Ilikuwa LAZIMA wafanye hivi, vinginevyo…

Ilikuwa LAZIMA wafanye hivi, vinginevyo…

Makumbele

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2009
Posts
243
Reaction score
1,060
Tafakari haya:

1. Watanzania walio wengi hawakupiga kura

2. Wachache waliojitokeza walifurumshwa na Gen Z.

3. Mawakala hawakuwepo tena.

4. Waliojiandikisha ni 37M na CCM wenyewe hawana wanachama hata milioni 10. Je, kura 32 milioni za Samia zimetoka wapi?

5. Bila intaneti, wamesafirishaje matokeo?

Kwanini wamelazimisha?

Si suala la Samia anymore, ni suala la CCM, Kundi Mtandao (alilolisema ndugu Polepole) kwani anguko halingekuwa la Samia tu; na hatari mbele ni CCM kufa mazima.

Wamejichimbia mizizi majeshini, hivyo uchafu wao unawagusa wakubwa wengi kwenye vyombo hivyo.

Ni zaidi ya Samia, ni zaidi ya CCM! Tuna safari ngumu, ila ni mwanzo wa mwisho usiotarajiwa hata na CCM yenyewe
 
Naamini hilo.

Mwanza JWTZ limewaambiwa wananchi waache mara moja kuandamana na pale lilikuta watu wamekusanyika lilikuwa linawalazimu kuondoa mawe matyre nk barabarani.

Kwa kifupi maandamano ndo yatakoma hivyo na yamekuwa hayana maana hasa sisi kwa tulichokuwa tunadai.

Tutegemee kuibiwa zaidi na kuishi maisha magumu kuliko kawaida!!
 
Kwani akiwa keshatangazwa hawezi kuondolewa?

Mmeshakufa moyo!
Kama imewezekana kutangazwa mbele yao maana yake wamekubaliana na hilo kwa 100% kuna haja gani ya kuendelea kusubiri raia wanakufa na wamefungiwa ndani hakuna kutoka internet hakuna je kuna ulazima gani huo?
 
1000187721.jpg
 
Kama imewezekana kutangazwa mbele yao maana yake wamekubaliana na hilo kwa 100% kuna haja gani ya kuendelea kusubiri raia wanakufa na wamefungiwa ndani hakuna kutoka internet hakuna je kuna ulazima gani huo?
Rajapaksa kule Sri Lanka alipoondolewa alikuwa yupo madarakani.

Sheikh Hasina naye hivyo hivyo.

Mubarak pia.

Kwanini ukate tamaa haraka hivyo?
 
Tunashukuru Mungu nchi imepata Rais, na maandamano yameisha.

Sasa ni Rais kuapishwa, kuunda serikali na itakayowatumikia watu wote kwa bidii...
 
Eti ni judge ndio katangaza, kweli wasomi wa Tanzania is something! Hata kama huna akili hata machale tu huna?

Japo uunde uongo ufanane na chembe ya ukweli? Hata Yesu mwana wa Mungu asingepata 98% kwa namna yoyote, tunajiunda kuwa pariah wa dunia yani!

Aibu sana kuwa msomi wa kitanzania desa's country
 
98% Is some Kim Jong Un of North Korea number.
 
Huyu ni wa kupingwa kila kona, hafai na hajashinda kwa hizo takwimu za kupika.
 
Kuna shinikizo la kutangaza huo uchaguzi, trust me, uonevu wa kijinga hautakuja kutokea tena , na utaona waliobambikiwa kesi wote kuachiwa na kuanza mchakato wa katiba mpya.

Kuanzia leo ule ujinga wa Muliro eti vikosi vyetu vimejipanga, ohh mkiandana tutaeanya hivi, sijui kesi za uchochezi hazitakuwepo.

Trust me tume shinda pakubwa.
Ujue mchawi mkubwa zaidi ambae alikuwa ana dharau watanzania ambae amekuwa akiongoza Tanzania kwa kivuli cha Samia ni Kikwete, yeye mwenye kakubali huu mziki wa sasa, yeye na mpenzi wake walikuwa Kenya kuomba msaada na ushauri.

Hii kuonea wapinzani ndio mwisho wake huu, huwezi kupata changes duniani kote kwa kuchekeana.

Kwa taarifa nilizo nazo Samia amepewa conditions na USA kuwa atangazwe haraka na atimize hayo masharti haraka, ndio maana umewaona hawana hata furaha, tume toa Jasho.
 
98% Is some Kim Jong Un of North Korea number.
Yaani kamuzidi hadi magufuri... hata kama ni uchakachuaji, basi wangeona aibu.. yaani kura za Samia ni zaidi ya JPM, hiyo bado haiingii akilini...
 
Tafakari haya:

1. Watanzania walio wengi hawakupiga kura

2. Wachache waliojitokeza walifurumshwa na Gen Z.

3. Mawakala hawakuwepo tena.

4. Waliojiandikisha ni 37M na CCM wenyewe hawana wanachama hata milioni 10. Je, kura 32 milioni za Samia zimetoka wapi?

5. Bila intaneti, wamesafirishaje matokeo?

Kwanini wamelazimisha?

Si suala la Samia anymore, ni suala la CCM, Kundi Mtandao (alilolisema ndugu Polepole) kwani anguko halingekuwa la Samia tu; na hatari mbele ni CCM kufa mazima.

Wamejichimbia mizizi majeshini, hivyo uchafu wao unawagusa wakubwa wengi kwenye vyombo hivyo.

Ni zaidi ya Samia, ni zaidi ya CCM! Tuna safari ngumu, ila ni mwanzo wa mwisho usiotarajiwa hata na CCM yenyewe
Walisema wana wanachama milioni kumi na tatu
 
Huwa wanang’olewa hata katikati ya muhula. Fighting spirit tu ndiyo inayohitajika!
Kimsingi hiyo fighting spirit kwasasa ndiyo iko on more than that.

Kwa hapa tulipo ikitokea CCM wakaacha kuja na Unite program wajue muda wowote kitawaka zaidi ya ilivyokuwa ,watu washauchungulia udhaifu wa serikali kwenye kupambana na waharifu .

Hii show ya sasa kwa karibu 98% imepigwa na Gen-Z ,unadhani ingelikuwaje kama ingelipata na ile Generation nyingine.
 
Back
Top Bottom