Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,898
- 942
MBUNGE NGASSA: "IGUNGA MLITUPA KURA, TUNAWALIPA MAENDELEO"
Mbunge wa Jimbo la Igunga Mhe. Nicholaus George Ngassa, amefanya Ziara ya Kikazi Jimboni kwa kufanya Ziara kwenye Vijiji vinne vya Kata za Mwamashimba na Mwamakona.
Mheshimiwa Ngassa (MB) amefanya Mikutano Kwenye Vijiji vya Mwanyalali, Mwamashimba, Imalanguzu na Mwamakona na kuwashukuru Wananchi kwa kuiunga mkono Serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika kusimamia Miradi ya Maendeleo inayotokana na Fedha zinazotegwa na kupitishwa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
"KAZI NA MAENDELEO"
Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Igunga
20 Mei, 2023