IGP Mangu: Hatuonei vyama vya upinzani

IGP Mangu: Hatuonei vyama vya upinzani

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
27,624
Reaction score
62,458
Mangu-05Feb2015.jpg

Wakati vyama vya siasa vikiendelea kupiga jaramba kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Ernest Mangu, amesema jeshi hilo limejipanga kuhakikisha uchaguzi huo unafanyika kwa amani na halipo kwa ajili kukikumbatia chama chochote cha siasa.


Akizungumza katika mahojiano maalum na NIPASHE juzi, alisema tafsiri iliyoanza kujengwa na baadhi ya wanasiasa kwamba jeshi lipo kwa ajili ya kukikumbatia chama tawala siyo sahihi.

"Polisi akifanya vizuri atahojiwa tu asipofanya vizuri atalalamikiwa tu, kimsingi sisi tupo kwa ajili ya kuhakikisha amani inakuwepo, Jeshi la polisi halipo kwa ajili ya kudhibiti vyama vya upinzani," alisema.

IGP Mangu alisema Jeshi la polisi halipo kwa ajili kudhibiti wapinzani kwa kuwa mikoani vyama vya upinzani vimekuwa vikifanya mikutano mingi kuliko Chama Cha Mapinduzi (CCM) lakini havidhibitiwi vinapofuata taratibu na sheria zilizopo.

"Huko kwingine ambako wapinzani wanafanya shughuli za kisiasa hakuna polisi kiasi kwamba hawawadhibiti tuje tuwadhibiti hapa Dar es Salaam, siyo hoja ya msingi yaani tukio moja la kuzuia maandamano ya CUF ndilo linachukuliwa tunadhibiti wapinzani," alihoji na kuongeza kuwa: "Nenda katika kila mkoa uliza mikutano ya kisiasa iliyofanyika kwa mfano mwaka uliopita baina ya vyama vya upinzani na chama tawala utakuta wapinzani wanafanya mikutano mingi sana kuliko CCM.

IGP Mangu alisema kama kungekuwa na huo udhibiti wapinzani wasingeweza kufanya mikutano mingi na kwamba mikutano ya chama tawala imekuwa ikizuwiliwa lakini hilo halisemwi.

Kuhusu madai kwamba Jeshi la Polisi linatumia nguvu kubwa kudhibiti wapinzani, alisema tafsiri ya nguvu kubwa ni pana na inategemea anayezungumza ana maana gani.

"Tunaangalia uhalali wa jambo, kama tunaona jambo linaweza kuleta athari za kiusalama tunazuia kwani yakitokea ya kutokea tutakuja kuulizwa tulikuwa wapi hadi yakatokea," alisema.

Kwa muda mrefu sasa vyama vya upinzani vimekuwa vikilitupia lawama Jeshi la Polisi kwamba linatumika na chama tawala kudhoofisha nguvu ya vyama hivyo.


Chanzo:Nipashe
 
Huyu akae kimya tu hana la maana analoongea hapa
 
Ni mteule wa nani? Atamtumikia asiyemwajiri wake?
Think big
 
Kiukweli nilikuwa na imani kubwa na homeboy Mangu. Sijui nini kimetokea.
Hilo tukio moja la CUF limemharibia sifa zooote.
Watu wanapanda gari kwa kipigo,dada anapigwa virungu kifuani!
Kulikuwa na haja gani yakutumia wheelspana?
Mnyampaa kama uliteleza rudi kwenye weledi wako.
Au vinginevyo unataka tukuhurumie eti kuna maofisa wenzio wanakuhujumu?
 
Tangu nianze kulifahamu jeshi la polisi sijawahi kusikia wamekosea wakakubali kosa.
 
Yeye akaendelee kununua cement za dili toka kiwandani wazo......atutaki kusema mengi juu Yake ila ukweli ni kwanza wanakandamiza wapinzani.
 
Ni hili la juzi tu la kova kuandaa maandamano ya uvccm ofisini kwake na hapo hapo kuyapiga marufuku akiwa ofisini kwake hapo hapo ndiyo anajitafsiria kuwa kuna fair ground?asitudanganye huyu,kwanza cuf wenyewe walipigwa wakiwa katika harati za kutimiza agizo la polisi kwa kuwatawanya wafuasi wao waliokuwa uwanjani,kwa hiyo hakukuwa na maandamano wala mkutano uliokuwa ukiendelea siku hiyo.
 
watu wameshakalishwa kwenye magari na wengine wanapanda gari bado polisi wanawapiga magongo na kule polisi tumeona kwe TV wamepigishwa kichura, ni sawa kabisa alivyosema Pinda mtoto wa nyoka naye ni nyoka
 
Aisee kama kuna watu wenye lugha za kilaghai na akili zao zimetindikiwa tope ni hawa jamaa, ukiwa na akili angalau kidogo unaweza kutapika ukiwa sikiliza... yaaani huyu jamaa amejua tukio la CUF tu!? walichotakiwa kusema waseme, wanaona hawa fanyi sahihi lakini lazima watumikie mabwana zao mafisadi ili mkono uende kimywani... ukitaka kujua hawa jamaa wanauongo wa kitoto kiasi gani? jikumbushe tukio la mwangosi na kitu cha ncha kali. Aibu ya mwaka
 
Taratibu watu wanaanza kuelewa ninji maana ya kuwa na upinzani na haki zao ni zipi, ifike mahali hawa jamaa wakiwa na kichwa ngumu kwa kukilinda chama tgawala na kuwabana wapinzani tusiandamane bali tukusanye saini za watanzania wote wasiotaka polisi ccm na kumtaka polisi mkuu aachie ngazi, nina imani hiyo itafanya kazi na itawafungua akili hao vibaraka.
 
Huyu IGP mangu ana kazi kubwa ya kurudisha uhusiano uwe Ktk hali nzuri Kati ya polisi na raia, raia wanachukua kubwa sana kwa polisi maana baadhi ya askari wamekuwa wakinyanyasa na kuwaambia raia kesi....kwa hali hii hata polisi akikutwa na tatizo na anatakiwa kupewa msaada raia/wanachukua hawatompa
 
Mwandishi wa habari angemuuliza aliyemteua ni Mwenyekiti wa chama gani? na je anaweza kutoheshimu maelekezo ya chama cha aliyemteua? then ndio aendelee kutema hizo pumba nyingine.
 
Back
Top Bottom