engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,149
- 1,441
Wapiganaji wa kundi la wanamgambo la Al Shabaab nchini Somalia meshambulia Ikulu ya Rais katika mji mkuu Mogadishu.
Umoja wa mataifa unasema umefahamishwa kuwa rais wa nchi hiyo hakujeruhiwa na yu salama na kwamba shambulizi la wanamgambo hao lilitibuka.
Waziri wa mambo ya usalama wa nchi hiyo Abdi Karim Hussein, amesema baadhi ya washambuliaji wamefariki na wengine kukamatwa.
Kundi la Al- Shaabab linalopigana na utawala nchini humo limedai kuhusika na shambulio hilo na kusema makabiliano yangali yanaendelea.
Walianza mashambulizi yao, kwa kutumia gari lililokuwa na bomu ndani yake kwa kuliegesha kando ya ukuta na kisha kuanza kupigana ili kuweza kuingia ndani.
Milipuko mikubwa ilisikika pamoja na milio ya risasi.
Majeshi ya muungano wa Afrika yamekuwa yakipambana na wapiganaji hao na hata kuwafurusha kutoka mji mkuu Mogadishu. Hata hivyo bado wanadhibiti sehemu nyingi nje ya Mogadishu
Chanzo:http://www.bbc.co.uk/swahili/habari/2014/02/140221_alshabaab_ikulu.shtml
UPDATE:
- ‪Somalia Govt officials say all ‪Shabab‬ attackers have been killed, but gunfire can still be heard inside the Presidential palace.
-All roads leading to the presidential palace in Mogadishu closed by Amisom & govt troops, no Journalists allowed to go near the scene
-Al-Shabaab militants say they attacked the presidential palace "in order to kill or arrest those who are inside
