibu au kuvuruga kabisa taasisi wanazoziongoza au kutumiwa kulinda maslahi ya watu flanflani. Tunayo mifano mingi ya watu waliopewa madaraka kwasababu jinsia mfano mzuri Sitta alinyimwa uspika akapewa Makinda, Zakia Meghji alipewa uwaziri wa fedha kilichofuata kila mtu anaelewa, kule South Africa Spika mwanamke kila siku anamlinda Zuma dhidi ya Impeachment. Wamarekani wamesema kwa urais bado sana kumpa Hillary nafasi wanayotoa ya juu kwa wanawake ni Secretary of State.
Hata hivyo wanawake wakiafrica wangekuwa serious na wanawake wenzao kwenda ikulu basi Anna Mghwira na Martha Karua wangekuwa sasa hivi ni Maraisi wa Tanzania.
My Take Feminism is just a propaganda and it does apply out there sisi tu ndiyo tunaimba mapambio ya feminism.
Siamini katika matabaka ya kijinsia, "wanawake na wanawake wenzao" ni lugha dhiafu isiyo na dira.
Siamini katika mipaka ya fursa na haki inayolindwa kwa mipaka ya jinsia.
Naasikitika kwamba Wamarekani hawajasema ulichokiandika kwamba ""uraisi bado sana eti nafasi ya mwisho kwa wanawake ni secretary of state!." Hii ni ya kwako mwandishi.
Ninaomba nikuweke vizuri kwamba, kuchambua sifa za uongozi kwa misingi ya jinsia ni upotovu kwa sababu jinsia kama ilivyo haina vinasaba vya mchocheo wa ufanisi ama udhaifu. Masuala ya jinsia ni sanaa ya maafikiano katika jamii kuhusu uhusiano na nafasi za wanawake na wanaume katika masuala ya kijamii. Si jambo la kibailojia kwamba jinsia hii ina mtindio huu na hii haina.
Ni suala la kimazingira zaidi.
Ninatamani watu wangeona hoja kuu kuwa ni sifa na uwezo wa mtu badala ya jinsia kwa sababu kuna mianaume kibao ambayo imethibitisha kushindwa kumudu hada madaraka ya kuongoza familia.
Ni vizuri tukalitazama suala hili kwa mtazamo mpana wenye maana na maslahi sahihi ya team badala ya vigezo dhaifu.
Umetaja wanawake wachache tena ukabainisha kwamba walipewa madaraka kwa misingi ya jinsia. Ina wezekana jinsia ilikuwa lugha ya kupotezea wa maana ya kwamba alitakiwa mtu dhaifu kwa maslahi unayoyasema. Tunafahamu wote Ujasiri wa Marehemu Sita kwenye lile bunge kiasi kwamba likawekwa zengwe la kumpata atakayetumika.
Tunaposema maendeleo ya akina mama na fursa sawa hatuanzii kwenye madaraka na nafasi za uongozi. Ninaona hii falsafa inalenta mantiki zaidi kama ingejikita katika kuboresha ukuzi, ufahamu na uwezo wa watoto wote bila kujali jnisia ili kuleta ushindani sahihi usio na upendeleo wala ulaghai pale linapokuja suala la fursa.
Wanawake wana uwezo sawa na wanaume na mara nyingi wamethibitisha kuwa juu ziadi kwenye fani mbali mbali kama vile wanaume wlaivyothibitisha. Idadi ya wanawake wenye maandalizi sahihi ikiwa kubwa, bila shaka hii lugha ya kimaskini na udhalilishaji wa kijinsia kwa mama zetu itakufa kifo asilia.
Ninaunga na wewe. Wateuzi na wachaguzi waache kuharibu maslahi ya uma kwa kutoa fursa kwa upendeleo iwe kwa wanawake ama kwa wanaume kwa sababu mtu aliyepewa fursa bila vigezo hawezi kutumikia nafasi hiyo ipasavyo. Anaposhindwa ku deliver, inahkuwa ni kurudisha nyuma kasi ya ufanisi wa kundi na ni hujuma kwa wadau!.
Ninatamani nikupe mifano ya wanaume waliojipachika amakupachikwa nafasi za uongozi bila sifa na jinsi wanavyokuwa mizigo haramu kwa wadau. Bahati mbaya mazingira hayaruhusu lakini mwenye macho haambiwi tazama.
America wamechagua mtu kwa sifa wanazotaka lakini si kwa jinsia. Hawajamwacha Clinton kwa sababu ni mwanamke na wala hawajmchagua Trump kwa kuwa ni mwanaume. Wameamua kwa kuona Trump atawafaa kwa changamoto na hali zinazowakabli kwa sasa ukizingatia Clinton amekuwemo serikalni muda wote na serikali hiyo hiyo ndiyo iliyoifikisha Marekani mahala walipo.
America wanajua mabadiliko wanayoyataka. Naomba tuacha kuwalisha maneno ya kuwapgia ramli.
UPENDELEO WOWOTE UWE WA KIJINSIA, KINDUGU, KICHAMA N.K, USIPOZINGATIA UWEZO NA SIFA NI LAANA!
TUJIFUNZE KUPATA WATU WENYE SIFA SAHIHI NA UWEZO UNAOTAKIWA KWA MAJUKUMU TUNAYOWAPA.