OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 457
- 773
Nimetumia muda kusoma ilani ya Uchaguzi ya CCM, sio kwa ubaya lakini nawaza inakuwaje kama mtu unakuwa na maswali dhidi ya utekelezaji wa Ilani. Maana kikubwa kilichopo ni ahadi za kuleta ajira, kukuza utalii na kuongeza mikopo nk. Lakini mambo yote haya hayajaweka ni kwa namna gani vitu hivi vitatimizwa.
Mathalani, suala la kujenga barabara haijaweka hizo hela zitapatikana wapi? Je ni wananchi watatozwa kodi zaidi au tutakopa zaidi na vizazi vije vilipe hela hizo kwa kodi kubwa. Aidha masuala ya utu hayajatafsiriwa kwamba hiyo "kazi na utu" utu unakuzwaje?
Ahadi nyingi zilizoweka hazijaweka gap, kwamba uhitaji ukoje, changamoto ni nini na itataliwaje. Bali imewekwa tu tutajenga barabara, tutajenga madarasa na hospitali.
Yote hii inarudi kwenye msingi wa kukosa falsafa ya kutimiza ahadi hizi. Yaani CCM akisema anajenga Barabara, na ACT akasema anajenga barabara, wananchi wanawezaje kuichagua ilani husika ikiwa haiko wazi kwenye mpango wa kutimiza mambo yaliyoahidiwa. Hapo ndipo unapokuta utapeli.
Nadhani vyama ambavyo havijatoa ilani vijikite kwenye kuonesha gap lililopo na namna watakayotumia kutatua changamoto zilizopo badala ya kuweka ahadi bila kuwa na mpango wa namna gani ahadi hizo zitatimizwa.
Nawasilisha.
Mathalani, suala la kujenga barabara haijaweka hizo hela zitapatikana wapi? Je ni wananchi watatozwa kodi zaidi au tutakopa zaidi na vizazi vije vilipe hela hizo kwa kodi kubwa. Aidha masuala ya utu hayajatafsiriwa kwamba hiyo "kazi na utu" utu unakuzwaje?
Ahadi nyingi zilizoweka hazijaweka gap, kwamba uhitaji ukoje, changamoto ni nini na itataliwaje. Bali imewekwa tu tutajenga barabara, tutajenga madarasa na hospitali.
Yote hii inarudi kwenye msingi wa kukosa falsafa ya kutimiza ahadi hizi. Yaani CCM akisema anajenga Barabara, na ACT akasema anajenga barabara, wananchi wanawezaje kuichagua ilani husika ikiwa haiko wazi kwenye mpango wa kutimiza mambo yaliyoahidiwa. Hapo ndipo unapokuta utapeli.
Nadhani vyama ambavyo havijatoa ilani vijikite kwenye kuonesha gap lililopo na namna watakayotumia kutatua changamoto zilizopo badala ya kuweka ahadi bila kuwa na mpango wa namna gani ahadi hizo zitatimizwa.
Nawasilisha.