ILANI:ukiswali huu msikiti uwe na pesa!

ILANI:ukiswali huu msikiti uwe na pesa!

Safi sana kuna watu wakaidi sana linapokuja suala la kuzima simu zao na hata Imam awakumbushe kabla ya sala zimeni simu zenu, cha ajabu mko katikati ya sala simu inaita.

Cha ajabu hao hao wanaokuwa wakaidi kuzima simu zao wanapokuwa mahakamani/benki au mahala pengine wanatii sana kuzima simu zao

Tunashindwa kujiongoza wenyewe bila kumuona askari na mtutu. Mbaya sana.
 
Hela inaingia katika mfuko wa msikiti.... Lazima kuwe na utaratibu
 
Mwaka jana watu wako kwenye swalaa, simu ya jamaa mmoja ikaita ina wimbo wa Rose Mhango unaosema "NIBEBE, NIBEBE BWANA YESU NIBEMBELEZE". ilikuwa ni kashikashi ndani ya msikiti.

karate itakuwa zilihusika humo ndani mbaya zaidi sheikh awe Ponda.
 
Buku tano? Hahahaha mkwara mwingine bhana. Sometimes viongozi wa dini wanatakiwa wawe strict namna hii, inapendeza sana, hebu imagine ndio unafunga swala halafu simu inaita, Yesu nibebe, nibeebe, nibembelezeee......unaharibu swala nzima

Ahahahahahaaaa
 
Muhasibu wa Kutwanga Faini Wasiosikia?
We kweli Mtoto wa Jongo.
Unachokisema kinaweza kikawa sawa lakini unakosa vifuatavyo
1. Anayehusika kukusanya hela na kutunza mahesabu ni mhasibu... Anaweza akawa anawatu wanaomsaidia kwa namna moja au nyingine, lakini mwisho wa siku hesabu zote za fedha na matumizi zinakaa kwake..
2. Inawezekana kabisa hujui au unafanya kusudi kutojuwa kwamba misikiti hainaga wahasibu... hence ndo inakuwa sababu kubwa ya watu kugombea uimamu wa maisiki mbalimbali
3. Jongo naye anafaa kuwa baba... Inawezekana wewe kwa uwezo wako wa kufikiri ukaona hafai na wala hatakiwi kuwa na watoto..
4. Kumbuka uwezo wa Jongo kuzaa au kutozaa hakuna uhusiano na akili yake... NB hata vichaa nao huwa wanazaaa
5. Wewe usiye mtoto wa Jongo unaweza kabisa ukawa na matatizo yasiyotokana na kuzaliwa na Jongo... Mazingira na makuzi yako yanajenga tabia ya mtu husika.... Ndiyo maana si ajabu kukuta familia ya baba mmoja kuna Madhehe, mapadre, wachungaji , majambazi na wavuta bangi kibao... Au baadhi wakawa na mchanganyiko wa hayo

 
Hawanaga wahasibu wa misikiti hao sijui hela atapewa anani.....
Hapewi mtu inaingia kwenye kamati ya msikiti ambapo pesa hiyo itasaidia kama kutakuwa na marekebisho(ukarabati), na hata itakapotokea kununua vifaa n.k
 
Tunashindwa kujiongoza wenyewe bila kumuona askari na mtutu. Mbaya sana.
Umeona hapo ndugu!

Haya basi tufanye wewe unaogopa au hutaki kuzima simu yako basi ondoa mlio iwe kimya kimya utakapomaliza swala utakuta missed calls kisha utaanza kuzirejea moja baada ya nyingine
 
Hapewi mtu inaingia kwenye kamati ya msikiti ambapo pesa hiyo itasaidia kama kutakuwa na marekebisho(ukarabati), na hata itakapotokea kununua vifaa n.k

As far as I know, kwenye RC kwenye kila level, kuanzi jumuiya, mtaa, kigango, parokia jimbo etc etc kuna mwenyekiti na msaidizi wake, katibu na msaidizi wake na mtunza fedha. Hao kwa pamoja wanaitwa kamati tendaji ya sehemu husika eg. kamati tendaji ya jumuiya fulani..

Hiyo kamati ya msikiti ina viongozi wepi? Au wote wapo level moja? eg wana mtunza fedha au anayefanana na cheo hicho..??
 
hizo pesa wanazokusanya wanazipeleka wapi au ndo zawadi ya shehe aliyekuwepo.
 
Back
Top Bottom