Imani ya wa Marekani kwa Wanawake ina Mipaka

Imani ya wa Marekani kwa Wanawake ina Mipaka

Siamini katika matabaka ya kijinsia, "wanawake na wanawake wenzao" ni lugha dhiafu isiyo na dira.


Siamini katika mipaka ya fursa na haki inayolindwa kwa mipaka ya jinsia.


Naasikitika kwamba Wamarekani hawajasema ulichokiandika kwamba ""uraisi bado sana eti nafasi ya mwisho kwa wanawake ni secretary of state!." Hii ni ya kwako mwandishi.


Ninaomba nikuweke vizuri kwamba, kuchambua sifa za uongozi kwa misingi ya jinsia ni upotovu kwa sababu jinsia kama ilivyo haina vinasaba vya mchocheo wa ufanisi ama udhaifu. Masuala ya jinsia ni sanaa ya maafikiano katika jamii kuhusu uhusiano na nafasi za wanawake na wanaume katika masuala ya kijamii. Si jambo la kibailojia kwamba jinsia hii ina mtindio huu na hii haina.
Ni suala la kimazingira zaidi.


Ninatamani watu wangeona hoja kuu kuwa ni sifa na uwezo wa mtu badala ya jinsia kwa sababu kuna mianaume kibao ambayo imethibitisha kushindwa kumudu hada madaraka ya kuongoza familia.


Ni vizuri tukalitazama suala hili kwa mtazamo mpana wenye maana na maslahi sahihi ya team badala ya vigezo dhaifu.


Umetaja wanawake wachache tena ukabainisha kwamba walipewa madaraka kwa misingi ya jinsia. Ina wezekana jinsia ilikuwa lugha ya kupotezea wa maana ya kwamba alitakiwa mtu dhaifu kwa maslahi unayoyasema. Tunafahamu wote Ujasiri wa Marehemu Sita kwenye lile bunge kiasi kwamba likawekwa zengwe la kumpata atakayetumika.


Tunaposema maendeleo ya akina mama na fursa sawa hatuanzii kwenye madaraka na nafasi za uongozi. Ninaona hii falsafa inalenta mantiki zaidi kama ingejikita katika kuboresha ukuzi, ufahamu na uwezo wa watoto wote bila kujali jnisia ili kuleta ushindani sahihi usio na upendeleo wala ulaghai pale linapokuja suala la fursa.


Wanawake wana uwezo sawa na wanaume na mara nyingi wamethibitisha kuwa juu ziadi kwenye fani mbali mbali kama vile wanaume wlaivyothibitisha. Idadi ya wanawake wenye maandalizi sahihi ikiwa kubwa, bila shaka hii lugha ya kimaskini na udhalilishaji wa kijinsia kwa mama zetu itakufa kifo asilia.


Ninaunga na wewe. Wateuzi na wachaguzi waache kuharibu maslahi ya uma kwa kutoa fursa kwa upendeleo iwe kwa wanawake ama kwa wanaume kwa sababu mtu aliyepewa fursa bila vigezo hawezi kutumikia nafasi hiyo ipasavyo. Anaposhindwa ku deliver, inahkuwa ni kurudisha nyuma kasi ya ufanisi wa kundi na ni hujuma kwa wadau!.



Ninatamani nikupe mifano ya wanaume waliojipachika amakupachikwa nafasi za uongozi bila sifa na jinsi wanavyokuwa mizigo haramu kwa wadau. Bahati mbaya mazingira hayaruhusu lakini mwenye macho haambiwi tazama.


America wamechagua mtu kwa sifa wanazotaka lakini si kwa jinsia. Hawajamwacha Clinton kwa sababu ni mwanamke na wala hawajmchagua Trump kwa kuwa ni mwanaume. Wameamua kwa kuona Trump atawafaa kwa changamoto na hali zinazowakabli kwa sasa ukizingatia Clinton amekuwemo serikalni muda wote na serikali hiyo hiyo ndiyo iliyoifikisha Marekani mahala walipo.


America wanajua mabadiliko wanayoyataka. Naomba tuacha kuwalisha maneno ya kuwapgia ramli.


UPENDELEO WOWOTE UWE WA KIJINSIA, KINDUGU, KICHAMA N.K, USIPOZINGATIA UWEZO NA SIFA NI LAANA!


TUJIFUNZE KUPATA WATU WENYE SIFA SAHIHI NA UWEZO UNAOTAKIWA KWA MAJUKUMU TUNAYOWAPA.
Usiamini lakini ukweli ndio huo, mwanamke kitandani na jikoni hayo mengine wanajitiatia tu
 
Usiamini lakini ukweli ndio huo, mwanamke kitandani na jikoni hayo mengine wanajitiatia tu

Hizo ni akili zako zisizotaka kuona ukweli. **** mianaume myenzangu kibao haiwezi hata kutunza familia. Mipango yote ya familia na akili za mafanikio zinatoka kwa mwanamke. Watoto wasome wapi na taratibu zote hata mahusiano na majirani anasimamia mwanamke. Mwanamme ni jina sauti na suruali!.

Bahati mbaya mianaume failures ndiyo inayotuaibisha hata mitandaoni kujiweka nafasi za mbele kuliko wa mama. Inajianika namna gani hata vichwa vyake haviwezi kufikiri.

Wewe kama umeoa mkeo au mama yako ni mbumbumbu wa kitandani na jikoni, hilo ni tabaka lako lakini siyo la wote.
Bila shaka utaona hata namna gani mkeo hawezi kuwa sawa na mke wangu na namna mawazo na uelewa wako hauwezi kuwa sawa na wangu ingawa sote ni wanaume.

Mkeo au ufahamu wako hauwezi kuwa rula ya dunia.
 
Hii ni moja wapo ya silaha za kutudumaza waafrika kimaendeleo, hakuna Taifa liloendelea duniani mwanamke anapewa nafasi kama wanavyotaka tuwape sisi hapa kwetu!

Nakubaliana na hili, mimi ningependelea kwanza Afrika iendelee karne kadhaa hivi, kiuchumi na kila nyanja ili likishafanikiwa tuwape wanawake nafasi kwa upendeleo kama vile hayo hayo mataiafa yaliyoendelea yalivyoanza hapo awali hadi kufikia walipo hivi sasa!
Kuna harufu kali ya hujma dhidhi ya Afrika!
 
I'm sorry kusema haya lakini saa zingine inapobidi ukweli ni lazima usemwe tu, no matter what, hilo la kumshadadia mama Clinton kisa tu kwamba ni mwanamke ni unafiki tu...
kama kweli wanapenda na wanawaunga mkono wanawake wenzao kushika madaraka makubwa ni kwa nini mwaka jana hawakumchagua mama Anna mghwira..? ukizingatia kuwa wao ndiyo wapiga kura wengi kabisa....?
 
Back
Top Bottom