IGP Mwema, 'mob justice' na kuuawa kwa polisi

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,308
mwema.jpg

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Said Mwema

"Salam, ….. naomba tafakari mob justice (kujichukulia sheria mikononi) ni adui wa human rights rule of law, (sheria za haki za binadamu). Good governance (Utawala bora) iwe kwa raia au askari aliyeuawa … ambaye niko njiani kwenda … kumzika. Na iwe sababu yoyote, hata Mungu hampendi anayetoa kikatili roho ya mtu mwingine…..Where are the good people? (Wako wapi watu wema?). Lets join hands and have ant mob justice campaign in this country for common good (Tushikamane kupinga wanaojichukulia sheria mikononi katika nchi kwa ajili ya ustawi)."

Huo ulikuwa ujumbe mfupi wa maneno kwa njia ya simu (SMS) kutoka kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Said Mwema, uliokuwa ukilalamikia kitendo cha baadhi ya wanakijiji wa Mwakashahala kata ya Puge, wilayani Nzega, Mkoa wa Tabora, kumuua polisi Joseph Milinga, Aprili 20, 2011 baada ya kuwakamata wakiwa na bangi.

Mwaka jana aliuawa polisi wa cheo cha chini. Mwaka huu ameuawa RPC. Mwaka kesho sujui atauawa polisi wa cheo gani. Kama RPC anauawa kilaini hivi ndani ya ardhi ya Tanzania basi hata usalama wa IGP Mwema ni wa mashaka sana maana "mob justice" is still at work.

UPDATE

Habari za kuaminika nilizopata hivi punde ni kwamba RPC Wa mkoa Wa mwanza KAMANDA BALO amekufa kwa kupigwa risasi. Habari zaidi zitaendelea!!

UPDATE

Askari polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia cha FFU ameuawa kwa kupigwa mapanga na kukatwa kichwa kufuatia vurugu zilizotokea visiwani Zanzibar jana mchana na kuendelea hadi leo. Mob justice still at work? (updated 18th October 2012)

UPDATE


VITENDO vya wananchi kujichukulia sheria mikononi vinaendelea kushika kasi ambapo askari wawili wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, wanadaiwa kuuwa na wananchi wenye hasira kali jana. Taarifa ambazo zililifikia Tanzania Daima Jumapili wakati tukielekea mitamboni jioni, zilisema kuwa mauaji hayo yalifanyika baada ya wananchi hao kuvamia na kukichoma moto kituo cha polisi cha Mugoma wilayani humo baada ya askari hao kudaiwa kumpiga risasi fundi wa pikipiki.

Kwa mujibu wa mashuhuda, tukio hilo lilitokea mchana wakati askari kadhaa wa kitengo cha usalama barabarani walipofika kwa fundi pikipiki huyo na kutaka kuichukua pikipiki aliyokuwa akiitengeneza kwa madai kuwa ilikuwa na makosa. Kwamba fundi huyo aligoma na kueleza kuwa asubiriwe mwenye pikipiki ili kuepuka kudaiwa chombo hicho cha usafiri.

Mmoja wa mashuhuda hao, aliyatambulika kwa jina moja la Libela, alidai kuwa baada ya mvutano wa muda mfupi, askari hao walifyatua risasi na kumpiga fundi huyo mguuni na kifuani, hivyo kusababisha kifo chake. Aliongeza kuwa, tukio hilo liliwapandisha hasira wananchi na kuwafukuza askari hao waliokimbilia katika kituo hicho cha polisi.

Lebela alifafanua kuwa, wananchi hao waliamua kukichoma moto kituo hicho hatua iliyosababisha askari waliokuwemo kutoka na kukimbia kila mmoja na muelekeo wake. Alisema kuwa askari aliyetajwa kwa jina la Koplo Paschal alianguka wakati akijinusuru, hivyo kuvamiwa na wananchi waliokuwa na zana mbalimbali za jadi ambazo walitumia kumshambulia na kumuua papo hapo.

Wananchi hao pia wanadaiwa kumfuata askari mwingine anayetajwa kwa jina la Pc Alex aliyekuwa amekimbilia kwenye nyumba ya mwananchi mmoja na kumtoa kwa nguvu na kisha kuanza kumshambulia hadi kumuua.

Tukio hilo limetokea ikiwa ni siku ya soko katika eneo hilo la Mugoma linalopakana na nchi jirani ya Burundi ambapo raia wa Tanzania na Burundi hukutana na kufanya biashara jirani na kituo hicho cha polisi.

Kutokana na kuchomwa moto kwa kituo hicho, nyaraka mbalimbali zinadaiwa kuteketea, huku pikipiki na baiskeli kadhaa zilizokuwa kituoni hapo nazo zikiteketea. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Philip Kalangi, hakuweza kupatikana kuthibitisha tukio hilo kutokana na simu yake ya kiganjani kuita bila kupokelewa.(updated 17th December 2012)

UPDATE


Wananchi wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma wamemuua askari polisi mmoja na kumjeruhi mwingine kwa kutumia silaha za jadi, baada ya askari hao waliokuwa doria kumuua kwa kumpiga risasi mwendesha pikipiki kwa kuvunja sheria za barabarani.

Source: RADIO ONE BREAKING NEWS

..polisi mmoja wa wa pikipiki na dereva wa bodaboda wauawa katika kijiji cha litola wilayani namtumbo.sababu ya mauaji inasemekana kuwa kulikuwa na polisi wawili wakiwa kwenye pikipiki wakawa wanamfukuza dereva wa bodaboda ambaye alikaidi kusimama,baada ya polisi kuona wameshindwa kumkamata dereva wa bodaboda wakaamua kumtandika risasi na kupelekea kifo cha dereva wa bodaboda.

wananchi kuona hivyo wakaungana kuwafukuza polisi.kuona hali nh tete polisi wa nyuma ambaye alikuwa amekamata bunduki akawa ameruka na bunduki akawa ameidondosha,raia mmoja akaioata akamtandika yule polisi aliyekuwa anaendesha pikipiki nae akauawa hapohapo na yule aliyeruka kwenye pikipiki ameumia vibaya sana na ametoweka inasadikiwa amejificha.mpaka sasa inasemekana bunduki haijulikani iliko gari mbili za polisi zimeelekea kwenye tukio moja likiwa limejaa polisi waliojikamilisha kwa mapambano na nyingine iko tupuinasemekana ni kwa ajili ya kubebea maiti.

wananchi wa namtumbo wanalalamikia sana utendaji kazi wa polisi,umekuwa ukiwanyanyasa sana madereva wa bodaboda,vijana wa kitanzania wanaojitafutia riziki zao.lawama zaidi ni kwa hawa polisi kuendekeza rushwa na kuwabambikia makosa ya uwongo na wananchi wamechoka.
 
"Salam, ….. naomba tafakari mob justice (kujichukulia sheria mikononi) ni adui wa human rights rule of law, (sheria za haki za binadamu). Good governance (Utawala bora) iwe kwa raia au askari aliyeuawa … ambaye niko njiani kwenda … kumzika. Na iwe sababu yoyote, hata Mungu hampendi anayetoa kikatili roho ya mtu mwingine…..Where are the good people? (Wako wapi watu wema?). Lets join hands and have ant mob justice campaign in this country for common good (Tushikamane kupinga wanaojichukulia sheria mikononi katika nchi kwa ajili ya ustawi).” And wht about killing of innocent tanzanian by police is dat da rule of law. Jee na polisi kutoa roho za kina daudi na ally jee mungu amependa when u talk good governance n rule of law u should stop ur men (police) to kill innocent pple
 
Apunguze kitambi kwanza.

aanzishe operation ONDOA vitambi kwenye jeshi la polisi
 
Tunasikitika sana kwa kifo cha Kamanda Barlow RIP kama tunavyosikitika kwa kifo cha Mwangosi RIP, askari na raia wengine ambao wameuawa ingawa katika mazingira tofauti tofauti.

Namshauri kwa nguvu zote IGP SMS na kukemea tu haitoshi, chukua hatua kwa wote wanaohusika na mauaji ya aina hii; awe polisi au raia. Anza na wote waliomuua Mwangosi na wote walioshiriki kuua raia kwenye maandamano kwa sababu wote wamechukua sheria mikononi mwao kuhukumu na kuua. Halafu wasakwe kwa hali na mali wote walioshiriki kukatisha maisha ya kamanda.

Na tafadhali tangaza hatua Kali kwa askali yeyote atakayeshiriki kuua raia au raia kuua raia katika mob justice.
Vinginevyo kukemea tu haitasaidia! Tabia imekwishajengeka kwa raia kuamini kuua katika mob justice ni sahii na polisi kuua raia ni sahihi! Tafadhali inspector hili liko katika uwezo wako
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mkuu EMT heshima mbele.

Mengi yanasemwa na mengi yatakuja lakini kumekuwa kukielezwa mambo mengi juu ya nidhamu na utendaji ulivyo mbovu ndani ya jeshi letu hili la polisi.

IGP Mwema ameshindwa kazi ya kuongoza jeshi hili na haya mambo yote yanayotokea sasa ni alama tosha kuonyesha kushindwa kwa IGP.

Mbali ya mamlaka ya raisi, IGP wetu hawezi kuhojiwa utendaji wa kazi zake iwe na meya wa jiji, mkuu wa mkoa au hata wananchi wenyewe, kwa hio anajiona kwamba yeye ni yeye na inakuwa ni vigumu kumfanya awe "accountable" pale madudu yanapofanywa na wale wa chini yake.

Sasa kujichukulia sheria mikononi au "mob justice" kunatokea pale wananchi wanapokosa pa kwenda katika kutatua tatizo la wezi wadogowadogo "petty thieves". Mwizi mdogo anapokamatwa kwa kosa la wizi anapelekwa kituo cha polisi na akiwa humo analala usiku mmoja na kesho yake anaonekana barabarani na anakwenda kuiba tena.

Hali hii ya kufanya kosa lilelile na hasira ya wananchi juu ya jeshi letu kwamba haliwajali, kupiga wananchi pale kunapotokea kutuliza ghasia au vurugu, kulazimisha utoaji rushwa na vitisho vya kuswekwa rumande endapo hutatoa rushwa, kuanza kukiuka miiko ya jeshi na kuanza hata kuishi hovyo uraiani kumeshusha hadhi ya jeshi hili na matokeo yake ndio unayaona haya ya leo ya IGP kushindwa kwenye "decision making process" kwamba "mechanism" yote imevunjika kwenye kutumia utaratibu na mbinu ili kutoa maamuzi sahihi na yenye ubora.

IGP ni cheo kikubwa na chenye kubeba dhamana ya kuongoza askari polisi kwenye kulinda usalama wa raia na mali zao.

IGP Mwema ameshindwa kutoa maamuzi sahihi na bora yenye lengo la kuboresha jeshi hili na kulifanya lijijengee heshima mbele ya jamii. Ntatoa mfano wa moja ya maamuzi yake kwenye eneo la kukabiliana na ujambazi alipokuja na sera ya" shoot to kill".

Hii sera ya "shoot to kill" ndio ime-backfire na tumempoteza kamanda wa polisi wa Mwanza na hata hiyo ya hao wanakijiji waliomuua Milinga waliona hawana njia.

Mtu unapotoa sera ambazo zinahusiana moja kwa moja na jamii inabidi uzingatie vitu vitatu muhimu, uwazi kwamba maamuzi na uendeshaji wa operesheni zote ziwekwe wazi na wananchi wafahamu kinachoendelea.

Pili, sera hizi zionekane zinafanya kazi yaani "effective" na kuonekane matunda yake, lakini bila kukamata majambazi, kuyatesa na hata kuyaua bila kuyafikisha mahakamani kuona sheria inavyochukua mkondo wake.

Tatu, ni sera hizo zionekane ni hazina upendeleo yaani "fairness". huwezi kusema unatoa sera ya shoot to kill wakati hujawasiliana na wadau mbalimbali kwenye jamii inayokuzunguka halafu utegemee matokeo mazuri ya sera hizo.

Kwahio kifo cha RPC wa Mwanza na Milinga ni matokeo ya polisi kutokuwa na mawasiliano mazuri na raia wake, kutumia nguvu kupita kiasi (hasa FFU), kukiuka maadili ya kijeshi kwa kuwa na mahusiano ya karibu mno na wananchi ambako kumetokana na kuishi uraiani, na mwisho ni polisi wenyewe kujishirikisha na vitendo vya UFISADI vikiwemo magendo na upokeaji milungula.

Hii topic ni kubwa sana na inahitaji michango minene zaidi na hata IGP mwenyewe akisoma aone kama anaweza kujiuzulu mara moja bila kungoja aambiwe.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mkuu Richard nakubali yote uliyoandika. Kuhusu kukiuka kwa maadili ya kijeshi kwa kunatokana na kuwa na mahusiano ya karibu mno na wananchi ambako kumetokana na kuishi uraiani, ni kweli, askari wanaopanga nyumba uraiani wanaweza kujiingiza katika vitendo vya kihalifu au kuwalinda wahalifu kutokana na kuishi nao na kujenga urafiki. Kuna mdau kule Wanabidii alifafanua hili kwa undani zaidi.

"Mkoloni hakuwa mjinga kutenga makazi ya maofisa wa serikali na kuyaweka Keko maeneo ya Mgulani. Eneo kubwa lote Keko matangini, chang'ombe, Kurazini quarters za polisi na yakaja makambi ya JKT baadae, maghorofa ya police na vyuo vyao. Kila mji na wilaya/zone ina nyumba za police-magomeni, Ilalla etc. Makahimu na viongozi huko Oysterbay, Upanga etc ambako baadae nyumba hizo zimeuzwa watu wanaporomosha maghorofa wanapangisha kwa $.

Kwa ufanisi kazini, kutenga makazi ya Jeshi, police, Magistrate/Lawyers wa serikali ni muhimu kwa ufanisi na ulinzi. Hata Walimu walikuwa na nyumba zao za GVT. Ujamaa umetufanya tuone huu ni utengano, polisi na raia budi wawe marafiki tuchanganyike. Uwezo mdogo wa GVt na ukuzi wa sekta mbali mbali umefanya polisi wakae Uraiani.

Imagine-kipato na ukubwa wa familia yake na anapanga vyumba visivyomtosheleza uraiani, anakosa hata hela ya kulipa kodi, anamkopa mwenye nyumba miezi. Anaadhirika. Atakuwa na ufanisi huyu? Anacheza bao mtaani na hao waharifu au ni watoto mwenyenyumba yake ambaye hajamlipa kodi, kamkopa hela au chakula dukani kwake. Na kama ni hakimu kapanga upande au vyumba au nyumba-ufanisi hupo hapo na mbakaji ni mtoto wa baba mwenye nyumba au jirani etc?

Ije hii ya police au JWTZ kuhusika na kuzuia vurugu ambapo mmojawapo au baadhi wameuawa. Jee, huyu mtu-police akaae uraianihana ulizi, kapanga ndani ya nyumba au kajenga huko anaishi kwake akihusika au kutohusika ktk mabomu ya machozi atakuwa salama? Watu watatumia excuse yoyote hiyo ya chuki zao ktk masuala ya kisiasa au ya jamii ya kuthibiti uhalifu au kukamata wahalifu mtaani na kumtolea yeye au familia yake kisasi. Kuna haja ya kufikiria upya kuhusu watu/watumishi wa vyombo vya sheria kukaa uraiani vichochoroni bila ulinzi au kuishi wao kiholela."

https://groups.google.com/forum/?fromgroups=#!topic/wanabidii/wWxw3BLiOE8
 
Last edited by a moderator:
Hivi ni nani mwenye haki ya kuua?. Kamanda Kamuhada kasema alichokifanya Iringa ni kutekeleza amri za wakubwa. Na je, waliomuua RPC. Barlow wakijitokeza na kusema walikuwa wanatekeleza amri ya mume wa mwalimu watashtakiwa?
Nauliza tu!!
 
Hivi ni nani mwenye haki ya kuua?. Kamanda Kamuhada kasema alichokifanya Iringa ni kutekeleza amri za wakubwa. Na je, waliomuua RPC. Barlow wakijitokeza na kusema walikuwa wanatekeleza amri ya mume wa mwalimu watashtakiwa?
Nauliza tu!!

Hakuna mwenye haki ya kuua awe mkubwa au mdogo.
 
Jeshi la polisi liache kuchanganya usalama wa raia na siasa, vinginevyo ...................................watu wema wataendelea kukatishwa maisha yao kwa uzembe wao. Let them concentrate on their job
 
Jeshi la polisi liache kuchanganya usalama wa raia na siasa, vinginevyo ...................................watu wema wataendelea kukatishwa maisha yao kwa uzembe wao. Let them concentrate on their job
Nilwahi kusema hapa JF kwamba Tanzania tunahitaji police reforms . Kama kuna Waziri, Dhaifu ,Mbunge na hata IGP Said Mwema and all police brass wanajua ninachosema . Mfumo wa Police ulioopo kwa sasa hauendani na uhalisia. The police force require massive modernization to cope with the developments. You can not understand how a top Regional Cop could be so insensitive with his own security. Driving in the depth of the night without backup or tracking is negligence of the highest degree. Where is the police intelligence .i don't meen that Lyimo deserved to die but he was in a better position to understand the insecurity in this country. Unapita kwenye Bank you find an FFU cop standing with a machine gun without protective gear and you think this guy is out of his mind . When you give them amuniition then provide them with the right gear,. Holding a sub gun you become a soft target of who ever chooses to attack you. Hivi Barlow (Marehemu) alishindwa vipi kutanguliza vijana wa patrol where he wanted to go in the night? Huyo Mama Kama alikuwa Shemeji yake au kabustani 02:00 is not the right time for a top cop to be on motion??
 
EMT Hakuna jeshi nchi hii..mbwembwe tu Yaani RPC anauwawa kama bata
 
Last edited by a moderator:
mwema.jpg

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Said Mwema

"Salam, ….. naomba tafakari mob justice (kujichukulia sheria mikononi) ni adui wa human rights rule of law, (sheria za haki za binadamu). Good governance (Utawala bora) iwe kwa raia au askari aliyeuawa … ambaye niko njiani kwenda … kumzika. Na iwe sababu yoyote, hata Mungu hampendi anayetoa kikatili roho ya mtu mwingine…..Where are the good people? (Wako wapi watu wema?). Lets join hands and have ant mob justice campaign in this country for common good (Tushikamane kupinga wanaojichukulia sheria mikononi katika nchi kwa ajili ya ustawi).”

Huo uliliwa ujumbe mfupi wa maneno kwa njia ya simu (SMS) kutoka kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Said Mwema, uliokuwa ukilalamikia kitendo cha baadhi ya wanakijiji wa Mwakashahala kata ya Puge, wilayani Nzega, Mkoa wa Tabora, kumuua polisi Joseph Milinga, Aprili 20, 2011 baada ya kuwakamata wakiwa na bangi.

Mwaka jana aliuawa polisi wa cheo cha chini. Mwaka huu ameuawa RPC. Mwaka kesho sujui atauawa polisi wa cheo gani. Kama RPC anauawa kilaini hivi ndani ya ardhi ya Tanzania basi hata usalama wa IGP Mwema ni wa mashaka sana maana "mob justice" is still at work.

“In a time of deceit telling the truth is a revolutionary act.”
― George Orwell
 
"Salam, ….. naomba tafakari mob justice (kujichukulia sheria mikononi) ni adui wa human rights rule of law, (sheria za haki za binadamu). Good governance (Utawala bora) iwe kwa raia au askari aliyeuawa … ambaye niko njiani kwenda … kumzika. Na iwe sababu yoyote, hata Mungu hampendi anayetoa kikatili roho ya mtu mwingine…..Where are the good people? (Wako wapi watu wema?). Lets join hands and have ant mob justice campaign in this country for common good (Tushikamane kupinga wanaojichukulia sheria mikononi katika nchi kwa ajili ya ustawi).” And wht about killing of innocent tanzanian by police is dat da rule of law. Jee na polisi kutoa roho za kina daudi na ally jee mungu amependa when u talk good governance n rule of law u should stop ur men (police) to kill innocent pple
umesema vyema mkuu! kwa sababu kila binadamu ana haki ya kuishi. Kifo kiwe kutoka polisi au mob ni kifo tu!! Tutafakari wote hivi! polisi wanapoua sehemu mbalimbali Arusha, Mwanza, Iringa na kwingineko na kuficha ushahidi kwa njia za kijinga kama yule kichaa wa Kova wanategemea nini? Je watu watakaa kimya tu? Je wenye ndugu zao wanaouawa na ushahidi kufichwa na kuzuiwa wakae kimya hadi lini!? Jeshi la polisi na vyombo vya utawala bora vibadili mfumo mbaya ama sivyo mob justice ni matokeo tu ya utendaji wao mbaya! kwa mfano kama ninajua polisi akinichukulia mke nikilalamika anaweza kuniua na hakuna kesi nifanye nini? mimi ni binadamu mwenye hisia!!
Sitetei mob justice ila ninasema mob justice ni matokeo ya ukosefu wa justice! Hata wale suicide commandos wa palestina na afghanistan wamefikishwa hapo kwa kukosewa haki kwa kiwango cha juu!! Hivyo serikali ichukue hatua mapema na siyo kufanya msako wa kuwawinda waliomuua Barlow tu bali kurekebisha utendaji wa vyombo vya kutoa haki. Juzi tulipata huko huko Mwanza Afisa uhamiaji anaponea kifo cha risasi za polisi kwenye tundu la sindano. Hatua zichukuliwe si utani.
 
police tendeni haki kwanza ndo mkemee mob justice ... mengine yanasababishwa na utendaji wenu!!
 
Haya taarifa za polisi mwingine kuuawa huko Zanzibar.

Askari polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia cha FFU ameuawa kwa kupigwa mapanga na kukatwa kichwa kufuatia vurugu zilizotokea visiwani humo jana mchana na kuendelea hadi leo. Mob justice?
 
Muslims are not happy in Gaza.
They’re not happy in Egypt or Libya
or Morocco.
They’re not happy in Iran.
They’re not happy in Iraq or Yemen
or Afghanistan.
They’re not happy in Pakistan.
And they’re not happy in Syria or
Lebanon.
So, where are they happy?
They’re happy in Australia.
They’re happy in Canada.
They’re happy in England, France
and Italy.
They’re happy in Germany. They’re
happy in Sweden, the USA and
Norway.
They’re happy in Holland and
Denmark.
Basically, they’re happy in every
country that is not Muslim and
unhappy in every country that is.
And who do they blame?
Not Islam. Not their leadership. Not
themselves.
They blame the countries they are
happy in.
And then they want to change those
countries to be like the country they
came from where they were
unhappy.
 
Back
Top Bottom