GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 63,059
- 126,639
Akizungumza kwa ‘ Mikogo ‘ kama kawaida yake Bungeni leo alipokuwa akiwasilisha Bajeti ya Wizara yake Waziri mwenye dhamana na masuala ya Michezo nchini ‘ Msomi ‘ wa hali ya juu Dkt. Harrison Mwakyembe ametoa sababu Kuu Tatu ambazo ndizo zimefanya Timu ya Taifa ya Vijana ya ‘ Serengeti Boys ‘ kufanya vibaya katika hii Michuano inayoendelea nchini.
Si vibaya tukizijua hizo sababu Kuu Tatu ( 3 ) za Waziri ‘ Msomi ‘ wa ‘ PhD ‘ Mwakyembe alizozitoa leo Bungeni…..
Shikamoo sana Waziri Dkt. Mwakyembe.
Nawasilisha.
Si vibaya tukizijua hizo sababu Kuu Tatu ( 3 ) za Waziri ‘ Msomi ‘ wa ‘ PhD ‘ Mwakyembe alizozitoa leo Bungeni…..
Serengeti Boys imefanya vibaya kwakuwa Mawakala wa akina El Haji Diof na Samuel Eto walianza Kuwarubuni na Kuwaahidi Mipesa Kibao.
Serengeti Boys imefanya vibaya kwakuwa Wazazi wa hawa Wachezaji walishaanza Kuwakopa Watoto Wao Hela kwakuwa walishasikia kuwa Watoto Wao hao wanaenda kuwa Matajiri hivyo ikawaathiri Vijana Kisaikolojia.
Serengeti Boys imefanya vibaya kwakuwa kuna Watanzania wengine baada ya kusikia hawa Vijana wameahidiwa Pesa nyingi hao Watanzania walianza kuwaonea Wivu / Kijicho hawa Vijana hali ambayo ilianza kuwawekea Nuksi na wakaharibu kabisa.
Shikamoo sana Waziri Dkt. Mwakyembe.
Nawasilisha.
