Ikifika 40 years kama hujafanikiwa ni ngumu kutoka...

Hivi inaweza kuwa kweli ukifika umri wa 40,na hakijaelweka(kufanikiwa kimaisha) ni ngumu kufanikiwa(utajiri) baada ya apo?karibuni kushare .
bado kabisa miaka 40 Tz c ndiyo hata huruhusiwi kugombea uraisi
 
Kwa wale ambao wanapenda vya kurithi wanaogopa kuwa wakingojea mpaka baba afariki wanaweza kukuta vizuri vimekwisha. Hence, miaka ikiisha vuka 40 uwezo wa kuupamba mji kwa vimwana unakuwa haupo.
Najua moja tu;
Hata kama sikuzinyaka miye niliwaandaa watoto wangu nao sasa ni watu wenye vyao, huyu akileta laki 2 mwenziye anarusha 3 na mwingine anarusha 3. Tiyari kwa mwezi, bila hata kukatwa vat naingiza 8 yangu taratiiib bila jasho wala mkwara. Jioni, naning'inia juu ya stuli sina bp na mtu. Nyumbani wananikaangia kiti moto yangu. Mama akilia naumwa wanae wanakuja msomba ka mzigo wakimgombania ka mpira wa kona. Miye si ndo zaidi?? Sidhani kama kuna utajiri mkubwa kama watoto wakifanikiwa. Mtaji wa maskini, watoto asikudanganye mtu kitu. Tunza watoto uliozaa.
 
Back
Top Bottom