IGP - Mtandao huu ni hatari - Part I

IGP - Mtandao huu ni hatari - Part I

We Know Next

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2010
Posts
815
Reaction score
382
Mheshimiwa Kamanda Mwema - IGP,

Nadhani utakuwa na taarifa na kama huna taarifa basi tunaomba uanze kuifanyia kazi taarifa hii:

Kuna Genge moja la Kitapeli ambalo limezuka hapa jijini na kufanya utapeli wa kuvamia viwanja vya watu na kujifanya ni vya kwao. Genge hili linafanya kazi zake zaidi maeneo ya Kawe, Mbezi Beach, Tegeta, Boko mpaka Bunju. Genge hili la matapeli wanatembea na Magari yameandikwa Free Mansos, na wanatembea na silaha ( Bastola) vibindoni mwao na inasemekana wanapesa nyingi sana, ambazo ni pesa chafu. Wamekuwa wakifanya utapeli na usumbufu huo kwa baadhi ya watu wenye viwanja vyao ktk maeneo husika.

Kwa nini basi ni mtandao hatari?

Genge hili limejiimarisha sehemu zote muhimu ambazo linaweza kufanikisha kufanya mambo yao kwa urahisi, maeneo hayo ni katika Jeshi lako la Polisi, ofisi za manispaa, mahakama za ardhi, Wizara ya Ardhi na Makapuni binafsi ya ulinzi.

1. Jeshi la Polisi - Kuna baadhi ya polisi wanashirikiana na genge hili katika kuwadhurumu watu haki zao za msingi, tena kuna wengine ni maafisa wa juu kabisa ktk jeshi hili la Polisi. Maafisa hao wamekuwa wakikataa kutoa msaada kwa waathirika kwa misingi kuwa, migogoro ya ardhi Polisi haihusiki, ni wizara ya ardhi pekee. Hata mtu akienda kuripoti kuwa kuna wavamizi, wamevamia kiwanja, wamevunja nyumba, na wamekuja na silaha, bado polisi hao wanakataa kutoa msaada kwa walalamikaji. Badala yake, Polisi hao hao, wanakushauri kuwa la kufanya na wewe anza kubomoa kila anachokifanya huyo mvamizi. Kamanda, Tanzania tumefika hapo kweli? Yaani kimbilio la walalahoi limekuwashubiri? Unataka watu wachukue sheria mikononi? Maafisa hao wachache wasiokuwa na utu wala kufahamu kazi yao, wananunuliwa na pesa za hongo kutoka ktk genge hilo na kuwafanya kuwa nao ni wanamtandao, yaani polisi wanamsaidia mharifu? Je ni maadili ya kazi hakuna? Au ni sababu ya mishahara midogo? Kitakachokuja tokea Kamanda, watu wanaanza kukosa imani na Jeshi lako, na hata kuanza kujenga uadui na polisi, sababu tu, ya hao maafisa wachache wa polisi. Itafika kimbindi watatengwa kutokana na mambo haya. Genge hilo, limejijenga ndani ya polisi kwa ajili ya kupata usalama wao, kwani wanajua kabisa, wakifanya uvamizi huo, watu watakimbilia polisi kutoa taarifa, kwahiyo polisi hawata respond kwa haraka kama inavyotakiwa.

Maswali yangu ni haya kamanda,

i. Wananchi waende wapi ikiwa kama kimbilio lao, yaani polisi wakati wa matatizo ya uhalifu na ya jinai kuna kuwa hakuna msaada?

ii. Ikiwa kama maafisa hawa wataendelea kununuliwa na kuwa wanamtandao wa kiuhalifu, je unajenga jeshi la namna gani?

iii. Hivi wananchi wakipoteza imani na polisi tutakuwa salama kweli?

iv. Ni Kwanini maafisa wachache wa polisi waharibu sifa ya jeshi lako lote?

v. Nilisema mwanzo kuwa, unaweza kuwa umelisikia kundi hili au hapana, lakini je jibu lake au suluhisho lake ni nini kwa lolote kati ya uelewa au kutoelewa kuwepo kwa Genge hilo?

Nafahamu, kunaweza kuwa na wanajamvi wengine ambao wamesha lisikia au kukutana na mambo ya Genge hili, labda wanaweza kuongezea kwa hapa nilipoishia....! Kamanda, Mtandao huu ni hatari, chukua hatua.. PART II itaendela na maeneo mengine..

 
mkuu yaani mimi nilishapoteza imani na maaskari kitambo sana na tena nikishuhudia kapigwa risasi na mwangalia mpaka anakufa kama walivyomfanyia rafiki yangu inauma sana..

RIP Eddy Clux..
 
Kama unafahamu haki zako huwezi lalamika, namba ya simu ya huyo IGP ipo mpigie mweleze na ushahidi uwe nao
Utakaporudi na hiyo part 2 uje na majina ya hao wahalifu pamoja na hao makamanda
 
hizi zote ni ishara za a confirmed failed system.... umafia, neglience without accountability, a corrupt force, total control by a few hooligans (who in most cases are not even as reach as they portray) calling all teh shots
 
Kama unafahamu haki zako huwezi lalamika, namba ya simu ya huyo IGP ipo mpigie mweleze na ushahidi uwe nao
Utakaporudi na hiyo part 2 uje na majina ya hao wahalifu pamoja na hao makamanda
naomba unisamehe, let me call you mpuuzi, yani ni bora kupuuzwa, waliofanya hivyo either hawapo tena au kama wapo, basi hawatafanya tena hiyo jitihada

ukiona mtu kaleta hapa kwa namna hiyo ujue hizo jitihada nyingine ameshafanya
 
We unafikiri bila kupora viwanja vya watu hao mapeneshee watapata wapi pesa za kutunza wanamuziki wa dansi na wakina falii ipupa..
 
Nchi hii huu ujanja ujanja hatufiki popote. Tunajitengenezea mabalaa tu
 
Badala ya kuwa watendaji wamekuwa wanasiasa tangu intelijensia...ilipo fail IGP amepoteza umaarufu!!!
 
Mkuu mimi sijajua kama hilo genge lipo ila jana nikeona gari limewekwa stika ya neno free marson nikashangaa ila nilivyochungulia kwa ndani nikamuona ni kijana tu. IGP inabidi alifanyie kazi aisee polisi imeshakuwa corrupted
 
Aisee! hii ni hatari sana.... IGP chukua hatua dhidi ya suala hili la sivyo litaumiza wengi.
 
Kama unafahamu haki zako huwezi lalamika, namba ya simu ya huyo IGP ipo mpigie mweleze na ushahidi uwe nao
Utakaporudi na hiyo part 2 uje na majina ya hao wahalifu pamoja na hao makamanda

kiukweli pasipo na majina ya wahusika inakuwa ngumu kuitofautisha na hadithi za erick..
 
Makamanda wa polisi wawe wanachaguliwa na wananchi....

Mkubwa hili ingekuwa bomba kweli kweli!
Na hata RC angetakiwa achaguliwe na wanainchi na siyo kuteuliwa kijinga kama inavyofanya chama cha majambazi

Sina budi kusema kwamba hata hili genge hawako mbali na hii chama kijani.

Tuwe wapole kidogo kwani tutasikia mengi sana kuhusu hili.
 
Habari hii ni kweli kabisa. Wiki tatu nyuma walivamia kiwanja Mbezi beach maeneo ya Five Star na kuzungusha ukuta na kuleta walinzi. Nina habari mwenye kiwanja hakupata ushirikiano kabisa na polisi ya Wazo zilipo ofisi za OCD hivyo kwa msaada wa ofisi ya mwanasheria wake waliweza kupata amri ya kusimamisha ujenzi iliyotolewa na mahakama ya Ardhi na kesi itaanza karibuni. Katika uvamizi huo walitumia risasi za moto kumtisha the legal owner na majirani na hata baada ya ku report polisi hawakuchukua hatua yeyote. Habari ni kuwa tapeli mmoja papaa mfadhili wa bendi ndie kiongozi wa kundi lakini anawatumia wasaidizi wake kuongoza uhalifu huu kwa kuwa ameshaonywa karibuni na baadhi ya viongozi wa Polisi na hajatii alichoonywa. Naomba ifahamike kabisa hutapata msaada polisi hawa jamaa wakivamia kiwanja chako na hii ni kwa sababu ya wanalindwa na baadhi ya viongozi wa polisi. Nadhani huu ni uonevu uliokithiri na swala hili lingefuatiliwa na usalama wa Taifa kwani linakua kwa kasi. Nawakilisha wakuu
 
Pole sana mdau!Naamini kilio chako kimewafikia walengwa tusubirie matokeo!
 
sinauhakika na mtoa mada nikupe simu ya igp said mwema au ya dci manumba mimi mwenyewe nipo kwenye system kama nikweli na ushahidi unao mimi naweza kusaidia
 
sinauhakika na mtoa mada nikupe simu ya igp said mwema au ya dci manumba mimi mwenyewe nipo kwenye system kama nikweli na ushahidi unao mimi naweza kusaidia

Upo kwenye system ipi?
 
ndoleha Unaweza kukutana na mimi kesho njoo makumbusho unipe data naweza kufanyia kazi kama kweli unayoyasema na ushahidi unao sitaki mambo ya udaku au umepata viroba
 
Back
Top Bottom