Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 40,949
- 74,431
Mkuu wasikupe shida hao vibaraka. Kama huyo Mangu na hao vijana wake wangekuwa na unavu kama wanavyojinadi wangeangua kilio kule Tarime baada ya kutembezewa kichapo na vijana wa Mwamunyange? Kama hujaipata hiyo story ni kuwa kama kawaida yao walimkamata mjeshi akiwa anaendesha pikipiki bila helmet na amevaa kiraia. Basi kama kawaida yao wakamsumbua wakitaka hela ya "mboga" Sii unajuwa wanavyoendekeza njaa? Mjeshi akagoma na ngumi zikaanza.Angejua kazi majambazi yangemshinda, kazi anayojua ni kutii maagizo ya mabwana zake tu kuwadhibiti watetezi wa wanyonge. Siku ipo na siku yaja ambayo wauaji wote kuanzia fastjet mpaka mangu watajibu.
Basi bwana hao vijana wa Mangu sii wakaitana ili wamsulubu huyo mjeshi kama walivyowapiga wale wanawake walioandamana leo. Mjeshi akaona Polisi wamekuwa wengi na hawezi kuwamudu. Akaruka hewani kuwaita wenzake waje stand ya Tarime kuokoa jahazi. Kilichofuata hapo ni kuwa hao wanaosifiwa hapa walikula kichapo kama watoto wakaishia kuangua kilio hadharani mchana kweupe na wengine kupelekwa hospital kwa huduma ya kwanza.
Kwa hiyo hao wanaoitwa mashujaa kwa kupiga wanawake na raia wasio hata na manati kumbe si lolote wala chochote wanapokutana na wanaume wenzao wa kazi. Kumbe hata waandamanaji ni kwa vile wanaheshimu sheria tuu, lakini siku kikiwaka na kuamua jino kwa jino yatatokea yale ya Pemba ya kutenganisha kichwa na kiwiliwili.