IGP - Mtandao huu ni hatari - Part I

Kama unafahamu haki zako huwezi lalamika, namba ya simu ya huyo IGP ipo mpigie mweleze na ushahidi uwe nao
Utakaporudi na hiyo part 2 uje na majina ya hao wahalifu pamoja na hao makamanda

Namba zao wanatoa kwa gelesha tu hawa utekelezaji hamna
 
Mkuu mimi sijajua kama hilo genge lipo ila jana nikeona gari limewekwa stika ya neno free marson nikashangaa ila nilivyochungulia kwa ndani nikamuona ni kijana tu. IGP inabidi alifanyie kazi aisee polisi imeshakuwa corrupted

Corruption waanza kupewa hao police wa juu hawa kajamba nani huku chini wanaishia kuonywa kumfuatilia mtu tu
 
nafikiria kununua bunduki yangu. Hii nchi hivi sasa magumu yoyote yakikukuta unatakiwa kuyakabili mwenyewe tu. Utawala wa sheria ulishafutwa hapa nchini. Unaweza usiwe na kosa ukafungwa maisha. Bora tu uwe na bunduki yako, wakikuvamia unawawasha risasi halafu unakwenda gerezani mwenyewe bila kungoja kuitwa.
 
Wakati Mwakyembe linamkuta ulisema haikuhusu na hata sasa watanzania tutasema haituhusu, hivi kwanini isifike mahali tuwe wazalendo? Tukubaliane nini cha kufanya.
Kwani kinachowashinda kubeba mawe, mikuki na mapanga na kuingia mitaani kumtaka kikwete ang'oke ni nini? Maana Kikwete is a completely failed leader. Ukishakuwa na rais mbovu kama Kikwete usitegemee kwamba kutakuwa na utendaji mzuri huku chini. Mapambano yaanze dhidi ya Kikwete kwanza kabla hatujawakataa wahuni wengine wengi.
 
kama kweli upo police jamii fatilia eneo lililotajwa na ndohela kuliko kumtaka aje hapo uliposema, kwa sababu za kiusalama. Simshauri ndohela aonane na wewe. Unanipa mashaka, au nawe ni kati yao?

kama anapatikana makumbusho siyo polisi, ni usalama wa taifa huyo
 
mmesahau yule mama wa kule mbezi beach jina lake nimesahau aliporwa kiwanja na papaa musofe na alipokwenda kanda maalum ya kinondon kwa charles kenyela akupata ushirikiano wowote mpaka bibi ananilea ndio akaokoa jahazi adi kwa pinda ??!!
 
Kuushitaki mtandao huo kwa IGP ni sawa na kesi ya Ngedere kumpelekea Nyani, kwani ukiisoma vizuri taarifa ya Mwakyembe ile inayokanusha maelezo ya DCI hapo utapata picha halisi iliyojificha ndani ya jeshi letu la POLISI, hebu angalia huyo IGP alivyosigina sheria na uadilifu kazini.......


, alisemasiku chache baada ya kumkabidhi IGP Mwema barua hiyo, alitumiwa timu yawapelelezi ofisini kwake ili kuchukua maelezo yake ya ziada. Alifafanuakuwa timu hiyo ilikuwa inaongozwa na Ofisa wa polisi ambaye wiki chachezilizopita alikuwa miongoni mwa askari waliotuhumiwa kupokea rushwa kwa lengola kumbambikizia dawa za kulevya mtoto wa mmoja wa wafanyabiashara maarufunchini, suala alilodai kuwa mpaka sasa uongozi wa Polisi umeshindwa kulitoleamaelezo ya kuridhisha.
Alisema kwa msingi huo,aliona ameletewa mtuhumiwa wa rushwa na ujambazi kuendesha uchunguzi wawatuhumiwa wengine wa ujambazi jambo ambalo haliwezekani na kwamba suala lakelimefanyiwa mzaha. Mwakyembe alisema wiki chache baada ya barua yakekuwasilishwa kwa IGP na timu ya polisi kuanza kazi, Jeshi hilo likachukua hatuaya kuwapongeza na kuwazawadia askari aliowatuhumu kushirikiana namajambazi. "Huhitaji kuwa profesa wa falsafa kuelewa kuwa huo ulikuwaujumbe tosha wa kunipuuza,"ilibainisha taarifa hiyo.
Alisema tuhuma za askari polisikujihusisha na vitendo vya ujambazi mkoani Morogoro zilipopamba moto nakuwagusa askari, wale aliowatuhumu kwenye barua yake, walihamishiwa mikoamingine. Mwakyembea alisema ili kumkatisha tamaa kabisa, barua yake ya ‘siri'kwa IGP ikavujishwa kwa makusudi kwenye vyombo vya habari na kuchapishwa kamahabari iliyokebehi na kukanusha taarifa nzima aliyoitoa "Sijui kwafaida ya nani," alihoji katika taarifa hiyo na kuongeza, " Lakini huu ni mchezowa kawaida kwa Jeshi la Polisi. Akitoa mfano wa Waziri Sitta, kuwa hivikaribuni, kiongozi huyo alihojiwa na ofisa mwandamizi wa Jeshi la Polisiofisini kwake, wakiwa wawili tu, lakini taarifa ya mahojiano ikaonekana kwenye moja ya magazeti, ikikebehi ushahidi aliotoa Sitta nakubainisha kuwa

Akamalizia kwa kusema.......

uadilifu wauongozi wa Jeshi la Polisi, umefikia pabaya.


JE HAPO BADO MNASEMA TUNA POLISI WA WANAINCHI WA TANZANIA?
 
kwa hii serikali yetu mimi naona kupeleka haya mashtaka polisi ni kupoteza muda-maaana hawafaitilii kabsa-naweza sema hizi taarifa wanazo na hawatazitendea kazi.kilichobaki ni kupinda sheria na kujitetea mwenyewe as an individual,kama unabunduki,kuwa sniper,umalize wale wote wanajihusisha na uonevu kama huu na kjutumiam pesa/vyeo vyao vibaya
 
Habari hii ni kweli kabisa. Wiki tatu nyuma walivamia kiwanja Mbezi beach maeneo ya Five Star na kuzungusha ukuta na kuleta walinzi. Nina habari mwenye kiwanja hakupata ushirikiano kabisa na polisi ya Wazo zilipo ofisi za OCD hivyo kwa msaada wa ofisi ya mwanasheria wake waliweza kupata amri ya kusimamisha ujenzi iliyotolewa na mahakama ya Ardhi na kesi itaanza karibuni. Katika uvamizi huo walitumia risasi za moto kumtisha the legal owner na majirani na hata baada ya ku report polisi hawakuchukua hatua yeyote. Habari ni kuwa tapeli mmoja papaa mfadhili wa bendi ndie kiongozi wa kundi lakini anawatumia wasaidizi wake kuongoza uhalifu huu kwa kuwa ameshaonywa karibuni na baadhi ya viongozi wa Polisi na hajatii alichoonywa. Naomba ifahamike kabisa hutapata msaada polisi hawa jamaa wakivamia kiwanja chako na hii ni kwa sababu ya wanalindwa na baadhi ya viongozi wa polisi. Nadhani huu ni uonevu uliokithiri na swala hili lingefuatiliwa na usalama wa Taifa kwani linakua kwa kasi. Nawakilisha wakuu
hapo kwenye red siku hizi ni wambea wa taifa hakuna kitu
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom