IGUNGA - Bila Mwl. Kashindye CHADEMA inajichimbia KABURI

IGUNGA - Bila Mwl. Kashindye CHADEMA inajichimbia KABURI

kibogo

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2012
Posts
9,739
Reaction score
4,745
Leo kuna upigaji kura ya maoni ya kuteua atakaye peperusha Bendera ya CHADEMA kwa nafasi ya Ubunge jimbo la Igunga, ninapenda kuchukua nafasi hii kuelezea hali halisi na kinachotaka kufanyika hapa Igunga.

Kuna njama za makusudi zimepangwa na kuratibiwa na baadhi ya viongozi ili kuhakikisha Mwl.Kashindye apati nafasi ya kugombea Ubunge kwa awamu hii akiwemo na kiongozi mkubwa aliyejitanabaisha kuwa ana mapenzi na CHADEMA Igunga .

Ikumbukwe Mwl. Kashindye alijiondoa kwenye utumishi wa Umma kama Mkaguzi wa Elimu Wilaya na kuingia kwenye Siasa huku akipoteza rasilimali zake, muda wake na kujiweka kwenye hatari kwani CCM hawakuwa tayari kumuona yupo kwa jinsi alivyoichachafya wakati wa uchaguzi mdogo.
Kinachosikitisha na kuhudhunisha ni baadhi ya viongozi wanadiliki kuweka wazi na kusema Mwl.kashindye kwa sasa hana fedha hivyo hata wakimpitisha hataweza kushinda huku watu hao hao wakiwa hawana kumbukumbu kuwa waliweza kushinda nafasi walizopo sasa bila wao kutumia fedha isipokuwa ni wanachama na wananchi walio na mapenzi mema na CHADEMA ndio walijitolea mali zao kukichangia chama hadi kufanikisha kushinda nafasi hizo.

Napenda kutoa angalizo kwa uongozi makao makuu wawe makini sana na suala hili hapa Igunga kwani kukua kwa kasi kwa CHADEMA Igunga hasa wakati wa uchaguzi Mdogo wa Marudio haikuwa kwa sababu eti CHADEMA kilipendwa au kinapendwa sana, sababu kuu ya yote hayo ilitokana na ujio wa Mwl.kashindye kwa kujitoa kwenye utumishi wa umma na kuamua kugombea Ubunge kwa lengo la kuwakomboa wana Igunga kwani alipata support kubwa sana kutoka kwa watumishi wa Umma na hasa walimu kwani hawakuwa tayari kumuangusha Mwalimu mwenzao na pia ni huyu huyu kashindye aliyefanya kazi ya Ziada kama mwenyekiti wa CDM Wilaya kuweza kufanya kampeni zilizozaa matunda ya Igunga kupata viti vingi vya wenyeviti wa Vitongoji na vijiji katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Ni vema ikaeleweka wazi hawa vijana waliokuja kugombea sasa wote sio wenyeji wa Igunga na hawaishi Igunga, mmoja anakaa Kahama na mwingine anaishi Dar es salaam na wananchi wa Igunga kwa sasa wameweka wazi hawako tayari kumchagua mtu anayetoka mbali na kuja kupitia Ubunge na kutokomea zake pasipo kuwa pamoja na wananchi kwenye shida na raha.

Kwa Igunga napenda kuweka wazi kama jina la Mwl.Kashindye alitapitishwa ni vema Uongozi makao makuu ukafanya mapinduzi ili kurejesha jina lake kwani pasipo kufanya hivyo CHADEMA itakuwa imejiondoa rasmi kwenye ushindani na itapoteza nafasi za huo Ubunge na hata udiwani kwani wananchi hawatakuwa na imani tena kwa chama kwani itakuwa imeonyesha kutothamini mchango pale mtu anapojitoa kwa moyo wake wote kwenye chama.

Nawasilisha!!
 
Kashindye ashiriki kura za maoni na awe tayari kukubaliana na maamuzi ya vikao. Chadema sio mtu mm
 
Huo nimtazamo na mawazo yako finyo

Hakuna unachokijua ni vema ukakaa kimya, na ninachokuomba uweke kumbukumbu zako vema kama Mwl. kashindye asipopitishwa uje tena hapa baada ya uchaguzi unlete majibu ya kitakachotokea na hapo ndipo tutajua mwenye mawazo finyu ni mimi au wewe.
 
Kashindye ashiriki kura za maoni na awe tayari kukubaliana na maamuzi ya vikao. Chadema sio mtu mm

Hata Mwl. kashindye akikubali je wananchi watakubali? tukumbuke kuwa hao wanaopiga kura kuteua haya majina si wananchi kwa wingi wao bali ni kakikundi ka watu wachache.
 
Hakuna unachokijua ni vema ukakaa kimya, na ninachokuomba uweke kumbukumbu zako vema kama Mwl. kashindye asipopitishwa uje tena hapa baada ya uchaguzi unlete majibu ya kitakachotokea na hapo ndipo tutajua mwenye mawazo finyu ni mimi au wewe.
Mkuu unahoja ya musingi sasa unaborongaborongo hoo mara kunambinu tupe hzo mbinu na nikinanani umewaona wapi au umewasikia wapi wakipanga hzo mbinu za Ku mchakachua mwalimu ndo maana nanuku hayo nimawazo yako na mtazamo wako vinyuuuu:thumbup::thumbdown:
 
Unalazimisha apitishwe? Acha demokrasia ichukue mkondo wake.
 
Amekijenga chama .....sawa tunakubali kama usemavyo......ila kama ameshiriki kura za maoni na akishindwa,kama mwanademokrasia hana budi kukubaliana na matokeo..........jaribu kujiuliza kama wote waliopigania vyama ndo wapewe nafasi za kiuongozi kisa tu walikijenga kungekuwa na migogoro mingi sana. Uongozi ni kupokezana sio kulipana fadhila........amekijenga chama akubaliane na mchakato wa kura za maoni wengine ( inawezekana wana uwezo kuliko uliemtanabaisha) wampokee wasukume gurudumu la mabadiliko
 
Wanachama ndio waamuzi wa mwisho, wal ndio watachagua wanayemtaka. Hayo maneno ya BILA MWL KASHINJE ni ya kwako, ajipange, akifanya mchezo wanachama watamuweka pembeni.
 
Amekijenga chama .....sawa tunakubali kama usemavyo......ila kama ameshiriki kura za maoni na akishindwa,kama mwanademokrasia hana budi kukubaliana na matokeo..........jaribu kujiuliza kama wote waliopigania vyama ndo wapewe nafasi za kiuongozi kisa tu walikijenga kungekuwa na migogoro mingi sana. Uongozi ni kupokezana sio kulipana fadhila........amekijenga chama akubaliane na mchakato wa kura za maoni wengine ( inawezekana wana uwezo kuliko uliemtanabaisha) wampokee wasukume gurudumu la mabadiliko

Ndugu mimi sipingani na hiki ulichokiandika lakini nimetoa angalizo kuwa wananchi ambao ndio wapiga kura hawata kuwa tayari kupigia kura mtu mwingine tofauti na Mwl. Kashindye kwani hao vijana hawajawahi kuonekana au kuwepo Igunga tofauti na kipindi hiki cha mchakato wa Ubunge kwani walijikita kuwa karibu na hao wajumbe wanaohusika na upigaji kura na kuwapa hicho walichokuja nacho sio wananchi hivyo CHADEMA itapoteza Ubunge ambao kwa kiasi kikubwa chama kilikuwa na nafasi kubwa ya kushinda.
 
Hakuna unachokijua ni vema ukakaa kimya, na ninachokuomba uweke kumbukumbu zako vema kama Mwl. kashindye asipopitishwa uje tena hapa baada ya uchaguzi unlete majibu ya kitakachotokea na hapo ndipo tutajua mwenye mawazo finyu ni mimi au wewe.
Ikiwa uliyoandika ni ya kweli basi inashangaza wasiwasi wako ni nini? Kwa mujibu wako Mwl kashindye ndiye kajenga chama wilayani, amesaidia kushinda uongozo wa serikali za mitaa. Hawa ndiyo wapiga kura wake kwenye kura za maoni...sasa kinachokusumbua ni nini mpaka ulete uzi hapa ukikata rufaa kwa viongozi makao makuu hata kabla kura hazijapigwa?
 
Wanachama ndio waamuzi wa mwisho, wal ndio watachagua wanayemtaka. Hayo maneno ya BILA MWL KASHINJE ni ya kwako, ajipange, akifanya mchezo wanachama watamuweka pembeni.

Mimi nafikiri nyie mnaotoa hii michango hampo kwenye uwanja wa mapambano, mnaandika kwa hisia tu ninakuhakikishia ingawa mimi sio muumini wa watu wanao hama hama vyama lakini CHADEMA wakifanya kosa na Mwl. Kashindye akahamia chama kingine na kugombea matokeo mtayaona na wapo watakaokumbuka hiki nilichokiandika.
 
Mimi nafikiri nyie mnaotoa hii michango hampo kwenye uwanja wa mapambano, mnaandika kwa hisia tu ninakuhakikishia ingawa mimi sio muumini wa watu wanao hama hama vyama lakini CHADEMA wakifanya kosa na Mwl. Kashindye akahamia chama kingine na kugombea matokeo mtayaona na wapo watakaokumbuka hiki nilichokiandika.

Kama anapendwa kweli kwa maelezo yako, then huna haja ya kuwa na wasiwasi. Nyie mpitisheni kura za maoni tu.
 
Ni bora ukasubiri kura kwanza......wasiwasi wako usije ukawa ni uchochezi hasa kwa kauli eti wanachadema hawatakuwa tayari kumpigia kura mtu mwingine tofauti na mwl Kashindye.....hii inamaanisha sio wasiwasi wako.......ni swala ambalo mmeshakaa vikao vyenu mkaamua hamtakua tayari kumpigia mtu tafauti na huyo mwl.............kama ni mawazo yako kama ulivyosema sikutarajia kuona na maoni ya wanachadema.........sema tu kuna kitu unajaribu kutuaminisha ila unashinshindwa kuweka wazi......mtoa posti pitia tena maneno yako then urudi
 
Kama anapendwa kweli kwa maelezo yako, then huna haja ya kuwa na wasiwasi. Nyie mpitisheni kura za maoni tu.

Ndugu kuna sentensi ipo kwenye maelezo yangu kama inavyojionyesha hapa chini, hii ina maelezo mengi lakini nimeiweka kwa ufupi sana.

''Kuna njama za makusudi zimepangwa na kuratibiwa na baadhi ya viongozi ili kuhakikisha Mwl.Kashindye apati nafasi ya kugombea Ubunge kwa awamu hii akiwemo na kiongozi mkubwa aliyejitanabaisha kuwa ana mapenzi na CHADEMA Igunga .''
 
Mimi nafikiri nyie mnaotoa hii michango hampo kwenye uwanja wa mapambano, mnaandika kwa hisia tu ninakuhakikishia ingawa mimi sio muumini wa watu wanao hama hama vyama lakini CHADEMA wakifanya kosa na Mwl. Kashindye akahamia chama kingine na kugombea matokeo mtayaona na wapo watakaokumbuka hiki nilichokiandika.

Muda Mrefu huyo kashindye wako alikua mfuasi wa zitto na ACT yake kwanza nashangaa kuniambia kuwa bado yupo CDM
 
kibogo

Kama haya yote uliyoyaandika ni ukweli mtupu basi nyinyi ndio mnaopiga kura bila shaka mtamchagua mgombea huyu, kinyume na hapo nitashindwa kuwatofautisha na ccm maajenti wa Lucifer.

Kwa haya uliyoyaeleza hapa kama ni kweli tupu msipompigia kura za ndio basi na nyinyi ni wala rushwa tu kama mijumbe ya ccm isiyokuwa na akili hata chembe.
 
Last edited by a moderator:
cdm mwaka huu kuna rushwa kali,geita mjini ilikuwa mikononi mwa cdm 99% baada ya kura za maoni sasa ni mali ya ccm 99.3%
 
Back
Top Bottom