Ili kukuza muungano tugawane sawa kwa sawa na Zanzibar

Ili kukuza muungano tugawane sawa kwa sawa na Zanzibar

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,144
Reaction score
48,368
Hii ndiyo njia sahihi. Kama Kuna mabalozi 40 basi 20 wawe toka Zanzibar na 20 watoke Tanganyika.

Kama tukikopa hela kwa jina la Tanzania basi zigawanywe nusu kwa nusu.

Kama kuna ajira 1000 kwenye Serikali ya Tanzania basi mgao uwe ni nusu kwa nusu.

Hii itaimarisha muungano wetu.
 
Hapo hesabu zinakataa, ikifanya hivyo wazenji watanufaika zaidi maana kwa idadi ya watu wao wapo chini sana, sidhani kama wakazi wote wa Zanzibar kwa idadi yao wanawazidi wakazi wanaoishi Mwanza kwa mfano.
Tatizo liko wapi? Mtaanza kusema wasukuma ni wengi sana kuliko wandengereko. Wazanzibari ni watanzania kama watanzania wengine tu.
 
Hilo nalo haliwezekan
Labda ili kuondoa msuguano ni lazma kuwepo na serikali tatu na kila mmoja ajue mipaka yake
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika
Na
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
 
Hii ndiyo njia sahihi. Kama Kuna mabalozi 40 basi 20 wawe toka Zanzibar na 20 watoke Tanganyika.

Kama tukikopa hela kwa jina la Tanzania basi zigawanywe nusu kwa nusu.

Kama kuna ajira 1000 kwenye Serikali ya Tanzania basi mgao uwe ni nusu kwa nusu.

Hii itaimarisha muungano wetu.
Yaani umesemaje? Kwa kwa sasa mnagawanaje?
 
Ili muungano udumu dawa ni moja tu, kuchukua wazanzibari wote kuwaleta mikoa tofauti tofauti ya bara kisha kuchukua wabara mil 1 kuwapeleka unguja na pemba
 
Back
Top Bottom