Tz kweli hakuna maono ya kibiashara. Hizi fukwe zote za Dsm, Pwani, Znz/ Pe, Mtwara na Ta, zingekuwa ni vituo vya kitalii cha kimataifa. Wazungu wanasafiri kwenda kwenye visiwa na fukwe mbali mbali hasa sehemu za joto kama hapa kwetu, sisi ni kupiga marufuku kila kitu, au huyu anaruhusu na kufanya ugoigoi mpaka anatoka madarakani mradi haujakamilika, akija mwenzake, amri za marufuku na kupitia upya Miradi zinaanza. Miradi ya maendeleo iwe ni sera za miaka hata 50, sio makubaliano ya rais aliyepo madarakani akiondoka na kila kitu kinasahaulika, iwe ni mwendelezo.